A man stands in front of a herd of cattle with his back to the camera

“Ni Kama kuua Utamaduni”

Athari za Haki za Binadamu za Kuwahamisha Wamaasai wa Tanzania

Mwanaume mmoja akichunga mifugo yake kuelekea kwenye malisho na kutafuta maji katika wilaya ya Ngorongoro, mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Oktoba 25, 2019. © 2019 Nichole Sobecki / VII / Redux


 

Muhtasari

Mwaka 2021 serikali ya Tanzania ilikuwa imeshaweka mpango wa kuwahamisha takribani watu 82,000 wa jamii ya Kimaasai kutoka katika makazi yao na ardhi ya mababu zao katika mkoa wa Arusha eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kufikia mwaka 2027. Serikali ya kikoloni ya Waingereza ilianzisha NCA mwaka 1959, eneo linalotambulika kwa matumizi mtambuka na kuanzisha makazi ya kudumu ya watu waliokuwa wanaishi ndani na maeneo yanayozunguka bonde la Ngorongoro, wengi wao wakiwa ni wafugaji wa asili ya Kimasai.

Mwaka 2022, serikali ilianza mkakati wa kupunguza upatikanaji na ufikiaji wa huduma muhimu kwa wakazi wa eneo la NCA, ikiwa ni pamoja na kutokutoa fedha kwa taasisi zinazotoa huduma hizo. Wakati huo, huduma za kijamii katika eneo hilo tayari zilikuwa zimeshapunguzwa kwa kiasi kikubwa, zikipatikana kwa shida na kwa ujumla zikiwa na ubora duni ukilinganisha na zile zitolewazo maeneo mengine ya nchi.  Mamlaka pia zilichukua hatua za kuzuia wakazi, ambao wanategemea zaidi ufugaji kujipatia kipato, kulisha mifugo yao katika maeneo maalumu ya NCA.

Huku kukiwa na ushirikishwaji mdogo wa jamii za waathirika au wakati mwingine kutokuwepo kabisa, serikali imewahamisha na kwa mujibu wa mpango wake wa kuwahamisha, itaendelea kuwahamisha watu kutoka eneo la NCA kwenda Kijiji cha Msomera mkoa wa Tanga, wilaya ya Handeni takribani kilomita 600 kutoka NCA. Serikali imezipatia familia zilizohama kutoka NCA nyumba na heka mbili hadi tano za shamba kwa ajili ya kilimo, hii ni pamoja na kujenga na kukarabati barabara, shule za msingi, zahanati, ofisi ya posta, kituo cha polisi, mfumo wa usambazaji wa maji, umeme na minara ya huduma za simu kuhudumia Msomera.

Kati ya Agosti 2022 na Disemba 2023, Human Rights Watch ilifanya mahojiano na watu wapatao 100 – ikiwa ni pamoja na wakazi wa NCA wanaopaswa kuhama, wakazi wa zamani wa NCA ambao wamehamishiwa Msomera na wakazi wa Msomera walokuwepo toka awali --- na kugundua kuwa kile ambacho serikali ilikiita “mpango wa kuhama kwa hiari” kutoka eneo la NCA ni kinyume kabisa na hiari. Katika kutekeleza mpango huo, mamlaka zimetumia mbinu ambazo ni sawa na kuwafurusha watu kwa lazima jambo ambalo ni uvunjifu wa sheria na viwango vya haki za binadamu kimataifa. Kuwahamisha watu kwa lazima ni uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu zinazotambulika kimataifa, ikiwa ni pamoja na haki za binadamu kupata makazi yanayokidhi, chakula, afya, elimu, kazi, usalama wa mtu, uhuru dhidi ya ukatili, matendo yasiyokuwa ya kibinadamu, matendo ya kudhalilisha na uhuru wa kutembea. Katika kuwapatia makazi mapya wale waliohamishwa kutoka NCA, mamlaka pia zimewaondoa wakazi wa Msomera kwa kujenga majengo na miundombinu mingine na kuwapatia nyumba na maeneo ya kulima wale waliohamia katika ardhi ambayo tayari ilikuwa na wamiliki na ilikuwa ikitumika na wakazi waliokuwepo.

Kundi la wanawake na wanaume wa Kimasai wakiwa wamevalia mavazi na vito vya asili vya Kimasai karibu na Endulen, Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA), mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023.  © 2023 Human Rights Watch
Muonekana wa bonde la Ngorongoro katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA), mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023. © 2023 Human Rights Watch

Serikali haikutafuta ridhaa huru, ya wali na inayotokana na kuwa na taarifa sahihi (FPIC) kutoka kwa wakazi wa NCA ambao ni jamii ya Asili ya Wamasai. Viongozi wa kijamii walisema kuwa hawakushirikishwa ipasavyo kuhusu mpango wa serikali kuwahamisha, wala hakukuwa na namna ya kupata taarifa kuhusu masuala yahusuyo mchakato wa kuhama, malipo ya fidia, hali gani wategemee huko Msomera na wanakijiji gani walijiandikisha kuhama. Kukosekana kwa ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa sahihi kuna maanisha kuwa mamlaka hazijashughulikia wasiwasi wa wakazi na wakazi hawajapewa nafasi na kushauriana na mamlaka kupunguza madhara au kulinda haki zao, ikiwa watachagua kuhama kutoka NCA au kubaki.

Jambo linalowatia wasiwasi wakazi ni hatua za serikali zinazo walazimisha wakazi kuondoka NCA. Hii ni pamoja na kupunguzwa kwa huduma muhimu kama vile elimu na huduma za afya, vizuizi vya kuingia na kutoka katika eneo la NCA, kupunguza upatikanaji wa malisho, maji na maeneo ya kiutamaduni na maaskari wanyamapori walioajiriwa na serikali kuwashambulia na kuwapiga wakazi bila kuchukuliwa hatua.

Mamlaka hazikushauriana na wakazi wa Msomera kuhusu mpango wa kuwahamisha watu. Bila ya kupata maoni yoyote kutoka kwa jamii inayoathirika, serikali ilichora michoro na kujenga nyumba katika ardhi ambayo wakazi wa Msomera wamekuwa wakiishi na kulisha mifugo yao kwa miongo kadhaa, jambo ambalo linawalazimisha kuondoka katika maeneo hayo. Wakazi hawa wamezozana na familia mpya zilizohamia kutoka NCA kutokana na uhaba wa ardhi ya kulima na kufuga na ufinyu wa rasilimali nyingine. Wakati wale wakazi waliokuwa wakiishi Msomera hapo awali walipoandamana juu ya kunyang’anywa ardhi yao, mamlaka ziliwatishia kuwafukuza na kuwakamata.

Wamasai waliohama kutoka NCA kwenda Msomera, uamuzi ambao baadhi wanasema wameuchukua kutokana na vizuizi vya serikali ambavyo vimefanya maisha kuwa magumu mno, nao wanahangaika. Kizuizi kimojawapo ni kuwa mkuu wa kaya pekee, ambaye mara nyingi ni mwanaume, ndie anaeandikisha familia kuhama, kitendo kinachomuondoa mwanamke katika mchakato wa kufanya maamuzi. Kuacha huku kwa mwanamke kumepelekea mchakato wa kuhama ambao hauakisi uhalisia wa familia za Kimaasai, ambazo nyingi ni za mke zaidi ya mmoja, vizazi mchanganyiko na wanafamilia mchanganyiko. Vile vile, nyumba zilizotolewa na serikali hazikidhi mahitaji ya kiutamaduni na kaya nyingi kutokana na ukweli kuwa baadhi ya nyumba hizo ni ndogo sana kwa familia za kimaasai zenye vizazi mchanganyiko na wana kaya mchanganyiko. Huko Msomera, kila mwanaume ambaye ni mkuu wa kaya anapatiwa nyumba moja kwa ajili ya familia yake, lakini utamaduni wa Kimaasai hauruhusu wake kuishi katika nyumba moja na muwe wao. Hali hii inapelekea baadhi ya familia kutumia pesa kidogo ya fidia waliyolipwa na serikali kujenga nyumba zaidi ili kuwapatia wake na wanafamilia wengine na kuandaa ardhi kwa ajili ya mifugo yao. Baadhi ya waliohamishwa pia walionyesha wasiwasi wa kupata maji safi na salama ukilinganisha na ilivyokuwa NCA.

Ofisi ya Kijiji cha Mokilal, mamlaka ya serikai za mitaa, ikiwa haina paa katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023. © 2023 Mathias Rittgerott/Rainforest Rescue

Serikali imewanyamazisha wakosoaji wa mchakato wa kuwahamisha watu, jambo ambalo limechangia mazingira ya uoga miongoni mwa wakazi na watetezi wazawa wa haki za binadamu. Wakosoaji wengi wamekuwa kimya kwa kuogopa kulipizwa kisasi na mamlaka. Mamlaka zimewakamata wanaharakati wa kijamii na kuwakatalia asasi za kiraia kibali cha kuingia NCA. Human Rights Watch iligundua kuwa wale waliopewa vibali vya kuingia walifuatiliwa kwa ukaribu na askari wanyamapori wa serikali. Vizuizi hivi na hofu ya visasi vya serikali vimewazuia vikundi vya asasi za kiraia kutoa uelewa kuhusu mchakato wa kuhamisha na uvunjifu wa haki za binadamu dhidi ya jamii zilizoathirika.

Kupitia mchakato wake wa kuwahamisha watu, Tanzania imevunja haki kadhaa za Wamasai wakazi na jamii yao katika eneo la NCA na wakazi wa Msomera, kama ilivyoelezwa katika mikataba ya kikanda na kimataifa iliyoridhiwa na Tanzania, mikataba hii ni pamoja na Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu, Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR), na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (ICESCR). Wamasai na Watu wengine wa Asili pia wanalindwa na Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Watu wa Asili (UNDRIP). Sheria ya kimataifa ya haki za binadamu inalinda haki za Wamasai na haki nyingine za wanaoishi maeneo ya vijijini, miongoni mwao zikiwa, mali na ardhi, kushiriki, taarifa, uhuru wa kujieleza, uhuru wa kukusanyika, elimu na kiwango kikubwa kinachoweza kupatikana cha huduma za afya.

Jamii ya Wamasai waishio NCA wanalindwa na sheria mahususi za Tanzania, ikiwa ni pamoja na Sheria ya Hifadhi ya Ngorongoro ya mwaka 1959 na marekebisho yaliyofanyika, Sheria ya Utwaaji Ardhi ya 1967, Sheria ya Ardhi ya 1999 na Sheria ya Ardhi Vijini ya 1999, ambazo zote zinatambua hadhi yao wa kisheria ndani ya NCA, haki ya kumiliki ardhi kimila, mashauriano na fidia.

Serikali ya Tanzania haina budi kusitisha mara moja zoezi la kuwahamisha wakazi kutoka eneo la NCA. Mamlaka zinapaswa kufanya mashauriano yenye maana na jamii zinazoathirika katika eneo la NCA na kutafuta ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa sahihi kutoka kwa jamii ya asili walioathirika. Aidha wanapaswa kufanya mashauriano yenye maana na wakazi wa Msomera walioathirika. Wale watakaoridhia kuhama wanapaswa kulipwa fidia inayokidhi kulingana na ridhaa yao inayotokana na kuwa na taarifa sahihi.  

Serikali inapaswa kurejesha ufadhili na na rasilimali nyingine kwa ajili ya huduma za kijamii ambazo zimepungua au kuhamishwa kutoka eneo la NCA ikiwa ni uvunjifu wa haki za jamii zilizoathirika, ikiwa ni pamoja na elimu na huduma za afya. Pia inapaswa kuanzisha utaratibu mbadala unaojitegemea wa malalamiko na utatuzi ambao utashughulikia malalamiko na kutoa suluhu kwa ukiukaji wa haki za binadamu kuhusiana na uhamishaji huu. 

Boma za Wamasai katika asubuhi yenye ukungu katika kijiji cha Kayapus, Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA), mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023. © 2023 Human Rights Watch


 

Faharasa

Eneo La Hifadhi (GCA): Maeneo yaliyotengwa kwa mujibu wa Sheria za Tanzania ambayo Rais anaweza kuyatenga kwa ajili ya uhifadhi wa uoto wa asili, kulinda idadi ya wanyamapori, kukuza utalii na kuzalisha kipato kupitia shughuli za uwindaji unaosimamiwa. Tofauti na maeneo ya hifadhi za wanyama, katika maeneo ya GCA, watu wanaweza kuishi, kulima na kufuga mifugo bila vikwazo.

Watu wa asili: Haki za watu wa asili zinashughulikiwa katika viwango vya Umoja wa Mataifa na Afrika. Chini ya sheria ya kimataifa, watu wa asili ni wale walio kwenye vikundi vya kikabila na kiutamaduni wenye uhusiano wa kina na ardhi na rasilimali zao za asili. Wana haki tofauti zilizoelezwa katika Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Watu wa Asili, ikiwa ni pamoja na haki ya kujitawala, kudhibiti ardhi na rasilimali zao, na ulinzi wa utamaduni na lugha zao na serikali zinapaswa kuhakikisha kunapatikana ridhaa huru, ya awali na inayotokana na taarifa sahihi kuhusu uamuzi unaowaathiri.

Eneo la Matumizi Mtambuka: Katika muktadha wa uhifadhi nchini Tanzania, “eneo la matumizi mtambuka” ni eneo ambalo jitihada za uhifadhi zinapaswa kuzingatia shughuli endelevu za binadamu. Wanalenga kulinda uoto wa asili, makazi ya asili na wanyamapori huku ikiruhusu matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali na makazi ya binadamu.

Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (NCA): eneo la NCA, linalopakana na tarafa ya Ngorongoro, ni eneo linalotunzwa na eneo la UNESCO la Urithi wa Dunia linalopatikana kaskazini mwa Tanzania katika wilaya ya Ngorongoro.

Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro (NCAA): NCAA ni shirika la umma chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii iliyoundwa kwa ajili ya kusimamia NCA.

Baraza la Wafugaji Ngorongoro (Baraza la Wafugaji): Baraza la Wafugaji, ambalo lilitambulika kisheria mwaka 2000, linafanya kazi kama chombo cha kati kinachounganisha jamii ya watu wanaoishi NCA na NCAA. Kinahusisha wawakilishi kutoka Kata na Vijiji vya NCA, linatoa ushauri kwa Bodi ya Wakurugenzi ya NCAA na lina mamlaka ya kuanzisha na kupendekeza miradi kwa ajili ya kuidhinishwa na NCAA kama vile ufadhili wa wanafunzi, ujenzi wa majengo ya shule na uchimbaji wa visima na mabwawa.


 

Mapendekezo Muhimu

Kwa Serikali ya Tanzania

Juu ya Ulinzi wa Umiliki wa Ardhi

  • Kuheshimu haki za binadamu, pamoja na haki za ardhi na umiliki, ikiwa ni pamoja na ardhi inayomilikiwa kimila na jumuiya, ya watu wa Asili na wengine wenye haki katika kuendeleza na kutekeleza mipango yote ya uhifadhi.

    • Kutambua kisheria ardhi na rasilimali ambazo jamii za wafugaji katika wilaya ya Ngorongoro zimetumia na kusimamia vizazi kwa vizazi, kwa kuheshimu mifumo ya kisheria, mila na desturi zao, pamoja na njia za kitamaduni za malisho na matambiko.

Juu ya Ridhaa Huru, ya Awali na Inayotokana na Taarifa sahihi na Ushirikishwaji

  • Kuwashirikisha kikamilifu na kutafuta ridhaa huru, ya awali na inayotokana na taarifa sahihi kutoka kwa jamii ya Asili walioathirika katika eneo la NCA na kufanya mashauriano yenye maana na wakazi wa Msomera waliokuwepo toka enzi na walioathirika na mchakato wa kuhamishwa watu kwa kuzingatia wajibu wa kitaifa na kimataifa.

    • Kuwapatia jamii zote zilizoathirika taarifa muhimu kuhusu mapendekezo ya mikakati ya uhifadhi na maendeleo ambayo itaathiri maisha yao kama watu binafsi na kama jamii.

    • Kuhakikisha ushiriki wa wanajamii wote wanaoathirika katika kufanya maamuzi yanayohusiana na ardhi na maliasili, ikiwa ni pamoja na michakato inayohusisha vijana na kuzingatia jinsia katika kuamua mikakati ya uhifadhi ambayo inaheshimu na kulinda haki zao.

Juu ya Elimu na Afya

  • Kulinda haki za Wamasai kupata elimu, viwango vikubwa vya huduma za afya, maji na usafi wa mazingira, makazi yanayokidhi, chakula na kushiriki katika maisha ya utamaduni katika eneo la NCA.

  • Kurejesha nafasi za ajira kwa watumishi wa afya wanaolipwa na serikali katika vituo vya afya, ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Endulen na zahanati nyingine katika eneo la NCA.

Juu ya Askari Wanyamapori wa NCAA

  • Kuhitaji na kuhakikisha kuwa askari wanyamapori wanapata mafunzo sahihi kuhusu sheria na viwango vya kitaifa na kimataifa vya haki za binadamu na kuwa na usimamizi huru na kuwajibika.

Juu ya Taratibu za Ufuatiliaji na Malalamiko

  • Kufanya ufuatiliaji endelevu na kusitisha utekelezaji wa mikakati ya uhifadhi inayokiuka haki kama vile maeneo ya hifadhi au uhamishaji wa lazima unaohusiana na uhifadhi na uhamishaji usio wa hiari.

  • Kuweka utaratibu mbadala ambao ni huru wa kushughulikia malalamiko na utatuzi ambao utapokea malalamiko na kutoa suluhu kwa uvunjifu wa haki za binadamu unaohusiana na kuhamishwa kwa wakazi kutoka eneo la NCA kuhamia Msomera.

Kwa Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro

  • Kurejesha ufadhili kwa huduma na kutunza miundombinu iliyopo katika eneo la NCA, ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Endulen na shule, kurejesha na kuimarisha Baraza la Wafugaji Ngorongoro na kuhakikisha hakuna vikwazo kwa Baraza la Wafugaji kutekeleza majukumu yake.

  • Kushauriana na wawakilishi wa jamii ikiwa ni pamoja na Baraza la Wafugaji kuanzisha miongozo ya wazi kuhusu vibali vya ujenzi na vifaa vya ujenzi vinavyoruhusiwa, kwa mfano vile vinavyopatikana katika mazingira yale yale, ambavyo vyanzo vyake ni endelevu na vina umuhimu kiutamaduni kwa jamii.

  • Kubuni mfumo ulio wazi, kwa kushirikisha wawakilishi wa jamii ya NCA, ambao utaondoa au kupunguza mzigo wa kulipa ada ya kuingia kwa wakazi wa NCA ambao hawana vitambulisho vinavyowaruhusu kuingia getini na kutoa njia nyepesi ya kuingia kwa wanajamii hawa wa asili.

  • Kuanzisha mikakati ya uhifadhi inayoheshimu haki na viwango na utaratibu wa utekelezaji ulio wazi unaoshirikisha wanajamii wa NCA katika mchakato.

    • Kushirikiana na jamii ya NCA kuandaa mpango wa vyanzo endelevu vya chakula na maji ambavyo vinakubalika kitamaduni, vitakavyowasaidia kimaisha na kuhakikisha wana usalama wa chakula.

  • Kutekeleza mpango wa muda mrefu wa ufuatiliaji na tathmini unaoongozwa na wanajamii kwa kuelewa kwamba mipango ya kuhamisha watu inahitaji usaidizi na usimamizi wa muda mrefu.

  • Kuongeza muda wa kutoa msaada kwa familia ambazo zimehamishwa kutoka NCA na kuwalipa fidia kulingana na ridhaa yao inayotokana na kuwa na taarifa.

  • Kuwaruhusu wakazi kurudi NCA, ikiwa watajisikia kufanya hivyo na kuwawezesha kurudi ikiwa ni pamoja na kuwapa msaada wa kifedha kujenga nyumba zao na kununua mifugo.

  • Kufanya uchunguzi kuhusu udhalilishaji unaofanywa na askari wanyamapori wa NCAA katika eneo la NCA, ikiwa ni pamoja na vikwazo vya kutembea na kuwawajibisha kupitia mifumo sahihi ya nidhamu na mahakama.


 

Mbinu za Utafiti

Ripoti hii inatokana na utafiti uliofanywa na Human Rights Watch nchini Tanzania maeneo ya Dar es Salaam; Arusha, kijiji cha Endulen kilichopo katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (NCA), Mto wa Mbu na vijiji vya Karatu mkoa wa Arusha; na Kijiji cha Msomera na mji wa Handeni, wilaya ya Handeni, mkoa wa Tanga kati ya Agosti 2022 na Disemba 2023.

Human Rights Watch ilifanya mahojiano na takribani watu 100, ikiwa ni pamoja na wanawake 37, wanaume 57 kwa ajili ya ripoti hii. Waliohojiwa ni mchanganyiko wa wanajamii wa NCA ambao wanakabiliwa na zoezi la kuhamishwa na wale waliohamishwa kwenda Kijiji cha Msomera, wakazi wa Kijiji cha Msomera waliokuwepo tangu awali, watumishi wa serikali, wawakilishi wa taasisi zisizo za kiserikali (NGOs) na wanaharakati wa ndani.

Human Rights Watch ilifanya mahojiano ana kwa ana na kwa njia ya simu. Mahojiano ya ana kwa ana yalihusisha mahojiano ya mtu mmoja mmoja na mahojiano ya kikundi cha watu kati ya wawili na wanne, isipokuwa katika kikao kimoja ambapo kulikuwa na watu 10. Mahojiano ya kikundi cha watu 10 huko Endulen, NCA ni matokeo ya vikwazo vya kutembea ndani ya NCA, kufuatiliwa na askari wanyamapori wa NCAA, hofu ya kugunduliwa na kupunguza uwezekano wa wakazi kutambuliwa na uwezekano wa visasi dhidi yao kutoka kwa serikali kwa wanajamii waliozungumza na Human Rights Watch. Human Rights Watch ilifanya mahojiano kwa kutumia lugha ya Kiingereza, Kiswahili na Maa, kwa usaidizi wa wakalimani kadri ilivyohitajika.

Mahojiano yalifanyika katika mazingira yenye faragha au kwa njia ya mtandao kupitia mifumo salama ya mawasiliano. Human Rights Watch iliwajulisha washiriki wote dhumuni la mahojiano, uhalisia wake kuwa ni ya hiyari, namna taarifa zitakavyotumika na kwamba wanaweza kukataa kushiriki au kusimamisha mahojiano wakati wowote. Kila mshiriki aliridhia kwa maneno. Human Rights Watch haikuwalipa waliohojiwa au kutoa motisha yoyote kwa kushiriki.

Ripoti imetumia majina bandia na kuficha utambulisho kulinda waliohojiwa dhidi ya uwezekano wa kufanyiwa visasi na mamlaka za serikali.

Pamoja na mahojiano, Human Rights Wach pia ilifanya mapitio ya nyaraka za kisheria, ikiwa ni pamoja sheria, kanuni za wizara, maamuzi ya mahakama na nyaraka nyingine zinazohusiana na NCA na haki za ardhi nchini Tanzania. Human Rights Watch pia ilipitia vyanzo vingine vya taarifa ikiwa ni pamoja na ripoti za NGO, ripoti za taasisi za utafiti na Makala za vyombo vya Habari.

Mei 10, 2024 Human Rights Watch iliandika barua kwa Wizara za Maliasili na Utalii, Afya, Elimu na Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto; Ofisi ya Rais – Kazi Maalumu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Jeshi la Polisi la Tanzania, na kwa Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro (NCAA), kuwashirikisha katika matokeo ya utafiti na kuwaomba taarifa lakini hakukuwa na majibu yoyote.


 

Historia

Juhudi za Tanzania Kuboresha Taswira yake

Samia Suluhu Hassan amekuwa Rais wa kwanza mwanamke Tanzania mnamo Machi 19, 2021 akimpokea Rais John Magufuli ambaye alifariki dunia Machi 17, 2021.[1]  Kuzorotoa kwa misingi ya kuheshimu haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na serikali kufungia vyombo vya habari, NGOs, wapinzani wa kisiasa na wakosoaji wengine wa serikali ndio alama ya uongozi wa Rais Magufuli.[2] Muda mfupi baada ya Suluhu Hassan kuchukua ofisi, aliahidi kushughulikia masuala ya haki za binadamu na kuchukua hatua ya kuondoa vikwazo vya uhuru wa kujieleza na kukusanyika, kama vile kuondoa marufuku ya miaka sita ya mikutano ya kisiasa kwa vyama vya upinzani, na kuvifungulia vyombo vinne vya habari.[3] Hata hivyo, vikwazo kwa vyombo vya Habari na raia, na kukamatwa kiholela kwa waandishi wa habari na wakosoaji wa serikali kumeendelea.[4]

Rais Suluhu Hassan ameongoza kampeni ya kukuza utalii nchini Tanzania kufuatia kudorora kwake kipindi cha uongozi wa Rais Magufuli na janga la UVIKO-19.[5] Kampeni hiyo ililenga kuvutia watalii wa kimataifa kutembelea Tanzania kwa kutangaza fukwe zake, wanyamapori, milima na urithi wa kitamaduni. Katika filamu ya “The Royal Tour”, ambayo ilirushwa katika Huduma za Matangazo ya Umma (PBS) nchini Marekani mwezi Aprili 2022,[6] Rais Suluhu Hassan aliwapeleka watengeneza filamu katika utalii kwenye Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro, Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (NCA), Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na hifadhi ya asili ya Mkomazi, miongoni mwa nyingine.[7]

Taratibu za Asili za Wamasai na Uhifadhi

Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu imeweka vigezo vinne muhimu vya kutambua watu wa asili: “kazi na matumizi ya eneo maalum; uendelezaji wa hiari wa upekee wa utamaduni; kujitambua kama mkusanyiko tofauti na kutambuliwa hivyo na makundi mengine; uzoefu wa kukandamizwa, kutengwa, kunyang’anywa mali, kutokushirikishwa au kubaguliwa.”[8] Tume inaeleza kuwa “jambo moja ambalo linaonekana katika vigezo mbalimbali vinavyojaribu kuwaelezea watu wa asili – kwamba watu wa asili wana mahusiano yasiyo na utata na eneo maalum na kwamba majaribio yote ya kuelezea dhana hii yanatambua uhusiano uliopo baina ya watu, ardhi yao na utamaduni.”[9]

Wamasai ni watu wa asili ambao,[10] sambamba na makundi mengine ya kikabila wamekuwa wakiishi katika ardhi ya Ngorongoro iliyoko kaskazini mwa Tanzania vizazi kwa vizazi.[11] Wanalima mahindi, maharage, maboga na viazi vitamu na wanafuga ng’ombe, kondoo na mbuzi ambao wanahitaji eneo kubwa la malisho. Kwa sababu Wamasai wanajitahidi kuishi kwa amani na wanyamapori, mila zao zinakuza uhifadhi ya maliasili.[12] Mila hizo zinakataza matumizi ya nyamapori – nyama kutoka kwa wanyama wa porini- badala ya nyama kutoka kwa ng’ombe zao; na kwamba matawi ya mti na sio mti mzima ndio hukatwa kwa ajili ya matumizi. Zaidi ya hayo, kanuni za kijadi za Wamasai katika kusimamia maeneo ya malisho ni pamoja na vipindi vya kulima, malisho yaliyopangwa kwa msimu na mifumo ya uhamaji wa wanyamapori.

Kwa karne nyingi Wamasai wamechangia kuwepo kwa mazingira yanayochochea muingiliano wenye faida na maelewano kati ya wafugaji, mifugo na wanyamapori.[13] Matendo yao ya kitamaduni na kiroho ikiwa ni pamoja na mila za kuwatambua vijana kama watu wazima zimeoanishwa na ardhi yao, na maeneo matakatifu ya kukusanyika kuwafundisha vijana wa Kimasai kuhusu utamaduni wao na namna ya kuishi na mazingira yanayowazunguka.

Matumizi Mtambuka ya Ardhi ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro

Wakati mamlaka ya kikoloni ya Uingereza ilivyotangaza eneo la Serengeti kuwa hifadhi ya Taifa mwaka,[14] jamii zilizokuwa zinaishi ndani ya eneo hilo zilihamishiwa Ngorongoro kwa makazi ya kudumu. Kwa kuzingatia mikataba iliyoingiwa baina ya Wamasai ambao hapo awali walikuwa wakiishi na kutumia eneo la Serengeti na serikali ya kikoloni, serikali ilianzisha Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro mwaka 1959 ili kuwa na makazi ya kudumu kwa watu walioishi ndani na maeneo yanayozunguka bonde la Ngorongoro, wengi wao wakiwa ni wafugaji wa Kimasai.[15] NCA ilianzishwa kama eneo la matumizi mtambuka, huku wafugaji Wamasai wakiishi pamoja na wanyamapori.[16]

Eneo la Urithi wa Dunia la Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni tangu mwaka 1979, NCA ina ukubwa wa ardhi upatao hekari 809,440 unaohusisha maeneo makubwa ya uoto wa asili, misitu na bonde la Ngorongoro.[17] Inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na ni sehemu ya mfumo wa ikolojia wa Serengeti-Mara unaofanya kazi kama njia muhimu ya wanyamapori kuwalinda wanapohama.[18]

Ramani na taarifa za watalii katika geti la Loduare la Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA), mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023.  © 2023 Human Rights Watch

Muundo wa Utawala wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro

Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro (NCAA) iko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Mhifadhi au Kamishna wa Uhifadhi na Wakurugenzi wa Bodi wana majukumu ya kusimamia NCAA.[19] Kamishna wa Uhifadhi anateuliwa na Rais wa Tanzania na wakurugenzi wa bodi wanateuliwa na Waziri wa maliasili na utalii.[20]

Ijapokuwa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro liko katika wilaya ya Ngorongoro, kwa mujibu wa Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, kamishna wa uhifadhi wa NCAA chini ya Waziri wa maliasili na utalii ana mamlaka ya msingi na wajibu wa kusimamia Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro

NCAA ni taasisi ya umma inayosimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii ambayo inasimamia NCA.[21] Kuna kata 11 eneo la NCA ambazo zimegwanyika katika vijiji 25, 16 kati hivyo vina namba rasmi za usajili. Vijiji hivi vimepimwa, kuwekwa mipaka na kusajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 1982 ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro.[22] Kamishna wa Ardhi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametenga vijiji 18 kwa ajili ya kupimwa, kutengenezewa ramani na kurasimishwa kama ardhi ya Kijiji kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji yam waka 1999.[23] Kwa mujibu wa sensa ya Tanzania yam waka 2022, idadi ya watu NCA inakadiriwa kuwa 100,793.[24]

Tangu kuanzishwa kwake, NCA imeunganisha uhifadhi na maendeleo ya binadamu.[25] Mpango Mkuu wa Usimamizi wa NCAA, ambao uliandaliwa mwaka 1996 una lengo kuu la kuhifadhi maliasili za NCA, kulinda maslahi ya wafugaji Wamasai na kukuza utalii.[26]

Kwa kipindi kirefu, serikali ya Tanzania, Kamati ya Urithi wa Dunia ya UNESCO, ambayo hutoa tafsiri ya mamlaka ya Mkataba wa Urithi wa Dunia wa UNESCO,[27] na bodi zake za ushauri,[28] Umoja wa Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira (IUCN), Baraza la Kimataifa la Makumbusho na Maeneo (ICOMOS), na Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Uhifadhi na Urejeshaji wa Mali za Kitamaduni (ICCROM), mashirika matatu ya kimataifa yaliyotajwa kwenye Mkataba yameeleza ongezeko la idadi ya watu na mifugo katika eneo la NCA kama suala la kuangaliwa.[29] Taasisi hizi zilieleza kuwa kutakuwa na ongezeko la mahitaji ya ardhi na rasilimali jambo ambalo lingeleta shinikizo kubwa nap engine kuvuruga mfumo wa ikolojia.[30] Wasiwasi huu hatimaye ulipelekea wito kutoka Kituo cha Urithi wa Dunia cha UNESCO na bodi zake za ushauri kuitaka serikali kupitia upya Mpango Mkuu wa Usimamizi,[31] na mapendekezo ya “kuhimiza jamii kuhama kwa hiari, kunakoendana na sera ya Mkataba na taratibu zinazokubalika kimataifa kutoka ndani ya eneo kwenda nje kufikia mwaka 2028.”[32]

Human Rights Watch haijatoa uamuzi kuhusu uhalali wa mashaka kuhusu ongezeko la binadamu na mifugo katika eneo la NCA. Hata hivyo, hata ikiwa kuwa wasiwasi huo ni kweli, kushughulikia wasiwasi huo hakuwezi kutumika kama sababu ya uvunjifu wa haki za binadamu, n ani muhimu serikali kuzishirikisha jamii zinaoishi katika eneo la NCA kutafuta njia mbadala zinazoheshimu haki kwa ajili ya kulinda maisha yao ya asili katika eneo la NCA.

Serikali ilianzisha Baraza la Wafugaji wa Ngorongoro mwaka 1994 na kuanza kazi mwaka 2000.[33]    Baraza la Wafugaji linajumuisha wawakilishi kutoka Halmashauri ya Kijiji na Kamati ya Maendeleo ya Kata, ambao ni pamoja na madiwani wa kata, wenyeviti wa vijiji, wanawake, vijana na viongozi wa kimila.  Baraza la Wafugaji huandaa na kupanga utekelezaji wa miradi kwa lengo la maendeleo ya wafugaji ndani ya eneo la NCA.[34] Huwasilisha miradi iliyopendekezwa kwa NCAA, na NCAA hutoa fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika mwaka husika wa fedha kwenda kwa Baraza la Wafugaji kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake.[35] Baraza la Wafugaji pia linashauri Bodi ya Wakurugenzi ya NCAA kuhusu miradi ya maendeleo katika eneo la NCA, kama vile wakati wa kupanga na kujenga hoteli na maeneo mapya ya kuweka kambi.

Kwa mujibu wa mawasiliano ya serikali ya Aprili 2022 kwa Tawi la Utaratibu Maalum la Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa UN (OHCHR):

Baraza la Wafugaji lina kazi zifuatazo: (i) Kuangalia mahitaji ya jamii ya wafugaji waishio NCA. (ii) Ni chombo cha ushauri kwa bodi ya wakurugenzi ya NCAA juu ya maendeleo ya wakazi na masuala ya uhifadhi NCA. (iii) Kuhakikisha kuwa vyombo vingine kama vile serikali ya Kijiji na kamati ya maendeleo ya kata vinapewa nafasi ya kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na changamoto zinazokabili jamii ya NCA. (iv) Kushirikiana na wadau wengine hususan NCAA, wafadhili, mashirika ya serikali na yale yasiyokuwa ya kiserikali, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na mamlaka nyingine za wilaya (wilaya jirani) katika kutekeleza majukumu yake. (v) Kutekeleza kazi za baraza na sera zake kama zilivyoidhinishwa na bodi ya wakurugenzi ya NCAA. (vi) Kutambua vikwazo vya maendeleo ya wakazi na kutengeneza mikakati ya kutatua changamoto hizo kwa kushirikiana na wadau wengine.[36]

Baraza la Wafugaji lilikuwa linatoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa shule na vyuo, na kujenga shule za msingi, visima na mabwawa mpaka NCAA ilipoacha kutoa fedha mwanzoni mwa mwaka 2019.[37]

Serikali ya Tanzania na NCAA tangu mwaka 1975,[38] zimekuwa zikionyesha mashaka juu ya kuongezeka idadi ya binadamu na mifugo ndani ya eneo la NCA kuhalalisha vikwazo kwa wanajamii na mifugo kufika maeneo ambayo NCAA inayaona ni ya kipaumbele, ikiwa ni pamoja na bonde la Ngorongoro, eneo linalozunguka bonde na hifadhi yam situ ya nyanda za juu kaskazini.[39] Vile vile walipiga marufuku kilimo – kilichoondolewa baada ya muda kupita,[40] na kutenga maeneo tofauti ya makazi ya binadamu na wanyamapori. Mwaka 2021, serikali iliandaa mpango wa kuwahamisha takribani wakazi 82,000 kutoka eneo la NCA kufikia 2027.[41]

Wamasai Kuhamishwa na Kuondolewa kwa lazima hapo Awali

Tangu mwaka 2022, serikali imekuwa ikitekeleza mpango wa kuhamisha familia za Wamasai wanaoishi eneo la NCA kwenda Kijiji cha Msomera, wilaya ya Handeni, mkoa wa Tanga, ambao upo kilomita 600 mashariki mwa Ngorongoro. Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Albert Msando, Msomera ilichaguliwa kwa sababu “ni eneo ambalo bado ni pori lenye ardhi kubwa ambayo bado haijaingiliwa na shughuli za kilimo, hali ambayo inarahisisha upangaji wa shughuli za ufugaji,” na kuongeza kuwa jamii nyingine za wafugaji Wamasai zilikuwa tayari zinaishi Msomera.[42]

Hii sio mara ya kwanza serikali imewahamisha watu kutoka eneo la NCA. Kati yam waka 2007 na 2010, NCAA ilihamisha familia 159 kutoka NCA kwenda Kijiji cha Jema, tarafa ya Sale, wilaya ya Ngorongoro.[43]  Ijapokuwa serikali iliweka miundombinu ya husuma za kijamii ikiwa ni pamoja na shule ya msingi, zahanati, kituo cha polisi na mabomba ya maji, serikali ilisisitiza kuwa zoezi hilo halikuwa na mafanikio.[44] Zaidi ya asilimia 50 ya wakazi waliohamishwa wakati huo wamerudi NCA au katika maeneo mengine nchini.[45]  Mwaka 2019, familia zipatazo 50 hadi 70 ambazo zilibaki katika makazi mapya zilikabiliwa na upinzani kutoka kwa jamii iliyowapokea na wamekuwa wakipanga kuondoka katika eneo hilo pia.[46]

Wamasai Kufukuzwa katika maeneo mengine ya Wilaya ya Ngorongoro

Kaskazini mwa NCA katika tarafa ya Loliondo, wilaya ya Ngorongoro, serikali imeanza operesheni kadhaa za kuwaondoa kwa nguvu jamii ya Wamasai kutoka katika baadhi ya vijiji vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti licha ya pingamizi kutoka kwa jamii, ukosoaji mkubwa wa kimataifa, na zuio la mahakama dhidi ya kuwaondoa la mwaka 2018.[47]

Juni 6, 2022, serikali ilitangaza kuwa itabadilisha kilomita za mraba 1,500 za ardhi ya Kijiji katika eneo la hifadhi kuwa eneo maalum linalodhibitiwa [48], jambo ambalo litawazuia wakazi ambao ni jamii ya Wamasai wafugaji kuishi na kuendelea kutumia ardhi kama walivyokuwa wanatumia awali. Siku mbili baadaye, makumi ya askari polisi, wanajeshi na askari wanyamapori walifika Loliondo kuweka mipaka katika eneo la hifadhi maalumu linalodhibitiwa

Human Rights Watch iligundua kuwa katika siku kadhaa, vikundi vya ulinzi vilifyatua mabomu ya machozi na risasi za mpira kwa waandamanaji na mashuhuda, na kujeruhi angalau watu 30 ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto na wazee na pia waliwakamata watu kiholela na kuwaweka kizuizini viongozi 10 wa kijamii. Baada ya Juni 2022, mamlaka zilianza kutumia vitendo vya unyanyasaji kinyume cha sheria ikiwa ni pamoja na kuunguza nyumba zilizo ndani ya mipaka ya eneo lililotengwa la hifadhi, kuwapiga, kuwafyatulia risasi, kuwakatili kijinsia na kuwakamata kiholela ili kuwaondoa kwa nguvu wakazi katika ardhi yao.[49]


 

Wamasai Kuondolewa kwa Nguvu kutoka Hifadhi ya Eneo ya Ngorongoro

Serikali imetuleta hapa, na nimekuja kutokana na usumbufu na manyanyaso niliyokuwa nikipata pale Ngorongoro. Huwezi kujenga, kulima au kuendesha pikipiki, hivyo tukaamua kuondoka.


–Mary I., Msomera, Aprili 11, 2023

Kwa mujibu wa ripoti ya 2019 ya Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi (MLUM) ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, uhamishaji wa watu hapo awali haukufanikiwa, [50] lakini mamlaka zimeendelea na mipango mipya ya kuhamisha watu.   

Mnamo Juni 16, 2022, serikali ilianza zoezi la kuwahamisha Wamasai kutoka NCA kwenda Kijiji cha Msomera, mkoa wa Tanga. Makadirio ya serikali yanaonyesha kuwa takribani kaya 551, zenye watu 3,010 na mifugo 15,321 wamehamishwa kufikia Januari 2023.[51] Msando aliwaambia Human Rights Watch kuwa tofauti na yaliyotokea kwenye zoezi la kuwahamisha kwenda tarafa ya Sale kati yam waka 2007 na 2010,[52] serikali imefanya jitihada ya kuratibu kwa kushirikiana na serikali za mitaa za kila mkoa, ikiwa ni pamoja na NCAA, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.[53]

Hata hivyo, mipango na utekelezaji wa serikali vimeshindwa kuhakikisha mamlaka zinapata ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa (FPIC) kutoka kwa wanajamii. Mpango wa serikali wa kuwahamisha maelfu ya wafugaji wa Kimasai kutoka katika ardhi waliyoimiliki na kuitumia vizazi kwa vizazi ulipaswa kufuata utaratibu wa FPIC kwa serikali kupata ridhaa kutoka kwa waathirika ambao ni Watu wa Asili, ridhaa huru na inayotokana na kuwa na taarifa kabla ya mpango wa kuwahamisha haujapitishwa na kabla ya kuanza kuutekeleza. Jamii ya Wamasai iliyoathirika haikuhusishwa katika kuandaa na wala katika kupitisha mpango huo. Zaidi, serikali haijatoa taarifa za kutosha na kufanya mashauriano na jamii husika kuhusu mpango wa kuwahamisha kutoka NCA kwenda Kijiji cha Msomera.

Mamlaka pia zinasukuma familia za Wamasai katika eneo la NCA kuondoka bila ridhaa yao kwa kukiuka haki zao za kibinadamu. Wamepunguza upatikanaji na ufikiwaji wa bidhaa na huduma muhimu kwa haki za kibinadamu za wakazi kwa kupunguza ufadhili katika vituo vya elimu na afya. Wamezuia uhuru wa wakazi kutembea na kufika katika ardhi za mababu zao ambazo zina maeneo ya kiutamaduni na malisho muhimu maisha yao. Askari wanyamapori wa NCAA wamekuwa wakiwapiga na kuwadhalilisha wakazi wa NCA ambao hawatii sheria za serikali kama ilivyoandikwa hapa chini.[54] Matokeo yake, baadhi ya wakazi walisema hawakuwa na namna bali kuondoka NCA. Vitendo hivi ambavyo vimetumika na mamlaka kuwaondoa wakazi katika eneo la NCA vinavunja haki kadhaa za wakazi wa NCA na kwa pamoja ni saw ana uondoshaji wa lazima ambao ni uvunjifu wa wajibu wa Tanzania katika Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni.[55]

Mchakato Hafifu wa kupata Ridhaa Huru, ya Awali na inayotokana na kuwa na Taarifa

Kupata ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa (FPIC) ni sehemu ya haki ya ujumla ya kujitawala na haki mahususi ya watu wa Asili inayoendana na sheria na viwango vya kimataifa.[56] FPIC inahakikisha kuwa watu wa Asili wana uhuru wa kuamua hali yao ya kisiasa na kuendeleza shughuli za maendeleo za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.[57] Inawaruhusu watu wa Asili kukubali au kukataa kutoa ridhaa kwa mradi ambao unaweza kuwaathiri wao au maeneo yao. Pale wanapotoa ridhaa yao, wanaweza kuiondoa muda wowote. Zaidi pia, FPIC inawawezesha watu wa Asili kujadili namna ambavyo maendeleo yanayoathiri ardhi, maeneo, na rasilimali ambazo wamekuwa wakizimiliki au kutumia zitakavyotumika, kutathminiwa na kufuatiliwa. FPIC imejikita katika mashauriano yenye maana kupitia taasisi au muundo wa uwakilishi wa watu wa Asili (bila ya shuruti, vitisho, au ghiliba); mapema kabla ya kupata idhini au kuanza kwa shughuli; na kupata taarifa zote kuhusu shughuli zitakazofanyika, sera au mradi ambao utaathiri watu wa Asili na ardhi yao.[58]  Haipaswi kuwahamisha watu wa Asili kutoka katika ardhi au maeneo yao bila ya kupata ridhaa yao ambayo ni huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa na baada ya kukubaliana juu ya fidia sahihi na ya haki na pale inapowezekana kuwe na chaguo la kuamua kurudi .[59]

Utafiti na uchambuzi wa Human Rights Watch uligundua kuwa serikali ya Tanzania haijatekeleza mpango wowote wa kuhakikisha inapata ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa kutoka kwa Wamasai katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Mashauriano Hafifu

Kwa kuzingatia vipengele vya FPIC: mchakato wa kushauriana, muda na muundo wa kufanya maamuzi unapaswa kuongozwa na jamii inayoathirika. Hii inamaanisha, mikutano na maamuzi yanafanyika katika maeneo, muda, lugha na mfumo unaoamuliwa na jamii inayoathirika; wanajamii wote wana uhuru wa kushiriki bila kujali jinsia, umri au nafasi katika jamii; na jamii ya waathirika inabidi iwe na uwezo wa kushiriki kupitia wawakilishi waliowachagua wenyewe bila shinikizo, huku wakizingatia ushiriki wa vijana, wanawake, wazee na wenye ulemavu kwa kadri iwezekanavyo.[60] 

Kiongozi wa kimila ameeleza kile anachokiana kama mashauriano yenye maana:

Mashauriano sio kujulishwa pekee. Ni kitu ambacho tunapaswa sote kukaa chini na kufanya uchambuzi wa masuala yote: ufugaji, maendeleo, utalii…vitu vinavyogusa watu wote. Haitoshi kwa sisi viongozi pekee kukutana: tunahitaji kukutana na jamii. Serikali iseme inachotaka na sisi tuseme tunachotaka na kwa pamoja tunajadili yote hayo.[61]

Kinyume na matakwa ya mchakato wa FPIC, serikali haikushauriana na jamii ya wanaoathirika kabla ya kuandaa mpango wa kuwahamisha. Mwaka 2018, serikali ilipitia Mpango wa NCA wa Matumizi Mtambuka ya Ardhi na kupendekeza kutenga maeneo kutokana na shughuli zinazoruhusiwa kama vile makazi, malisho na mengineyo kukiwa na uwezekano wa kuwahamisha watu.[62] Wakazi wa NCA ikiwa ni pamoja na viongozi wa kijamii waliwaambia Human Rights Watch kuwa serikali haikufanya mashauriano ya kutosha na jamii inayoathirika wakati na baada ya kufanya mapitio hayo. Baada ya serikali kuchapisha ripoti ya mapitio yake mwaka 2019, wakazi na NGO zinazofanya kazi na jamii ya NCA walitoa ripoti yao ya kijamii mwezi Mei, 2022 iliyopinga baadhi ya matokeo ya ripoti ya serikali na kuiwasilisha serikalini.[63]  Hata hivyo, viongozi wa jamii wanasema serikali ilikataa kuangalia ripoti yao na mapendekezo yake yanayopendekeza mbadala wa kuhama.[64]

Wakazi wanasema serikali iliamua kuhusu “kuhama kwa hiari”, eneo ambalo watu watahamishiwa, na kujenga nyumba bila ya kupata maoni kutoka kwa jamii inayoathirika au viongozi wao. Diwani wa Kijiji kutoka wilaya ya Ngorongoro alieleza wasiwasi wake juu ya ukosefu wa uwazi: “serikali ilifanya mambo kwa usiri na kuchagua Msomera na kujenga zaidi ya nyumba 100 kwa siri.”[65]

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikutana na viongozi wa kijamii, pamoja na madiwani wa Kijiji Februari 17, 2022 kwa ajili ya kuzungumzia mpango wa kuwahamisha watu kutoka NCA. Diwani wa Kijiji aliyeshiriki mkutano huo anasema washiriki walifikiri mkutano huo uliitishwa ili kupata maoni na walitoa njia mbadala wa kuwahamisha watu lakini Waziri Mkuu alikuja pale kwa ajili ya kutoa maelekezo ya namna ya kujisajili kwa ajili ya kuhamishwa.[66]

Kiongozi wa kimila eneo la NCA alielezea mkutano huo:

Haukuwa mkutano wa mashauriano kwa sababu alizungumza na kuondoka. Hakukuwa na kuchukua maoni wala kusikiliza mawazo ya watu. … Waziri Mkuu alitembelea eneo hili; watu wengi walienda, lakini hawakuruhusiwa kuingia. Alichagua watu wachache – watendaji wa kata na vijiji – kisha akasema alichokuwa nacho na kuondoka.[67]

Kiongozi mwingine wa kimila, Mjumbe wa Baraza la Wafugaji, alisema kwamba mashauriano yoyote ya serikali na jamii ikiwa ni pamoja na mkutano na Waziri Mkuu vilikosa ushiriki mzuri wa viongozi na jamii kwa ujumla.[68]

Utawala Ngazi ya Wilaya:

Wilaya ya Ngorongoro inaundwa na tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sale. Kila tarafa hugawanywa kwenye kata. Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, ndio kiongozi wa halmashauri ya wilaya na ndio mamlaka ya juu katika ngazi ya wilaya na anaripoti kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha. Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro inasimamia wilaya ikiwa na wawakilishi kutoka ngazi ya tarafa (makatibu tarafa) na mabaraza ya kata (makatibu kata).

Utawala Ngazi ya Kijiji:

Kila Kijiji kina mkutano mkuu unaoongozwa na baraza la kijiji lililochaguliwa. Viongozi wa kuchaguliwa wa kijiji ni pamoja na mwenyekiti wa kijiji wa baraza la kijiji na wenyeviti wa vitongoji. Muundo wa utawala na mamlaka wa kijadi, kama vile laigwanak, huteua kiongozi wa kimila ambaye hushughulikia migogoro na kutoa ushauri katika jamii, mfumo huu uko nje ya mfumo wa serikali wa utawala wa kijiji.

Sheria inaelekeza kuwa kwa Tanzania bara, wanawake wanapaswa kuunda theluthi moja ya wajumbe wa halmashauri ya wilaya[69] na robo ya wajumbe wa mamlaka za miji[70] na baraza la Kijiji.[71] Kwa Tanzania Zanzibar, manispaa, miji na halmashauri za wilaya zinaundwa na wajumbe wanaoteuliwa na Waziri anayeshughulikia serikali za mtaa, ambapo asilimia 40 lazima wawe wanawake.[72]

Upatikanaji duni wa Taarifa

Kuhusu na mchakato wa mashauriano na ili kukidhi matakwa ya FPIC, mamlaka zinapaswa kuhakikisha kuwa jamii inayoathiriwa inapata taarifa za kutosha. Hii inamaanisha kuwa jamii iliyoathiriwa inapaswa kupata taarifa kila wakati (ikiwa ni pamoja na taarifa kutolewa katika lugha yao, katika sehemu inayofikika kirahisi na katika utaratibu unaokubalika kiutamaduni), inayoeleweka, isiyobadilika badilika, sahihi, isiyokuwa na upendeleo, iliyokamilika na iliyo wazi.[73] Hata hivyo, mamlaka za Tanzania zilitoa taarifa kwa uchache sana kuhusu maeneo kadhaa ya mpango wa kuwahamisha watu ikiwa ni pamoja na kuhusu fidia na hali ilivyo katika Kijiji cha Msomera. Wakazi wanasema kuwa hakuna nafasi ya kupata majibu kwa maswali waliyonayo kuhusiana na mchakati wa kuhama.

Baadhi ya wakazi walisema kuwa taarifa pekee waliyopata kutoka serikalini ni kutoka kwa Waziri Mkuu wakati wa mkutano wa tarehe 17 Februari, 2022 kuhusu kujiandikisha kwa ajili ya kuhama. Waziri Mkuu alisema kuwa wale wanaotaka kuhama wajiandikishe majina yao katika ofisi za Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na Kamishna wa Hifadhi ya Ngorongoro. 

Mwenyekiti wa halmashauri ya Kijiji – chombo cha utawala chenye jukumu la kuongoza Kijiji – katika eneo la NCA, alisema:

[Sisi] tumekuwa tukifanya mikutano kulalamika kuhusu serikali au chama cha siasa, lakini hakuna majibu toka Machi [2022]. Hatujaona kiongozi yoyote kutoka ngazi ya wilaya au taifa kuja Ngorongoro kuzungumza na wananchi na kujibu maswali yao tangu machafuko [katika eneo la Jirani la Loliondo mwezi Juni 2022.[74] Kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa, hakuna kiongozi aliyekuja kuwasikiliza wananchi wa Ngorongoro na kuelewa matatizo yao ni nini. Tumekuwa tukipiga kelele na ni kama viongozi wametutelekeza. Watu wanapoteza matumaini na wanahisi kukaa kimya ndo njia pekee.[75]

Baadhi ya wakazi walisimulia taarifa ambazo wanaamini ni uvumi kuhusu wakazi waliohama kupokea fidia ya fedha kiasi cha shilingi milioni 10 (US$ 3,970). Human Rights Watch iligundua kuwa mamlaka hazijatoa taarifa kuhusu fidia, ikiwa ni pamoja na kiasi au namna hesabu za fidia zinavyofanyika au kujadiliwa. “Mchakato mzima hauna uwazi,” mwenyekiti wa halmashauri ya Kijiji alisema. “Serikali inasema inatoa fedha lakini hakuna anayejua serikali itawapa nini mpaka watakapohama. Hakuna nafasi ya mazungumzo.”[76]

Baadhi ya viongozi wa kijamii walisema kuwa hawakujua wanakijiji waliojiandikisha kuhama mpaka siku waliposafirishwa kuondoka eneo la NCA. Kwa hivyo, viongozi wao wa kijamii hawawezi kuwapa usadizi wowote wakati wa mchakato wa kuhama.[77]

Diwani alisema hakuna taarifa za kutosha kuhusu mchakato wa kuhama: “Serikali haijawahi kumpeleka kiongozi yeyote au wawakilishi Msomera. Serikali haitaki sisi tujue. Mtu akijiandikisha kuhama, anaacha kuongea na viongozi.”[78]

Kutokana na upatikanaji hafifu wa taarifa kwa jamii, mchakato wa kuhama usiokuwa wazi na kukosekana na kwa njia inayoeleweka ya kushughulikia malalamiko, wakazi walisema wana njia finyu ya kushirikiana na serikali ili kuhakikisha inalinda haki zao, ikijumuisha iwapo watachagua kuhama au kubaki.

Kiongozi wa vijana alisema:

Hatufahamu chochote kuhusu Msomera. Tulichosikia ni kuwa watu wamepoteza mifugo yao. Je, tunahakikishaje kwamba serikali inahakikisha kuwa katika miaka miwili hadi mitano kama wakazi waliohama watapoteza mifugo yao yote, watapatiwa mingine, watalipwa fidia, ¿au kupata msaada? Je, jamii inahakikishaje serikali inatoa uhakika huu kama hatuna taarifa?[79]

Nyaraka za Human Rights Watch zinazoonyesha mashauriano duni na upatikanaji duni wa taarifa zinaweza kuonekana kama uhamishwaji wa lazima kama ilivyoelezwa na Kamati ya UN inayoshughulikia Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (CESCR) na miongozo kutoka kwa mwandishi maalumu wa UN kuhusu makazi yanayokidhi.[80]

Kupunguzwa kwa ufadhili wa Huduma za Kijamii katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro

Wakazi wote zaidi ya 70 wa NCA waliozungumza na Human Rights Watch walisema kuwa hawakutaka kuhama. Walisema kuwa tangu 2019, baada ya kuchapishwa kwa ripoti ya serikali,[81] serikali ilianza kupunguza huduma muhimu za kijamii kwa wakazi wa NCA na kupunguza ufadhili kwa Baraza la Wafugaji wa Ngorongoro.[82] Utoaji huduma katika eneo la NCA ulikua hafifu na mgumu kufikiwa na kwa ujumla wa kiwango duni kulinganisha na maeneo mengine nchini.[83]

Wakazi walidai kuwa serikali ilipunguza ufadhili wa huduma za kijamii ili kuwalazimisha kuondoka maeneo hayo. “Hapa Ngorongoro serikali imetumia jina la ‘kuhama kwa hiari,’ lakini hakuna kuhama kwa hiari,” alisema mkazi mmoja. “Serikali inatumia njia mbalimbali kutesa jamii yetu.”[84]

Serikali imepunguza upatikanaji, ufikiaji na ubora wa huduma muhimu za kijamii kama shule na hospitali katika eneo la NCA, kupitia kupunguza bajeti na vikwazo vingine kwenye rasilimali muhimu kama wafanyakazi wenye ujuzi. Vitendo hivi vimedidimiza upatikanaji wa haki kwa wakazi wa NCA, ikiwa ni pamoja na haki ya kupata elimu na huduma za afya na vimefanya ufikiaji wao wa maeneo ya kiutamaduni kuwa mgumu zadi. Familia za Wamasai zimeachwa bila kuwa na chaguo zuri zaidi ya kujiandikisha kwa ajili ya kuhama kutoka NCA kwenda Msomera.

Uandikishwaji wao sio wa ridhaa, ambapo ridhaa kwa mujibu wa FPIC inahusisha maamuzi ya pamoja yanayofanywa na watu wa asili walioathirika na kufikiwa kupitia mchakato wao wa kiutamaduni wa kufanya maamuzi. Ridhaa inapaswa kutafutwa na kutolewa au kukataliwa kupitia mifumo ya uwakilishi iliyo rasmi na isiyo rasmi ya kufanya maamuzi inayotumika na jamii ya watu wa asili iliyoathirika.

Kupunguza Ufadhili wa Baraza la Wafugaji la Ngorongoro

Baadhi ya wakazi ambao walikuwa au bado ni wajumbe wa Baraza la Wafugaji walisema kuwa hadi mwaka 2019 Baraza lilikuwa linaainisha mahitaji ya jamii, ikiwa ni pamoja na elimu, afya, maji na chakula; kisha kuandaa na kuwasilisha miradi kwa ajili ya kukidhi mahitaji haya kwa bodi ya NCAA kwa ajili ya kupata idhini na kupewa fedha; kisha kuitekeleza miradi hiyo. Kabla ya mwaka wa fedha 2019/2020, ambao ulianza Julai 1, 2019, bajeti ya mwaka ya Baraza la Wafugaji ilikuwa takribani shilingi bilioni 3 (US$ 1,150,000) kwa ajili ya miradi ya maendeleo na program ya NCAA ya ufadhili wa wanafunzi.[85]  Bajeti yote ya Baraza la Wafugaji ilikuwa inatoka NCAA.

Wakazi walisema kuwa mwaka 2019, NCAA kupitia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, ambacho ni chombo kinachochunguza na kufungua mashtaka ya makosa ya rushwa Tanzania bara, iliibua tuhuma za ubadhirifu wa fedha uliofanywa na Baraza la Wafugaji.[86] Kwa mujibu wa mjumbe wa Baraza la Wafugaji, tuhuma hizi hazikuthibitishwa lakini Taasisi hiyo ilitoa mapendekezo kwa Makamu wa Rais wa wakati huo ambaye ni Rais wa sasa, kuwa NCAA iwe inapeleka fedha hizo kwa Idara ya Maendeleo ya Jamii chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro badala ya Baraza la Wafugaji kwa ajili ya utekelezaji wa miradi.[87]

Wajumbe wa Baraza la Wafugaji walisema kuwa serikali haikufuta usajili wa baraza lakini iliondoa utoaji wa bajeti ya kila mwaka, na kuhakikisha kuwa Baraza halina uwezo wa kutekeleza miradi na kufanya maamuzi huru.[88] Mjumbe mmoja alieleza madhara ya uamuzi wa serikali kwa baraza:

Kwa sasa, Baraza la Wafugaji halina maamuzi, linakaa kwa ombi la NCAA. NCAA inaitisha vikao na kupendekeza bajeti. Mamlaka ya [Baraza la Wafugaji] imepungua. Kuondoa rasilimali ni kuhakikisha kuwa Baraza la Wafugaji halina nguvu, hususan kwa kuwa haliwezi kutafuta fedha peke yake kwa kuwa linachukuliwa kama taasisi ya serikali.[89]

Tangu mwaka 2020, Baraza la Wafugaji halijapokea fedha yoyote kutoka NCAA au Idara ya Maendeleo ya Jamii – ikiwa ni pamoja na fedha kwa ajili ya maboresho, ujenzi wa miundombinu ya shule na miradi mingine ya kijamii katika eneo la NCA – jambo ambalo limeathiri utunzaji wa miundombinu ya shule, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vyoo, marekebisho ya madarasa na utoaji wa madawati na vitanda vya ziada kwa jili ya wanafunzi.[90] Wajumbe wa Baraza la Wafugaji pia walisema tangu wakati huo upatikanaji wa fedha kutoka NCAA kwa ajili ya vituo vya afya na shule ulipungua.

Athari kwa Upatikanaji wa Elimu

Vitendo vya mamlaka za serikali kupunguza kwa makusudi na kudhoofisha hali za shule katika eneo la NCA vinaathiri mamia ya Watoto kupata na kufurahia haki ya kupata elimu.

Utoaji wenye ukomo wa Ufadhili wa Wanafunzi

Kupunguzwa kwa ufadhili wa Baraza la Wafugaji, kwa mujibu wa waliohojiwa kumepelekea kuchelewa kutolewa fedha kwa wanafunzi wa chuo, jambo ambalo linapelekea vikwazo vya gharama na kupunguza ufikiaji wa elimu ya juu. Kuanzia mwaka 2020, NCAA imehamisha jukumu la kufadhili wanafunzi kutoka Baraza la Wafugaji kwenda ofisi ya Wilaya ya Ngorongoro.[91] Ufadhili huu ni wa wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka eneo la NCA, wanaofadhiliwa na NCAA kupitia program ya Ufadhili wa Wanafunzi.[92]

Wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wamefaidika na usaidizi wa masuala ya shule au udhamini walisema kuwa hapo zamani, Baraza la Wafugaji lilikuwa linatoa fedha mapema. Hata hivyo, wanafunzi hao wa vyuo vikuaa wanasema kwa sasa inabidi wasubiri muda mrefu na changamoto nyingi kabla ya kupata fedha hizo. “Wakati mwingine fedha inakuja kutoka halmashauri ya wilaya baada ya muda mrefu kupita na kwa kawaida baada ya mapambano,” mwanafunzi mmoja alisema. “Pia, hazitoshi.”[93]

Mkazi mmoja wa NCA alisema kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu sio tu wamekuwa akipokea fedha kidogo za ufadhili, halmashauri ya wilaya inachelewesha malipo ya ufadhili na wakati mwingine vyuo haviwatambui kama wanufaika wa ufadhili kwa sababu hawapati barua ya utambulisho kutoka NPC.[94]

Athari kwa Upatikanaji wa Vifaa vya Shule vya Kutosha

Viongozi wa kijamii na wakuu wa shule wanatakiwa kuomba fedha na idhini kutoka NCAA kujenga au kufanya maboresho ya miundombinu ya shule ndani ya eneo la NCA. Hata hivyo, tangu mwaka 2021, NCAA imekataa maombi yote ya vibali vya ujenzi bila maelezo yoyote.[95]  Viongozi wa kijamii walisema kuwa wakijaribu kutumia rasilimali zao wenyewe bila ya vibali vya NCAA wanakumbana na unyanyasaji na wakati mwingine kukamatwa. 

Human Rights Watch iligundua shule kadhaa katika eneo la NCA zilizo katika hali mbaya kutokana na NCAA kukataa kutoa fedha au vibali kuruhusu maboresho kufanyika kwa shule za msingi na sekondari. Wakazi walieleza kutokea kwa matukio haya.[96] Shule ya Msingi Esere iliyoko Esereina majengo mengi ya zamani na yaliyo katika hali mbaya, vyoo vilivyojaa na madawati machache yasiyokidhi mahitaji, lakini wanajamii walisema kuwa NCAA imekataa maombi yao ya fedha na idhini ya kufanya maboresho.[97] Shule ya Msingi Olbalbal iliyoko Olbalbal inahitaji choo, lakini NCAA imekataa pendekezo la kujenga choo.[98] Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Ngorongoro, yenye wanafunzi takribani 500, haina madawati ya kutosha, hivyo wanafunzi hukaa chini wakati wa masomo, na kuna vyoo saba pekee kwenye jengo moja kwa ajili ya wasichana wote. Inaonekana kuwa NCAA inasita kuidhinisha ujenzi wa jingo jingine la vyoo.[99] Wakati paa la jengo katika Shule ya Msingi Misigiyo lilivyoharibiwa kipindi cha msimu wa mvua mwaka 2021, NCAA ilituma shilingi 2,780,000 ($1,065) kwenye akaunti ya shule kwa ajili ya ujenzi wa paa wakati tukio lilipotokea mwaka 2021. Hata hivyo, tangu wakati huo, NCAA imekataa kutoa kibali cha kuruhusu maboresho kufanyika na kukataa kuruhusu wakazi kuleta mabati mapya ndani ya eneo la NCA kwa ajili ya ukarabati. Wanajamii walisema kuwa walipojaribu kutumia mabaki ya paa yaliyoezuliwa, NCAA ilikataa kuwapa kibali cha ujenzi.[100]

Majengo katika Shule ya Msingi Mokilal, Kijiji cha Mokilal, Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA), mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023. © 2023 Human Rights Watch

Vibali hivi ni muhimu, bila ya kuwa navyo wakazi hawawezi kuingia katika geti la NCA wakiwa na vifaa vya ujenzi kwa ajili ya shule kama vile mabati ya kuezekea au kufanya marekebisho yoyote bila ya kuwa na kibali. Wanakijiji walipochanga fedha kwa ajili ya kufanya marekebisho na kujenga majengo ya shule katika eneo la NCA, NCAA ilikataa kuwapa vibali vinavyohitajika, pamoja na idhini ya kusafirisha vifaa vya ujenzi ndani ya eneo la NCA. Hawatoi maelezo pale wanapokataa. Kwa mfano, Shule ya Wasichana ya Ngorongoro ina shilingi milioni 300 ($115,000), ambayo ilichangwa kwa miaka kadhaa na wanajamii, kwa ajili ya kufanya marekebisho kwenye shule, lakini NCAA haijatoa vibali vinavyohitajika.[101]

Mwaka 2022, mkazi mmoja alitumia rasilimali zake kujenga vyumba viwili vya madarasa kwa ajili ya shule ya awali, lakini NCAA haikumruhusu kuingiza vifaa vya kuezekea ndani ya eneo la NCA. Matokeo yake, wanafunzi wanakosa kitu cha kuwakinga na mvua wakati wa msimu wa mvua.[102]

Wakazi wamejaribu kutumia vifaa vya jadi kujenga lakini hilo nalo lina changamoto zake, kutokana na vikwazo vya kukata miti na matawi.

Mwaka 2022, serikali ilihamisha fedha za elimu kutoka NCA kwenda mkoa wa Tanga kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya Msomera, ambapo wakazi wa NCA wanahamishiwa.[103] Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro ilitoa maelekezo mawili kwa shule sita za umma katika eneo la NCA mwezi Machi 2022, ikiwaelekeza kuhamisha takribani shilingi milioni 200 ($76,500) ambazo ni fedha za kukabiliana na Uviko kwenda eneo ambalo watu wanahamia Msomera.[104]

Kupunguza Ufadhili na kushusha hadhi ya vituo vya afya

Wakazi ambao wamehojiwa na Human Rights Watch walisema kuwa serikali imesababisha moja kwa moja na kwa njia zisizo za moja kwa moja kupungua kwa upatikanaji wa huduma za afya na kupungua kwa ubora wa huduma za afya katika eneo la NCA.

Diwani katika Kijiji cha Esere alitoa mfano wa namna serikali imeacha kusaidia huduma za afya katika eneo la NCA:

Siwezi kufananisha Endulen [Hospitali] ya sasa na hapo awali. Hapo awali, serikali ilikuwa inatoa msaada pamoja na watumishi wa hospitali waliowalipa. Hapo awali, Endulen ilikuwa na huduma ya mama na mtoto na dawa za kutosha. Sasa, serikali imesitisha misaada yote; wamewaondoa madaktari waliowaleta [hapa hospitali ya Endulen] na kuwarudisha katika hospitali za serikali.[105]

Mnamo Oktoba 2022, serikali ilitangaza kuwa itaishusha hadhi hospitali ya Endulen, hospitali yenye vitanda 110 inayosimamiwa na Kanisa Katoliki toka mwaka 1965 na hospitali pekee inayotoa huduma zote za matibabu kwa Wamasai waishio katika eneo la NCA, kuwa kituo cha afya kutokana na uhaba wa wafanyakazi.[106] Mtoa huduma za afya alieleza namna serikali ilivyofikia uamuzi huo: “Mwaka 2018 NCAA ilisitisha ufadhili kwa Hospitali ya Endulen. Kwa kawaida hutenga takribani shilingi milioni 30 ($11,900) kwa mwaka. Lakini Hospitali ya Endulen ilikuwa na fedha za mradi kutoka kwa wafadhili wengine mpaka kufikia mwaka 2022.”[107] Mtoa huduma za afya alisema kuwa wafadhili wengine wa hospitali hiyo wamesitisha kutoa fedha kwa sababu wana wasiwasi juu ya uendelevu wake kutokana na mashaka yanayotokana na mchakato wa kuwahamisha watu na uwezekano wa hospitali kulazimika kufungwa.[108]  

Njia ya kuingia Hospitali ya Endulen katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA), mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Juni 22, 2023. © 2023 Mathias Rittgerott/Rainforest Rescue

Kufikia mwaka 2022, idadi ya wafanyakazi wa hospitali ilipungua kutoka karibia watu 60 hadi 17 baada ya wafanyakazi waliokuwa wanalipwa na serikali kuondoka kwenda kuchukua nafasi serikalini zilizotangazwa katika maeneo mengine, na hakuna nafasi mpya ya ajira ilitangazwa katika Hospitali ya Endulen kwa ajili ya kujaza nafasi za watumishi walioondoka. Huko nyuma, nafasi za kazi katika Hospitali ya Endulen zilitangazwa kwa watumishi wa serikali. Mwezi Disemba 2022, serikali iliunda kamati iliyoongozwa na mganga mkuu wa mkoa na mganga mkuu wa wilaya kuchunguza huduma katika hospitali na kugundua kuwa haikuwa na wafanyakazi wa kutosha. Kamati ikapendekeza kuwa hospitali iache kutoa baadhi ya huduma ikiwa ni pamoja na huduma za magari ya wagonjwa na huduma za dharura, kutokana na uhaba wa wafanyakazi, kushushwa hadhi kutoka kuwa hospitali hadi kituo cha afya, na kuruhusu utoaji wa huduma za msingi na huduma za madawa pekee.[109]

Wakazi na wafanyakazi wa afya walisema kuwa Hospitali ya Endulen ilikabiliana na uhaba mkubwa wa madawa, kueleza kuwa matokeo ya uhaba huo yakapelekea dawa za kutuliza maumivu na homa zikawa zinatolewa kwa magonjwa yote.

Wakazi waliiambia Human Rights Watch kuwa kutokana na ukosefu wa baadhi ya huduma za kiafya zilizokuwa zinapatikana hapo awali, ilibidi watafute huduma za matibabu katika zahanati zenye vifaa vichache. Mfanyakazi wa afya katika zahanati moja katika eneo la NCA anaeleza kuwa zahanati yao yenye vyumba vinne ilishuhudia ongezeko la wagonjwa katika kipindi cha mwaka uliopita: “Wagonjwa wanapoona huduma nyingi zinapatikana hapa, wanaambiana na hivyo wengi wanakuja hapa kwetu.”[110] Anaeleza kuwa zahanati hii ni ndogo sana kuhudumia wagonjwa wote ambao hapo awali walikuwa wakipata huduma za afya katika Hospitali ya Endulen, na haiwezi kuongeza majengo kwa sababu NCAA imewakatalia maombi yao ya kibali cha ujenzi. Aliongeza kuwa wafanyakazi pia wanaogopa serikali inaweza kufungia zahanati kutokana na mpango wa kuwahamisha watu.[111]

Zaidi ya hayo, baadhi ya mbadala wa huduma za afya katika maeneo hayo umevurugika. Mwezi Februari 2022, serikali ilisitisha Huduma za Afya za Anga, huduma afya zitolewazo na Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, ambayo hutoa huduma ya kliniki katika wilaya ya Ngorongoro, ambayo ilikuwa inawafaa sana wanawake wajawazito, hususan wale wanaokumbana na ugumu katika kujifungua kwa sababu inaweza kuwasafirisha wagonjwa haraka kwenda hospitali nyingine nje ya eneo la NCA.[112]

Ili kupata huduma muhimu, wakazi wamelazimika kusafiri umbali mrefu nje ya eneo la NCA. Mwanaharakati alieleza umbali ambao watu hupaswa kusafiri kupata dawa fulani:

Serikali ilikuwa inasambaza dawa kwa ajili ya matibabu ya VVU, lakini hawafanyi hivyo tena. Ikiwa unahitaji dawa hizo inabidi usafiri [Kilomita 60] kwenda Karatu [jirani na wilaya ya Karatu]. Na kwa matibabu ya TB, waliacha kutoa huduma hizo pia. Inabidi uende [kilomita 200] kwenda Arusha [makao makuu ya mkoa] ili kupata huduma hizo.[113]

Kuongezeka kwa umbali wa kupata huduma za msingi za afya kunasababisha changamoto kubwa katika hali ambayo njia za usafiri zina ukomo na utegemezi ni wan jia za usafiri zisizo za mashine, ikiwa ni pamoja na kutembea.[114] Mfanyakazi wa jamii alisema kuwa mwanamke mjamzito mwenye upungufu wad amu hakuweza kupata huduma ya kuongezewa damu katika Hospitali ya Endulen kutokana na kupungua kwa watumishi na huduma, na matokeo yake alipewa rufaa ya kwenda hospitali ya Karatu, takribani umbali wa kilomita 60[115] Mwanamke mwingine mjamzito kutoka Esere, ambaye alihgongwa na gari la watalii ilibidi akimbizwe Karatu kwa ajili ya huduma za matibabu; akiwa njiani kurudi eneo la NCA, alipata uchungu na kujingua kwenye gari.[116] Kutokana na huduma duni za afya katika eneo la NCA, wafanyakazi wa afya wanawashauri wanawake wajawazito kwenda Karatu kwa ajili ya huduma za ujauzito na utunzaji wake; wengine wenye hali ngumu za ujauzito inawabidi kukaa Karatu, mbali na familia zao, kwa wiki kadhaa wakati wakisubiri uchungu kuanza.

Katika baadhi ya matukio na dharura matokeo yake yamekuwa mabaya. Mwanamke mmoja alisema kuwa kati ya Aprili na Mei 2023, wanawake watatu walipoteza maisha kutokana na changamoto zitokanazo na ujauzito kwa kukosa huduma za haraka za kuokoa maisha katika Hospitali ya Endulen.[117] Mwanamke mwingine alieleza ugumu unaohusiana na afya ndani ya familia yake: “Mtoto wa mjomba wangu alijifungua mapacha. Watoto walizaliwa tukiwa njiani kwenda hospitali ya Karatu. Walizaliwa mapema wakiwa na miezi saba. Watoto wote walifariki kwa kushindwa kuwapatia huduma sahihi kwa wakati.”[118] Human Rights Wach haikufanya uchambuzi wa viwango vya vifo vya uzazi na watoto wachanga kabla na baada ya mwaka 2022 katika eneo la NCA.

Wakazi walisema kuwa huko nyuma, serikali na NGOs zilifanya kampeni kujenga uelewa wa wanawake wajawazito na afya ya mtoto mchanga na kuwahimiza wanawake kwenda hospitali wakati wa ujauzito na kwa huduma za kabla na baada ya kujifungua. Kutokana na hali ya sasa, wakazi walieleza wasiwasi wao kuwa serikali inabadili sera zake kwa kupunguza upatikanaji wa huduma za afya ndani ya eneo la NCA. “Tumeelimishwa kuwa tunatakiwa kwenda hospitali wakati wa ujauzito,” mwanamke mmoja alisema. “Lakini sasa hatuna huduma hizo tena.”

Taarifa za Shirika la Afya Duniani zilizochambuliwa na Human Rights Watch zilibainisha kuwa serikali ya Tanzania ilitumia sawa na asilimia 0.91 ya pato la taifa (GDP) au asilimia 5.14 ya bajeti ya serikali katika huduma za afya kwa mwaka 2021, mwaka wa karibuni ambao taarifa zake zinapatikana.[119] Hii ni pungufu ya vigezo viwili muhimu vya kimataifa vinavyohusiana na kupunguza ukosefu wa usawa wa upatikanaji wa huduma za afya na matokeo: kutumia asilimia 5 ya GDP au asilimia 15 ya matumizi ya nchi katika huduma za afya kupitia njia za umma. Kiwango hiki cha uwekezaji wa umma pia kinashindwa kukidhi ahadi ya wazi ya Tanzania kwa Umoja wa Afrika katika Azimio la Abuja la 2001 la kutumia angalau asilimia 15 ya bajeti kuu katika huduma za afya .[120] Wakati Tanzania pia imekabiliwa na deni kubwa la taifa, kulipa takribani mara nne zaidi kwa kipimo cha mtu mmoja kuhudumia deni lake la nje mwaka 2021 kuliko inavyogharamia huduma za afya, serikali haina budi kuchukua jitihada kuhakikisha kuwa makundi yaliyotengwa kijamii na kiuchumi, ikiwa ni pamoja na jamii za watu wa asili hazibebi mzigo wa kupunguzwa ufadhili.

Vizuizi vya kuingia na kutoka katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro   

Baadhi ya wakazi waliiambia Human Rights Watch kuwa NCAA iliweka vizuizi kuingia eneo la NCA toka Februari 2022,[121] kupunguza mizunguko ya wakazi, pamoja na wale wanaohitaji kupata huduma nje ya eneo hilo.

Askari wanyamapori wa NCAA wanawataka wakazi kuonyesha kitambulisho (ID) kama kithibitisho cha ukazi katika eneo la NCA kabla ya kuwaruhusu kuingia getini kuelekea katika vijiji vyao. Wakazi wasiokuwa na ID au kitambulisho cha mpiga kura au waliosahau vitambulisho nyumbani huzuiwa kuingia wanaporudi nyumbani na hulazimika kulipa shilingi 11,800 ($5), ambayo ni ada ya kuingia NCA kama mtalii Mtanzania. “Watu wa NCA hutoka na kwenda Karatu kununua nafaka, kwenda hospitali au mwanafunzi kwenda chuo kikuu,” mkazi mmoja alisema. “Wanaporudi, walinzi wa getini huwakatalia kuingia na kuwaaibisha.”[122] Diwani wa Kata alisema kuwa alikataliwa kuingia alipokuwa anarudi kutoka katika mkutano wa madiwani Loliondo kwa sababu alisahau kitambulisho chake cha mpiga kura nyumbani. Alikaa getini mpaka mtu aliyeweza kumtambua alipokuja. Alisema: “Kama mimi nakumbana na mambo haya vipi kuhusu wananchi wa kawaida?”[123]

Mkazi mmoja wa NCA alisema kuwa askari wanyamapori wa NCA bila mpangilio huuliza aina tofauti tofauti ya utambulisho:

Kama leo niko Arusha na ninahitaji kwenda Ngorongoro, lazima niwe na ID kuingia pale…. Hata kama wanajua wewe ni mkazi, lazima uonyeshe kitambulisho. Unaweza kuwa na kitambulisho cha Taifa, [lakini] wakati mwingine wanataka uonyeshe kitambulisho cha mpiga kura. Na wakati mwingine una kitambulisho cha mpiga kura, na wao wanahitaji uonyeshe kitambulisho cha taifa.[124] 

NCAA pia inatoza magari yote, pamoja na yale yanayowasafirisha wenyeji, ada ya kuingia kila mara wanapoingia. Ada hiyo inatofautiana kulingana na uzito wa gari, kiwango cha chini kikiwa shilingi 23,600 ($9). Madereva wanalipa ada ya siku. Wakazi wanasema kuwa madereva wa magari yanayosafirisha watu kuingia na kutoka eneo la NCA wamehamisha gharama hizi za ziada kwa wakazi, jambo linalofanya usafiri kuwa wa gharama sana na “kutoka nje kuwa ngumu.”[125]

Kiongozi wa kimila alieleza athari kwa wakazi wanaougua na hawawezi kumudu gharama ya kusafiri:

Kila mkazi anaumia. Ukiugua unafikiria gharama kubwa utakayotumia kutafuta huduma za afya. Watu maskini wapo katika hatari zaidi kwa sababu hawana pesa za kusafiri mbali, na zahanati za karibu hazina dawa. Unaweza kuuza mifugo na kupata huduma hizi. Njia nyingine ni kutumia mitishamba ya kitamaduni au kuomba Mungu kwa ajili ya muujiza.[126]

Mkazi ambaye amekuwa akikosoa waziwazi mpango wa serikali kuwahamisha Wamasai kutoka NCA alisema mamlaka zimemzuia kurudi nyumbani kwa sababu ya uanaharakati wake. Alisema kuwa askari polisi alimkatalia kuingia getini kuelekea NCA walipokuwa wanarudi nyumbani kutoka safari mwezi Oktoba 2022na kusema kuwa nyaraka zao za utambulisho hazikuwa zimesajiliwa. Mwanaharakati huyu anaamini kuwa walikuwa wanafuatiliwa na maafisa usalama wa serikali wakati wa safari yao na kwamba maafisa waliokuwa getini walikuwa wametahadharishwa kuhusu kurejea kwao.[127]

NCAA inaomba kitambulisho tofauti ili kuthibitisha makazi na vinginevyo kutoza ada ya kutalii kwa wakazi wanaorudi nyumbani jambo linaloongeza msigo kwa watu wa Asili ambao wana uhusiano wa kihistoria na wa kitamaduni wa sasa na ardhi nna ambao serikali imewafungia katika eneo la NCA. NCAA inapaswa kuanzisha mfumo wa uwazi, na kuwashirikisha wanajamii, ili kupunguza au kuondoa mzigo huu na kutoa wepesi wa kuingia kwa wanajamii wa asili.  

Vizuizi vya kufikia maeneo ya malisho, maji na maeneo ya kiutamaduni katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro

Kutokana na sheria na sera za serikali, jamii ya Wamasai katika eneo la NCA linakabiliana na vizuizi vya kufikia na haki za kutumia ardhi waliyoishi vizazi kwa vizazi na hawana uthibiti au uwezo wa kufanya maamuzi kuhusu ardhi hiyo, ikiwa ni pamoja na namna mapato yatokanayo na utalii yanavyogawanywa[128] Hii ni pamoja na uwezo wa kufikia maeneo yyenye majani mengi ya malisho, vyanzo vya maji na maeneo ya utamaduni.

Upatikanaji wa Malisho

Wakazi wa NCA walisema kuwa mamlaka zimeweka vizuizi kwa wao kufika maeneo muhimu ya malisho, jambo ambalo limeleta changamoto kutokana na kwamba wanategemea ufugaji kuendesha maisha yao. Walisema kuwa mamlaka zimewazuia kulisha mifugo yao katika maeneo mbalimbali ndani ya NCA, hii ni pamoja na bonde la Ngorongoro, kuwanyima mifugo yao vyanzo muhimu vya maji, majani na miamba na ardhi ya volkano yenye virutubisho vingi. Kwa kuongeza, wakazi walisema kuwa NCAA iliacha kutoa huduma za mifugo kwa mifugo ya wanajamii katika wakati ambao serikali ilianza kuwahamisha watu kwenda Msomera.[129]

Mwenyekiti mmoja wa Kijiji alisema:

Serikali inaanza kutufanya tusifanye kazi kabisa. Wanajaribu kutudhoofisha katika nyanja zote za maisha. Kukata tamaa, kuto kupigana na kuondoka. Wanajaribu kuhakikisha kuwa ufugaji unafikia kikomo. Hatujawahi kuwafukuza wanyamapori waondoke. Sisi ni wahifadhi wazuri sana; hatuwachukii wanyama pori.[130]

Baadhi ya wakazi walisema kuwa mwaka 2016, maafisa wa serikali waliwaeleza wanajamii katika eneo la NCA kupitia viongozi wao, juu ya uamuzi wa kuzuia mifugo yao kuingia kwenye Bonde la Ngorongoro kutokana na uhifadhi na “utalii wa mazingira.” Hali hii ilileta usumbufu kwani wanayamapori na mifugo katika eneo la NCA wanategemea ulaji wa udongo, ambao hufanywa na wanyama wengi pamoja na binadamu – kwa ajili ya virutubisho na kupunguza matatizo ya utumbo.

Bonde la Ngorongoro lina vyanzo vya maji vya thamani vya kudumu, ambavyo vilikuwa vya thamani zaidi wakati wa kiangazi, na ulaji wa udongo ambao ni muhimu kuwaongezea mifugo virutubisho, hasa virutubisho ambavyo havipatikani katika majani yanayoota katika maeneo hayo.[131] Kwa upande mwingine, virutubisho hivi na upatikanaji wa maji ni wa manufaa kwa afya ya mifugo na huongeza uzalishaji wa maziwa kwa ng’ombe, yenye manufaa muhimu ya lishe na fedha kwa wakazi wa eneo hilo.

Kihistoria wakazi wamekuwa wakipelekea mifugo yao kwenye malisho katika bonde kwa sababu inachangia afya na uzalishaji wa maziwa kutoka kwa ng’ombe wao, hii ni kutokana na kuwepo na masalia ya sodium na virutubisho vingine kama vile selenium, cobalt, manganese na molybdenum.[132] Wakazi watatu wa  kata za Alaitolei na Nainokanoka walisema kuwa wakati NCAA walipozuia kuingia eneo la bonde, mamlaka ilisema kuwa itatoa maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo kwa vijiji vyote, na kusambaza chumvi ya ziada kuhakikisha mifugo inapata chumvi nyumbani badala ya kula udongo katika bonde.[133] “[NCAA] walikuwa wanataka kuanzisha shamba la mifugo katika kitongoji cha Ngairish kata ya Kakesio,” alisema mkazi mmoja. “Tulikuwa tunaenda kujifunza namna ya kukuza majani ambayo ni mazuri kwa mifugo. Tutakuwa na mbegu nzuri ya ng’ombe, kuongeza idadi. Tulisema huu ni mpango mzuri.”[134]

Wakazi walisema kuwa tangu mwaka 2017, ambapo serikali ilianza kutoa chumvi ya ziada kwa jamii yao, zaidi ya ng’ombe 77,000 walikuwa wamekufa kufikia Disemba 2021.[135] Wanajamii walisema kuwa wanaamini kuwa chumvi iliyosambazwa na serikali ilikuwa na sumu na haikuwa salama. Mashaka yao yalithibitishwa na uchunguzi wa madini ya sampuli ya chumvi uliofanywa na Wakala wa Maabara ya Mifugo Tanzania, wakala wa serikali, ambao walihitimisha kuwa chumvi hiyo haikuzingatia Rasilimali za Malisho ya Wanyama na Ardhi ya Malisho (Kiwango cha Rasilimali ya Malisho kwa Wanyama) kanuni ya 2012.[136] 

Mwenyekiti wa baraza la Kijiji alisema chumvi iliyochafuliwa iliathiri jamii yake:

Tulipoteza ng’ombe wetu wote. Katika Kijiji change ng’ombe 6,294 walikufa. Nimepoteza ng’ombe 120. [Mtu mmoja] alikamatwa Juni 30, 2022, Simon Saitoti, diwani wa kata – kwa sababu  aliongea kuhusu chumvi hiyo. Alishtakiwa kwa mauaji [ya polisi Loliondo]. Ng’ombe wake wote walikufa. Aliingia gerezani akiwa mtu mwenye mali na akatoka akiwa mtu maskini.[137]

Mbali na kuzuia kuingia katika Bonde la Ngorongoro, askari wanyamapori wa NCAA pia wamezuia mifugo kufika kwenye maeneo yenye maji, hii ni pamoja na msitu wa kaskazini, Marshes, Ndutu na  mabonde ya Ormoti na Embakaai. [138] Wakazi walidai kuwa askari wanyamapori wa NCAA waliwapiga na kuwakamata wanajamii kwa kuchunga mifugo yao katika maeneo ambayo NCAA imezuia wanajamii kufika. Mnamo Juni 13, 2022, vyombo vya usalama vilimkamata Paresoi Kiboko baada ya kupeleka mifugo yake kuchunga malisho Ndutu, eneo ndani ya NCA ambalo wanajamii wamekuwa wakienda miaka yote.[139] Wakili anaefahamu kesi ya Kiboko alisema kuwa askari wanyamapori walimpiga na kumuweka kizuizini na kisha kumfikisha mahakamani siku inayofuata ambapo alisomewa shitaka la kulisha mifugo katika eneo lililopigwa marufuku na kuwatishia askari wanyamapori na mkuki.[140] Kwa sababu Kiboko hazungumzi Kiingereza wala Kiswahili na mahakama haikumpatia mkalimani, hakuweza kufuatilia mwenendo wa mahakama katika kesi dhidi yake. Kiboko alihukumiwa kifungo cha miezi tisa kabla ya kutolewa mwezi Machi, 2023.

Ufikaji wa Maeneo yenye Maji

Vizuizi vya serikali vya 2016 kwa jamii kuhusu kufika katika maeneo kadhaa ndani ya eneo la NCA ilijumuisha maeneo yenye vyanzo vya uhakika vya maji kwa wanakijiji na mifugo yao.

Kiongozi mmoja wa jamii aliiambia Human Rights Watch:

Katika Kijiji changu tulikuwa tuna maeneo mengi yenye uwezo [wa kupata maji kwa ajili ya mifugo yetu]. Kuna baadhi ya maeneo ambayo tulikuwa hatuendi kwa kipindi fulani katika mwaka, kuanzia Disemba hadi Mei tulikuwa hatufiki huko kutokana na uwepo wa nyumbu [kwa kuogopa kuwaambukiza ng’ombe magonjwa]. Wakati huo tulikuwa tunakwenda nyanda za juu na kuacha maeneo mengine kwa ajili ya nyumbu. Na katika kipindi fulani cha mwaka kuna maeneo ambayo tunakwenda wakati wa ukame. Lakini sasa wameanza kutuambia kuwa hatuwezi kwenda pale – sehemu kama Ndutu. NCAA imeanza kuwapiga wafugaji.[141]

Wakazi walisema kuwa NCAA iliwahakikishia kuwa jamii ingeendelea kuvifikia vyanzo vingine vya maji nje ya bonde. Hata hivyo, hali haikuwa hivi, kama utafiti. “NCAA haijatenga sehemu ya kudumu ya kupata maji [kwa ajili ya mifugo],” mwanamke mmoja alisema. “Mwaka jana [2022], wakati wa kipindi cha ukame, wanyama wetu wengi walitaabika.”[142] Mkazi mwingine alieleza kuwa ijapokuwa serikali ya kikoloni ya Uingereza ilichimba zaidi ya mabwawa 10 ya maji kwa ajili ya kuvuna maji ya mvua, ni mabwawa mawili pekee ambayo bado yanafanya kazi.

Kutokana na kwamba karibu mifugo yote katika vijiji vya karibu inatumia mabwawa hayo mawili, kuna shinikizo kubwa kwa mabwawa hayo. Hayawezi kuwapatia maji ya kutosha mifugo yote kwa sababu maji katika mabwawa hayatoshi, na shinikizo linalotokana na wingi wa mifugo kutegemea kwenye mabwawa hayo inamaanisha kuwa mifugo inaweza kuharibu mabwawa hayo. Baadhi ya wakazi walisema kuwa NCAA haijakarabati mabwawa nane ambayo hayafanyi kazi wala kujenga mapya.[143] Mwanamke mmoja alisema kuwa ijapokuwa NCAA imetoa maji ya bomba kwa jamii, haina ufanisi katika kutunza na kukarabati vituo hivi vya maji. “Kunapotokea uharibifu, NCAA inakataa kukarabati,” alisema. “Tunapopata vifaa vya kufanya ukarabati, NCAA inakataa [na kusema] hatupaswi kuyakarabati na kwamba wana mtaalamu nje ya eneo la NCA ambaye atayakarabati.”[144]

Vizuizi vya NCAA katika vituo muhimu vya maji na malisho vina athari hasi kwa afya ya mifugo, uzalishaji wa maziwa, na kipato kitokanacho na kuuza maziwa na mifugo. NCAA pia imepiga marufuku ya kulima mazao, ambayo ilitambulishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1975 ili kusaidia uhifadhi wa uoto wa asili.[145] Huko nyuma Waziri Mkuu aliondoa kwa muda marufuku hiyo, mfano mwaka 1992.[146] Wakazi walikiri kuwa NCAA inatoa mahindi kwa bei ya ruzuku, lakini kutokana na uthibitisho kuwa vifo vya mifugo yao vilitokana na chumvi mbaya waliyopewa na NCAA, iliyoelezewa huko juu, wakazi wamepoteza Imani na NCAA na baadhi wamekataa kununua mahini hayo.[147] Wakati wa mahojiano yetu mwezi Juni 2023, ilikuwa takribani miaka miwili tangu baadhi ya wakazi kuacha kununua mahindi yenye bei ya ruzuku. Vizuizi vya kufika kwenye maeneo ya malisho na maji na marufuku ya kilimo imepelekea hatari ya kukosa chakula na athari za kiafya kwa jamii ndani ya eneo la NCA.[148]

Ufikaji wa Maeneo ya Kiutamaduni

Mbali na vizuizi vilivyowekwa kufikia vitu muhimu kwa mifugo yao, wakazi walisema kuwa mamlaka zimewazuia kufika kwenye maeneo muhimu ya kiutamaduni na kijadi toka mwaka 2016. Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa kimila, hawaruhusiwi katika maeneo ya matambiko katika Bonde la Ngorongoro, Bonde la Olmoti na Mbakai na Wamasai wanakamatwa kwa kwenda huko.[149]

Kuwazuia kufika katika maeneo ya kiutamaduni, na matarajio ya kuhamishwa, kunaweza kupelekea Wamasai kutengana na utamaduni wao na aina yao ya maisha-kuingilia haki yao ya kiutamaduni. Hii ni kwa sababu utambulsiho wao na utamaduni wao umeshikamana na ardhi yao.  Mzee mmoja wa Endulen ambaye alishuhudia zoezi la kuwahamisha Wamasai kutoka Serengeti lililofanyika wakati wa ukoloni mwaka 1959 alisimulia juu ya upotevu wa ardhi ya kudumu:

Serengeti ilitumika kulisha mifugo na makazi ya muda, na tukahamia nyanda za juu [Ngorongoro] wakati wa kiangazi… ambapo tuliwazika babu zetu. Hatuna mahali pengine popote. Hapo awali, watu wetu wanaweza kuwa wameiacha Serengeti kwa sababu tulikuwa na ardhi nyanda za juu, eneo letu la kudumu. Sasa hatuna.[150]   

Vizuizi vya NCAA vimetokea kwa miongo kadhaa, huku kukiwa na ahadi za kutoa nafaka ya ziada, ufikiaji wa maeneo ya maji, chumvi, ranchi na huduma za mifugo kwa mifugo yao ili kupunguza madhara kwa jamii zilizoathirika na maisha yao, ambayo haijatimiza hadi sasa. Chini ya UNDRIP, ridhaa sio maamuzi yanayotolewa mara moja bali ni sehemu ya mchakato wa FPIC ambayo inatafutwa, inatolewa na inaweza kuondolewa. Human Rights Watch ilihitimisha kuwa ahadi za NCAA kutoa bidhaa na huduma za ziada hazijatekelezwa toka zoezi la kuwahamisha watu lilivyotangazwa, na vizuizi vilivyowekwa kwa jamii kufikia maeneo ya malisho, vyanzo vya maji na maeneo ya kiutamaduni haviendani na viwango vya FPIC.

Ukatili unaofanywa na Askari Wanyamapori wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro

NCAA imeajiri askari wanyamapori kulinda maeneo ya kuingia na maeneo mengine ndani ya NCA.[151] Huko nyuma, askari wanyamapori walikuwa wanatoka katika jamii inayoishi NCA au Wamasai, lakini wakazi walisema katika miaka ya karibuni, wanajamii ambayo waliajiriwa na NCAA kama askari wanyamapori ambao walikuwa na huruma kwa jamii, wamehamishwa kwenda Msomera. Kwa mujibu wa mwanaharakati mmoja:

Watu wanaofanya kazi na NCAA wana matatizo yao. Kwa sababu ni wazawa [wa NCA], serikali inawalazimisha kuhama. Kama hutaki kuhama, wanasitisha ajira yako. Mjomba wangu anafanya kazi na NCAA na wote walishinikizwa. Wanatakiwa kukubaliana na serikali. [152]

Baadhi ya wafanyakazi wa NCAA ambao hawakutaka kuhamia Msomera walihamishiwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania na katika maeneo mengine yanayodhibitiwa nje ya NCA ikiwa ni pamoja na Eneo la Hifadhi la Loliondo lililopo katika tarafa ya Loliondo.[153]

Wakazi wa NCA wanaeleza namna mahusiano baina ya askari wanyamapori wa NCAA na wanajamii yalivyoharibika tangu serikali ilipoanza kutekeleza mpango wa kuwahamisha watu mwaka 2022. Walisema pia kuwa askari wanyamapori wamekuwa wakiwashambulia na kuwapiga watu waishio maeneo hayo. Human Rights Watch iliandika angalau matukio 13 ya tuhuma za watu kupigwa na askari wanyamapori wa NCAA kati ya Septemba 2022 na Julai 2023. Wakazi wanasema kuwa matukio haya ya ukatili yameshika kasi kipindi cha Septemba 2022.[154]

Mkazi mmoja wa NCA alieleza namna maaskari wanyamapori wa NCAA walivyompiga Rafiki yake mwenye umri wa miaka 35 mnamo Septemba 2022 akiwa njiani kuelekea kwenye msiba wa mjomba wake katika kata ya Nainokanoka:

Alikua anatembea, wakamuhadhibu tu. Walimfanya achutame kichura [mtindo wa chura], na wakampiga kwa kutumia fimbo. Alipata majeraha kwenye miguu yake. Hatuna mahali popote pa kutoa taarifa. Unaenda kwa polisi wale wale waliompiga, kwa hivyo huwezi kupata msaada wowote. Kuna kesi nyingi kama hizi. Askari wanyamapori hawa ni kama watu walio juu ya sheria.[155]

Mwezi huo huo, askari wanyamapori wawili walimpiga mkazi mwingine, Letee Ormunderei, nyumbani kwake kata ya Ngoile katika eneo la NCA, na kumvunja miguu. Mwanaharakati alisema mmoja ya askari wanyamapori alimuambia Ormunderei, “Tunataka uende Msomera.”  Inadaiwa shambulio hili lilitokea kwa sababu Ormunderei  anamiliki pikipiki, ambayo wakazi wa NCA hawapaswi kumiliki ndani ya hifadhi ya Taifa.[156]

Human Rights Watch pia iligundua tukio la askari wanyamapori aliyemshambulia mtoto ambalo halikushughulikiwa. Mnamo Julai 13, 2023, askari wanyamapori wa NCAA alituhumiwa kumpiga kijana wa miaka 15- Joshua Oleparoto, kumvunja meno na kitako cha bunduki, kwa kuwa alikuwa analisha mifugo katika eneo la Ormoti, sehemu ambayo wakazi hawaruhusiwi kuchunga mifugo yao.[157] Kwa mujibu wa Wakili anaeifahamu kesi hii, Oleparoto alitoa taarifa na kumtambua askari wanyamapori huyo kwa polisi, lakini mpaka wakati ripoti hii inaandikwa, polisi hawakuwa wamefuatilia na Oleparoto au kumshtaki askari wanyamapori huyo kwa kosa lolote.

Wanawake kadhaa walisema kuwa kabla ya kuanza kwa zoezi la kuwahamisha, wanawake walikuwa wanaweza kujenga nyumba ndogo kwa ajili yao, hususan pale mke mwingine anavyoongezeka katika ndoa yao, lakini sasa hawaruhusiwi kujenga nyumba hizo tena. Mwanamke mmoja alisema:

Mwanamke ukijaribu kujenga nyumba ndogo, askari wanyamapori wanakupelekea polisi. Polisi wanakutaka ulipe faini. Faini yenyewe haina kiwango maalumu, haifanani, na wakati mwingine wanakufikisha mahakamani.[158]

Mwanamke mwingine alieleza, “Hapo awali, tulikuwa tunakata miti kwa ajili ya kujenga nyumba zetu bila shida. Lakini sasa, kama nyumba ikibomoka na ukaonekana unakata mti, unafuatiliwa mpaka ukamatwe na kuwekwa kizuizini.”[159]

Wakazi wengine walisema kuwa askari wanyamapori wa NCAA walianza kuwanyanyasa wanawake na wasichana kwa kuokota matawi ya miti iliyokufa kwa ajili ya kuni. “Wanawake wanaookota kunia wanashikiliwa, mapanga yao yanataifishwa,” Mzee mmoja Endulen alisema. “Sasa hivi askari wanyamapori wanazuia kila kitu, ikiwa ni pamoja na kuchukua nguzo kwa ajili ya kuweka uzio kulinda mifugo yetu dhidi ya Wanyamapori.”[160] Wakati wa ziara ya Human Rights Watch eneo la NCA mwezi Juni 2023, wasichana wanookota matawi ya miti kwa ajili ya kuni walitahadharishwa kuwa makini na waangalifu, kuepuka kukutana na askari wanyamapori na kunyang’anywa mapanga yao.

Askari Wanyamapori wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro

Sheria kadhaa zinaruhusu “maafisa waliodhinishwa” ikiwa ni pamoja na askari wanyamapori wa NCAA, kuwa na mamlaka ya:

  1. Kubeba na kutumia silaha za moto katika kutekeleza majukumu yao,[161]
  2. Kupekua na kukamata, bila ya kuwa na hati yoyote,[162]

3.      Kumuweka mtu kizuizini na kumpeleka “bila ya kuchelewa kwenye mahakama yoyote ya karibu.”[163] 


 

Changamoto za Kuhamishiwa Kijiji cha Msomera

Mababu zetu waliondoka Serengeti kwa ajili ya uhifadhi. Baba zetu walikuwa wakiishi ndani ya bonde [Ngorongoro] na wakaondolewa huko. Tumechoka kuhama. Tuna wasiwasi kuwa wakituhamishia Msomera pia watakuja kutuondoa. Tunataka kuwa na maisha thabiti.[164]


– Simon M., Diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023

Mpango wa Serikali ya Tanzania wa kuwahamisha watu unahusisha kuwahamisha Wamasai wa Asili kutoka Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, kuelekea mashariki takribani kilomita 600 hadi Kijiji cha Msomera kilichopo Wilaya ya Handeni, mkoa wa Tanga. Mpango huu wa kuwahamisha umetekelezwa bila ya mchakato wa FPIC na mashauriano hafifu pamoja na kukosekana utaratibu wa kupeana taarifa za kutosha na wakazi wa pande zote. Kuna vijiji 91 katika wilaya ya Handeni, ambapo Msomera ndio Kijiji pekee kihistoria kinachokaliwa na jamii ya wafugaji, ikiwa ni pamoja na Wamasai.[165] Hadi kufika mwaka 2022 iliripotiwa kuwa na idadi ya watu wapatao kaya 200 na watu 7,000.[166]

Serikali inakadiria kuwa kufika Januari 2023, zaidi ya kaya 500, pamoja na watu 3,000 na mifugo 15,300, walikuwa wamehamishwa kutoka eneo la NCA kwenda Kijiji cha Msomera.[167] Human Rights Watch iligundua kuwa kuhamishwa kwao kulikuwa na madhara mengi, ikiwa ni pamoja na uwezo wao wa kuendeleza mahusiano ya karibu na familia na jamaa zao walioamua kubaki.

Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika uhamishaji huo na imezipatia kaya zilizohama nyumba na ardhi kwa ajili ya kilimo. Vile vile inatoa mafao mengine. Afisa wa Serikali na baadhi ya wakazi waliohamia Msomera ambao wamezungumza na Human Rights Watch walisema kwa kila kaya serikali hutoa msaada wa kuhamishwa, hii ni pamoja na usafiri, fedha taslimu kiasi cha kati ya shilingi milioni 10 hadi 19 ($3,964 to $7,532), takribani kilogramu 200 za mahindi, heka 5 hadi 7 za ardhi kwa ajili ya makazi na kilimo na nyumba Msomera.[168] Hata hivyo, wakazi waliohamia wanasema nyumba ni ndogo, haziendani na utamaduni wao na hazitoshelezi kwa familia kubwa. Walisema kuwa karibu mifugo yote waliyohama nayo kutoka NCA imekufa, labda kutokana na uhaba wa maji kipindi cha kiangazi, kwani wamelazimika kunywesha mifugo yao maji ya chini ya ardhi yenye chumvi.

Barabara za vumbi zilizojengwa na mamlaka katika eneo hilo zilikuwa zikitunzwa wakati Human Rights Watch walipotembelea Msomera mwezi Juni 2023. Aidha walikuwa wamejenga miundombinu mipya kama vile shule, zahanati, ofisi za posta, kituo cha polisi, mfumo wa kusambaza maji, umeme na minara ya simu za mkononi kwa ajili ya kuhudumia eneo hilo, wakati wakiendelea kukarabati ile ya zamani.[169]

Licha ya uwekezaji huu, Human Rights Watch waligundua kuwa zoezi la uhamaji lilikuwa na matatizo, kwa sababu watu waliohamishwa hawakushirikishwa vya kutosha, na wakazi wa Msomera waliokuwepo toka awali wanaondolewa Msomera. Wakazi waliohama NCA hawakuwa wamepata msaada wa kutosha kutoka kwa serikali kuhamia Msomera kama inavyoelezwa hapa chini.

Wakazi Waliopo Msomera

Wakazi wa Msomera walioathirika na uhamiaji huo wanajitambulisha kama Wamasai, wafugaji ambao wameishi na kutumia ardhi hiyo kwa miongo kadhaa, lakini sio wakazi wa asili wa eneo hilo. Angalau familia ya mkazi mmoja ina hati za serikali zinazothibitisha dai lao la ardhi wanayoishi na kutumia. Hata hivyo, serikali haikushauriana na wakazi wa Msomera kuhusu mpango wa kuwahamishia watu kutoka NCA kwenda kweny eneo na ardhi wanayoishi na kulima. Badala yake, walikatishwa tamaa na kutishwa wanapouliza maswali na kuitwa “wavamiaji” ijapokuwa familia zao zimekuwa zikitumia ardhi hiyo kwa miongo kadhaa. Bila ya kuwashirikisha wale walikokuwa tayari wanaishi Msomera, watu kutoka NCA walihamia Kijiji hapo, na kupelekea migogoro juu ya ardhi na rasilimali nyingine.

Vitongoji vya kijiji cha Msomera, tarafa ya Misima, wilaya ya Handeni district,[170] mkoa wa Tanga

1. Tongoji Ormoti

2. Kati kati

3. Orokong’u

4. Tembo

Mashaurino Hafifu na Vitisho kutoka kwa Mamlaka

Baadhi ya wakazi wa Msomera waliiambia Human Rights Watch kuwa mpaka serikali ilipoanza kuweka mipaka na kuanza ujenzi Msomera mwezi Februari 2022, hawakuwa na taarifa kuwa eneo hilo lilikuwa limetambuliwa na kutengwa kwa ajili ya kuwapokea watu waliokuwa katika mpango wa kuhamishwa na serikali kutoka NCA. Serikali haikufanya vikao vya mashauriano na jamii ambayo itaathirika moja kwa moja na zoezi la kuwahamisha watu au kujadili mipango hiyo. Badala yake, serikali ilitumia mchanganyiko wa wakandarasi na watu wenye silaha kupima maeneo, kuweka mipaka, kujenga majengo na kuwahamisha watu wapya kutoka NCA katika ardhi iliyokuwa inatumika hapo awali na wakazi wa Msomera, kama inavyoelezwa hapa chini.

 

Wakazi wa Msomera walisema kuwa siku moja mwezi Februari 2022 waliona msafara wa magari yapatayo 60 ukiingia kijijini, pamoja na magari yaliyokuwa na Wakuu wa Mikoa kutoka Mikoa ya Tanga, Arusha na Manyara. Abiria “walikuja na kuangalia na kuondoka… na hawakuzungumza na sisi,” mkazi mmoja wa kitongoji cha Tongoji Ormoti alisema.[171]

Siku chache baadae, wanajeshi wenye silaha na wapimaji waliwasili, wakajenga na kuanza kuishi kwenye kambi katika eneo hilo. Wakazi wanasema wapimaji wakaanza kupima, kuchora ramani na kuweka mabango ya tahadhari katika Kijiji cha Msomera. Ndani ya siku kadhaa, wakandarasi wa serikali wakaanza kujenga nyumba pale kijijini. Maafisa wa serikali na wakandarasi hawakutoa taarifa au maelezo yoyote kwa wakazi wa Msomera.

Mkazi mmoja alisema:

Tulishangaa tulipoona msafara wa magari. Kisha wanajeshi wakawa wanazunguka na bunduki. Niliwaona watu wanakuja, na walipima hadi nyumba yangu. Wanajeshi hawakuwahi kuwasiliana nasi. Wapimaji walipoanza kusimika mawe, tuliwafuata huku tukisema, “Hap ani nyumbani kwangu! Hili ni shamba langu! Mnafanya nini?” Wapimaji hao walisema wao ni watumishi wa umma tu, hawana uwezo wa kusitisha, walitumwa hapa, na tunapaswa kuzungumza na Mkuu wa Mkoa au Wilaya.[172]

Wakazi walisema kuwa walipouliza kwa Mkuu wa Mkoa na Wilaya, waliitwa “wavamizi” na “wajenzi holela.” Mkuu wa Mkoa na Wilaya walisema eneo hilo ni eneo la hifadhi na mali ya serikali, kwa ajili ya serikali kutumia ipendavyo.[173]

Mkazi huyo huyo alisema kuwa wakati wa mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Handeni wa wakati huo, aliwatishia kuwakamata na kuwazuia kuuliza maswali.[174] Mkazi mwingine aliyeshiriki mkutano anakumbuka mkuu wa mkoa na wilaya wakisema, “nyie wote ni wavamizi na mkiendelea kuuliza maswali, mtafukuzwa.”[175] 

Wakazi wengi walisema kuwa wamepoteza haki ya ardhi ambayo familia zao zimekuwa zikitumia kwa kilimo na kuchunga mifugo kutokana na ardhi hiyo kugaiwa na kuwa makazi ya familia zilizohamia, na nyingine kujengwa majengo mapya ya huduma na miundombinu mingine. Mkazi mmoja alisema kuwa mawe na vibao vya alama viliwekwa katika ardhi yao yote. “waliweka mawe ya mipaka hadi mbele ya mlango wangu, hii inamanisha sitakiwi kuwa hapa,” alisema. “Tunazungukwa na mawe ya mipaka na kuna mawe yamesimikwa ndani ya maboma.”[176]  Mkazi mwingine alikumbana na kadhia hiyo pale serikali ilipogawa ardhi ambayo familia yake imekuwa ikitumia kwa miongo kadhaa na kujenga nyumba kwa ajili ya kaya zaidi ya dazeni mbili kutoka NCA, na miundombinu ya kuwahudumia, bila ya kushauriana naye au familia yake. Wamebakiwa na boma lao na kuzungukwa na wakazi wapya waliohamia.

Alisema:

Nilizaliwa hapa. Babu yangu alizaliwa hapa… Sisi ni familia ya takribani watu 72 yenye babu na bibi, wake, watoto. Hakuna ardhi ya kutosha kulisha kila mtu katika familia yetu. Sasa tunategemea ng’ombe wetu pekee, ambao tunawaweka mbali na hapa kwa sababu hakuna mahali pa malisho. Baadhi ya wanafamilia wamehamia mjini kwa ajili ya kazi kwa sababu ya ukosefu wa ardhi ya kulima.

Aliongeza kuwa ardhi ya Kijiji imesajiliwa na mamlaka husika, ikiwa na nyaraka rasmi zinazothibitisha haki yake katika ardhi hiyo. Mkuu wa Mkoa na Wilaya hawakushawishika, “Wote walisema sisi ni wavamizi, na kwamba Kijiji chetu kilisajiliwa kimakosa.”[177]

Kufikia Julai 2023, serikali ilikuwa imehamisha familia kutoka NCA kwenda kwenye nyumba zilizoko kitongoji cha Tongoji Ormoti na Orokung’u Kijiji cha Msomera, na ilianza kujenga nyumba zaidi,[178] kuanzia kitongoji cha Kati Kati. Wakazi wa Kati Kati waliiambia Human Rights Watch wameona watu “wakija na kuangalia” katika aina ile ile ambayo maafisa wa serikali walifanya kabla hawajaanza kujenga nyumba katika vitongoji vingine. Mkazi mmoja alitambua kuwa shamba lake limechukuliwa baada ya serikali kuanza ujenzi:

Shamba langu litachukuliwa. Hatua inayofuata ni kuendeleza sehemu lilipo shamba langu. Najua kwa sababu wamejenga pampu za maji katika eneo hilo na hiyo sio kawaida. Hakuna taarifa yoyote kutoka kwa serikali na siruhusiwi kusema chochote.[179]

Migogoro baina ya Wakazi Waliopo na Wale Waliohamia

Wakazi wa Msomera waliiambia Human Rights Watch kuwa kuhamishwa kwa watu kutoka NCA kumepelekea migogoro baina ya jamii mbili, kutokana na uhaba wa ardhi ya kulima na kulisha mifugo. “Mahusiano na watu kutoka Ngorongoro ni mabaya sana,” mkazi wa Msomea alisema. “Wanachukua maeneo yetu, mashamba yetu, nyumba zetu.”[180] Baadhi wanaeleza tukio ambalo mkazi wa Msomera alikamatwa “kwa sababu alipigana na mwanamke mwingine [ambaye alihamia Msomera kutoka NCA] kwa kulima katika ardhi yake.”[181]

Wakazi hawa walisema hawakupokea taarifa yoyote kutoka kwa mamlaka kuhusu fidia kwa ardhi waliyopoteza kwa wakazi waliohamia kutoka Ngorongoro.[182]

Sheria na Kanuni za Tanzania zinaelekeza kulipa fidia ambayo ni “kamili na ya haki.”[183] Chini ya Kanuni ya 7 ya Kanuni za Ardhi (Uthamini wa Thamani ya Ardhi kwa ajili ya Fidia) za mwaka 2001, fidia kwa upotevu wa umiliki wa ardhi ni pamoja na thamani ya maboresho yasiyokamilika, posho ya usumbufu, posho ya usafiri, posho ya malazi na upotevu wa faida.[184]

Kuhamishwa kwa Wamasai kutoka Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro

Wakazi wa NCA waliohamia Msomera walisema kuwa walichagua kuhama kwa sababu ya ugumu waliokabiliana nao wao na familia zao katika eneo la NCA kutokana na vikwazo vya serikali vilivyowekwa kwa muda, hususan hivi karibuni kuanzia Februari 2022.

Changamoto nyingine kwa familia zilizohama ni pamoja na mkuu wa kaya kuwa ndio mwenye wajibu wa kuandikisha familia kuhama, hali inayochochea ukosefu wa usawa wa nani anayeamua kuwa familia itabaki au kuondoka, uduni wa kushauriana kuhusu makazi Msomera, fidia isiyotosha kwa watu waliohama na upatikanaji duni wa maji.

Vigezo vya Kujisajili kwa ajili ya Kuhama

Katika mchakato wa kuhama, serikali ilitumia kigezo cha mkuu wa kaya na kudhani kuwa wana kaya wote wanafanana, bila ya kutofautisha mahitaji na haiakisi uhalisia wa changamoto za kaya, ambazo nyingi ni za wake wengi, vizazi mchanganyiko na wanakaya mchanganyiko. Maamuzi ya kumchangua mkuu wa kaya yanampa nguvu mwanaume bila kukusudia, jambo linalochochea mila ya kandamizi na mbovu zinazomtambua mwanaume kama mkuu wa kaya na mtafutaji mkuu wa kaya na mwenye maamuzi ya mwisho juu ya masuala ya ardhi huku wanawake wakitarajiwa kuwafuata.[185]

Katika eneo la NCA, mkuu wa kaya anasajili familia kwa NCAA au ofisi Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya, kuonyesha utayari wao wa kuhamia Msomera. Bila ya kujali maoni ya wanakaya wengine, makazi ya familia huharibiwa baada ya kuhama kwa sababu “katika jamii ya Wamasai, mume anapoamua, hata kama wake hawakubaliani na maamuzi yale, wote inabidi waondoke,” kwa mujibu wa mjumbe wa Baraza la Wafugaji la Ngorongoro ambaye anafahamu mila za Wamasai.[186]

Kutegemea mtu mmoja kusajili familia kunapelekea changamoto kubwa kwa wanakaya wa familia moja ambao wanataka kubaki NCA na wale wanaochagua kuondoka. Wakazi walisema kuwa wanafamilia ambao huchagua kubaki NCA wanakosa makazi na kulazimika kuhamia kwa ndugu. Wake ambao hukataa kuwafuata waume zao wakati mwingine hukabiliana na unyanyapaa kutoka kwa jamii. Wakati wa mahojiano ya kikundi Endulen, mtu mmoja alieleza taarifa ya mke kukataa kuhama kwa sababu hakushirikishwa kwenye kufanya maamuzi:

Mwanaume alishiriki kwenye mchakato bila ya kushirikishana. Mmoja ya wake zake alikataa kwa sababu hakushirikishwa kwenye kufanya maamuzi. [Wao] serikali wakamuhamisha mume na wake wengine na Watoto. Hii ilivunja familia. Ni jambo lililotokea hivi karibuni.[187]

Kikundi kiliwatambua wanawake wengine saba katika vijiji vya NCA ambao wamekumbana na hali kama hiyo na kukataa kuhama na waume zao.

Hakuna dalili kuwa mpango wa serikali wa kuwahamisha na kutoa makazi mapya ulihusisha masuala ya jinsia na ushirikishwaji wa wanajamii ili kuondoa kushamiri kwa ukosefu wa usawa kati ya wanaume na wanawake.

Mashauriano Hafifu Yaliyopelekea Makazi Yasiyokidhi Utamaduni

Kila ambacho mamlaka inakitoa kwa wanaohama hakiakisi muundo wa familia za Wamasai. Wakazi wa NCA, wale waliohamia Msomera na wale waliobaki, walisema hawakuombwa ushauri kuhusu nyumba walizopewa, ambazo zilikuwa hazikidhi ukubwa wa famili zao na aina ya maisha yao ya kiutamaduni.

Kiongozi wa kimila wa NCA alifafanua:

Kuhamia Msomera kutakuwa na changamoto zake kwa utamaduni wetu. Unaenda Msomera na una nyumba ndogo ya vyumba vitatu: utakuwa unaishi na mke wako, Watoto na wake wa Watoto wako na wajukuu. Katika utamaduni wa Wamasai, huu ni mwiko na ni jambo lililokatazwa kabisa. Ni kama kuua utamaduni.[188]

Kutoa nyumba moja kwa mkuu wa kaya aliyehama na wake zake na wanafamilia wengine ni jambo ambalo ni kinyume na utamaduni wa familia za Wamasai. Mwanamke mmoja alisema, “Tunayo nyumba moja tu, na tuko wake wawili. Wake wawili wa Kimasai hawawezi kuishi kwenye nyumba moja.[189]

Human Rights Watch ilitembelea Msomera mwezi Juni 2023. Nyumba zimejengwa kwa matofali, paa la bati na antena ya satelaiti. Nyumba hizi ni ndogo, zenye vyumba viwili hadi vitatu, zilizojengwa kwa ajili ya familia ndogo ya watu watatu hadi watano.

Baadhi ya familia za Wamasai zilizohama ziliiambia Human Rights Watch kuwa nyumba hizo hazikidhi idadi ya watu iliyopo kwenye familia zao zinazohusisha vizazi mchanganyiko na wanafamilia wengi na hakuna nafasi ya upanuzi wa nyumba hapo baadae.

Mwanamke mmoja alisema:

Tulipokuwa tunaishi Ngorongoro, mtoto wangu wa kiume alikuwa na nyumba mbili, na tuliposajiliwa kuhama mtoto wangu hakuwepo. Siku ya kuondoka, nyumba yangu pamoja nay a mtoto wangu zilivunjwa. Tumekuja hapa, na mtoto wangu hajapata fidia. Tunaishi pamoja na familia yake na watoto wake. Kuna familia mbili zinazoishi katika nyumba moja ya vyumba vitatu.[190]

Wakazi wanasema kuwa wamelalamika kwa mamlaka kuhusu changamoto ya makazi, lakini serikali haijachukua hatua yoyote kutafuta suluhisho. Wakati Human Righst Watch ilipotembelea eneo hilo, baadhi ya wakazi walitumia fedha zao kufanya upanuzi wa nyumba. Mkazi mmoja alijenga nyumba kubwa ya matofali katika eneo alilopewa, na wengine walijenga au walikuwa wanapanga kujenga nyumba kadhaa katika muundo wa maboma ya Wamasai.

Pamoja na kuelezwa changamoto ya nyumba hizi, serikali imendelea kujenga nyumba mpya kwa muundo huo huo wa awali na kuongeza wigo wa mradi kufikia wilaya mbili. Msemaji wa serikali alinukuliwa katika vyombo vya habari: “Awamu ya pili [ya ujenzi] ilianza mwezi Julai [2023] na kuendelea hadi Machi, lengo likiwa kujenga nyumba 5,000 katika eneo lote, ikiwa ni pamoja na Sauni, Kitawi na Msomera. …katika awamu hii ya pili, tunatarajia kujenga nyumba angalau nyumba 5,000, ambazo 2,500 zitajengwa Msomera, 1,000 Sauni, wilaya ya Kilindi na 1,500 Kitawi, wilaya ya Simanjiro.”[191]

Fidia Isiyotosheleza

Wakazi wa NCA waliohama waliiambia Human Rights Watch kuwa pesa ambayo walipewa na serikali haikuwa inatosha kugharamia matumizi yao wakati wa kuhamia Msomera, sehemu ya pesa hiyo ilitumika kujenga nyumba za ziada kwa ajili ya wake na wanafamilia wengine.

Mkazi aliyehamia alisema:

Fedha nyingi imetumika kwenye kuandaa mashamba – kusafisha mapori kumegharimu fedha nyingi. Kuanzisha shamba ni gharama kubwa, huwezi kulima bila kuweka uzio, kuna wanyama kama tembo, punda, mbwa, ambao ukilima wanapita na kuharibu mazao. Inabidi uweke uzio kwa kutumia miti yenye miiba. Ni gharama kubwa.[192] 

Mkazi mwingine aliyehamia anaelezea ugumu waliokumbana nao baada ya kujenga nyumba:

Sina mtaji wowote uliobaki. Tumetumia pesa yote kujenga nyumba kwa ajili ya vijana [ndugu] ambao hawana nyumba, na watoto wangu wako shule. Pia tunapakumbuka Ngorongoro kwa kuwa hata kama mvua isiponyesha, na tusipolima, tunaweza kuuza mbuzi kwa kuwa wanastawi kule. Tuliwafundisha watoto wetu, na maji ni mazuri [kule NCA], lakini hatuwezi kunywa maji ya hapa Msomera kwa sababu yana chumvi nyingi.[193]

Serikali imegawa heka mbili pekee za ardhi kwa kila kaya iliyohama kutoka NCA. Heka hizi ni ndogo mno ukilinganisha nae neo kubwa la kufuga lililokuwa linapatikana kule NCA, na kinyume kabisa na rasilimali asili za NCA na ufugaji. Mjumbe wa Baraza la Wafugaji la Ngorongoro alieleza asili ya wafugaji kuishi kwa kushirikiana na namna mpango wa serikali ulivyoangalia mtu binafsi kinyume kabisa na mfumo wa maisha ya wafugaji:

Kama wafugaji tuna eneo dogo la ardhi kwa ajili ya kilimo cha mazao nae neo lingine ni kwa ajili ya jamii yote. Lakini mpango wa serikali wa makazi mapya unakupa heka mbili kwa ajili ya nyumba yako na heka tatu hadi tano kwa ajili ya kilimo. Watu walipokea fidia ya fedha kulingana na uwezo wao wa kujadiliana na kushawishi. Huko Msomera, wana shule, kituo cha polisi lakini hakuna chochote kwa ajili ya maisha yao.[194]

Alisema: “Kuliko kuzungumza na mtu mmoja mmoja, serikali ilipaswa kuzungumza na jamii kwa ujumla.”[195]

Msemaji mkuu wa serikali aliviambia vyombo vya habari kuwa kwa kila familia iliyohama serikali inatoa:

1.       Nyumba ya vyumba vitatu katika eneo la heka mbili na nusu, na heka tano kwa ajili ya kilimo na kuweka mifugo, pamoja na hati za umiliki wa ardhi  au nyaraka za umiliki.

2.      Shilingi milioni 10 ($ 3,700), ijapokuwa alisema kuwa kabla ya kuwahamisha wakazi, serikali hufanya tathmini ya mali zao kwa ajili ya fidia.

3.      Usafiri kwa mali zao zote kwenda kijiji kipya.[196]

Upatikanaji Mbovu wa Maji na Upotevu wa Mifugo na Mazao

Upatikanaji wa maji umekuwa changamoto kubwa kwa wakazi wapya wa Msomera, ambao wanategemea maji kwa ajili ya mifugo na mazao yao. Kipindi kirefu cha ukame mwaka 2021 na 2022 kukiwa na mvua kidogo na wakati mwingine isiwepo kabisa ni sababu zilizopelekea upungufu wa upatikanaji wa maji.[197]

Baadhi ya wakazi waliohamia waliiambia Human Rights Watch kuwa ng’ombe na mbuzi waliokuja nao kutoka Ngorongoro wamekufa tangu walipofika Msomera. Takribani nusu ya mazao waliyopanda katika mashamba waliyopewa na serikali yameshindwa kustawi. Wanalaumu uwepo wa mvua kidogo, ukosefu wa mito na maji yasiyo na ubora katika eneo hilo kwa upotevu huo.

Angalau wakazi wawili walisema kuwa maji pekee yanayopatikana ni ya chumvi, na kwamba wingi wa kiasi cha chumvi unaweza kuwa ndio sababu ya vifo vya mifugo yao na kushindwa kustawi kwa mazao yao.[198]

Human Rights Watch haikufanya vipimo vya maji katika eneo hilo kuthibitisha kiasi cha chumvi au kubainisha uhusiano uliopo na vifo vya mifugo na mazao.

 Albert Msendo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, aliiambia Human Rights Watch kuwa serikali ilitoa matenki na pampu ambazo zinaweza kutoa hadi jumla ya lita 500,000 za maji kwa ajili ya matumizi ya watu na mifugo na wanachimba visima zaidi katika eneo hilo. Serikali pia imelenga kukabidhi kwa ajili ya matumizi ya jamii hifadhi ya maji kwa ajili ya mifugo mwezi Mei 2023.[199]


 

Mashambulizi dhidi ya Wakosoaji wa Uhamisho

Hauruhusiwi kusema chochote. Hata hapa, watu wanakuja, lakini wana hofu mioyoni mwao.


— Samson L., Msomera, Juni 24, 2023.

Serikali ya Tanzania imewanyamazisha wakosoaji wa zoezi la kuwahamisha watu, jambo linalochangia hali ya hofu. Wakazi wa NCA na Msomera na watetezi wa haki za binadamu waliiambia Human Rights Watch hawawezi kuzungumza hadharani kwa kuhofia kulipizwa kisasi na mamlaka.

Kukamatwa kwa Watetezi wa Haki za Binadamu

Wakaazi wa NCA ambao wanapinga kuhamishwa na waliojipanga kupaza sauti kuhusu hilo, walisema kuwa mamlaka iliwatishia na wakati fulani kuwakamata kwa kukosoa vitendo vya serikali. "Kwa kawaida hututisha," kiongozi mmoja wa kijamii alisema. “Tunapigiwa simu nyingi. Wanasema, ‘Kwa nini unazungumza kuhusu serikali?’ Lakini sisi hatujali.”[200]

Juni 30, 2022 mamlaka ilimkamata Simon Saitoti, diwani wa kata NCA na kumfungulia mashtaka ya kumuua Garlius Mwita, askari polisi, Juni 10 katika tarafa jirani ya Loliondo, kaskazini mwa NCA.[201] Wiki chache zilizopita, Saitoti alikuwa amesambaza ripoti inayodai kuwa serikali ilikuwa imesambaza chumvi yenye sumu kwa wakazi wa NCA kwa ajili ya mifugo yao. Mnamo Novemba, mamlaka ilifuta mashtaka dhidi ya Saitoti na wengine 23 ambao walikuwa wamekamatwa na kushtakiwa kwa mauaji ya polisi huyo.

Mnamo Agosti 15, 2023, vikosi vya usalama vilikamata wanajamii 39 wakati wa mkutano wa jamii katika kijiji cha Endulen, eneo la NCA, kupinga kupunguzwa kwa huduma za umma, kama vile NCAA kukataa kutoa vibali vya kukarabati shule katika jamii zao.[202] Mamlaka iliwashutumu kwa kuwashambulia “waandishi wa habari” waliokuwa wakihudhuria mkutano huo.[203]

Wakazi wa NCA na Msomera walisema hawawezi kuzungumza kwa hofu ya kunyanyaswa au kukamatwa. Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 31 wa kitongoji cha Orokung'u kilichopo Msomera alisema kuwa baada ya serikali kuanza kuwahamisha wakazi wa NCA kwenda Msomera bila kushauriana wala kupata ridhaa ya wakazi waliopo Msomera, mwezi Mei 2023 yeye na watu wengine waliunda kikundi cha kuzungumza na vyombo vya habari na "kuiambia serikali kuacha kile kilichokuwa kinandelea.”[204] Mtu huyo alisema wiki moja baada ya kuanza hivyo, polisi waliwaita kituo cha polisi Handeni ambako walihojiwa na kutakiwa kuacha kuzungumza hadharani.[205]

Vikwazo kwa kazi za NGOs na vyombo vya habari

Wafanyakazi wa NCAA waliopo katika mageti ya kuingia NCA wamewakatalia au kutoza mashirika ya asasi za kiraia ada ya kuingia, ambapo awali haikuwa hivyo, na askari wanyamapori wamekuwa wakifuatilia kwa karibu nyendo a shughuli za wale wanaoruhusiwa kuingia. Wawakilishi wa NGO walisema wanaamini kuwa vikwazo hivi vimewekwa kuwakatisha tamaa mashirika ya asasi za kiraia kutoa ufahamu kuhusu mchakato wa kuhama na haki za jamii inayoathirika.

Mwakilishi wa NGO alisema kuwa kabla ya 2021, shirika lako lilikuwa linapata kibali cha kuingia NCA na kukutana na jamii bila ya kulipa ada yoyote.[206] Mwaka 2021, walianza kulipa ada ya mwaka. Tangu kuanza kwa mchakato wa kuhama unaofadhiliwa na serikali Juni 2022, wafanyakazi wa NGO hiyo walisema wamekuwa wakikataliwa kuingia. Mwakilishi kutoka NGO nyingine alithibitisha taarifa hii kuhusu takwa jipya la NGO kulipa ada ya kuingia.[207] Mwaka 2021, walitakiwa kulipa ada ya mwaka kiasi cha shilingi 118,000 ($46) kwa ajili ya magari yao, na baada ya februari 2022, walitakiwa kulipa ada kwa kila mfanyakazi ($10, ada ya kuingia kwa Watalii wa Kitanzania), na ada ya ziada kwa kila gari kulingana na uzito wa gari, kama ilivyo kwa magari ya utalii.[208]

NGOs ambazo zimeruhusiwa kuingia zimekabiliana na unyanyasaji. Wawakilishi wa NGO ya pili walisema kuwa wafanyakazi wao walikuwa wanafuatiliwa na askari wanyamapori na kuulizwa maswali kuhusu shughuli wanazofanya wakati wakitekeleza mradi katika eneo la NCA.[209] Mwezi Machi 2024, Joseph Oleshangay, wakili wa haki za binadamu Mmasai alieyajiriwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na mkosoaji mkubwa wa uhamishaji NCA, alilazimika kukimbilia nchi ya Kenya kwa kuogopa kuwa usalama wake uko hatarini.[210]

Mamlaka pia zimezuia vyombo huru vya habari kufika NCA.Mwezi January 2022, polisi waliwaweka kizuizini kwa muda mfupi kundi la waandishi wa habari waliosafirishwa kwenda NCA na kikundi cha wazawa. Doreen Ajiambo, mwandishi wa habari anaefanya kazi na Global Sisters Report (GSP), chombo cha habari cha Wakatoliki, alikamata na vyombo vya usalama katika eneo la NCA na kushikiliwa na saa kadhaa kwa kuwahoji wakazi wa Kimaasai na alilazimishwa kufuta sauti na picha alizorekodi kama masharti ya kuachiwa.[211] Kwa mujibu wa mfanyakazi wa NGO inayotetea haki za Wamasai, vyombo vya habari haviko tayari kutoa habari inayokinzana na habari ya serikali kwa kuogopa kulipizwa kisasi.[212] Matokeo yake, masuala yanayowakabili jamii katika eneo la NCA yamepata nafasi finyu au kukosa kabisa nafasi katika vyombo vya habari vya ndani.

Majukumu ya Kisheria ya Tanzania

Mchakato wa kuwahamisha watu kwa ajili ya uhifadhi nchini Tanzania umekiuka haki ya jamii ya Wamasai wa Asili katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na wakazi wa vijijini katika Kijiji cha Msomera, eneo walilohamishiwa. Kwa kufanya hivyo, serikali ya Tanzania imeshindwa kutimiza wajibu wake kitaifa, kikanda na kimataifa wa haki za binadamu.

Chini ya sheria za kimataifa za haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR) na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (ICESCR), serikali ya Tanzania inawajibika kuheshimu, kulinda na kutimiza haki ya wakazi wake, ambao ni pamoja Wamasai wa Asili na wamiliki wa haki za ardhi vijijini na kuepuka kuhatarisha haki yao moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja.[213] Tanzania, nchi mwanachama wa Umoja wa Afrika, pia imeridhia mikataba kadhaa ya kikanda ya haki za binadamu, ambayo ni pamoja na Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu (Mkataba wa Afrika).[214] Katiba ya Tanzania na sheria za kitaifa pia zinaratibu haki husika.[215]

Ulinzi kwa Wamasai wa Asili katika Hifadhi ya Ngorongoro  

Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro yam waka 1959, na marekebisho yaliyofanyika, inaeleza kuwa, Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) inawajibu wa kuwalinda na kukuza maslahi ya Wamasai wanaojihusisha na ufugaji wa ng’ombe na na uzalishaji wa maziwa katika eneo la NCA.[216] Sheria hiyo inawapa Wamasai haki ya maslahi yao kuzingatiwa na NCAA.[217]

Sheria za Tanzania zinahakikisha haki ya ardhi, mashauriano, fidia, na uhuru wa kujieleza, na zinalinda hadhi ya jamii ya Wamasai katika eneo la NCA. Katiba ya nchi inaamuru kwamba serikali na vyombo vyake “kuelekeza sera na shughuli zao katika kuhakikisha … heshima ya binadamu inahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu Haki za Binadamu.”[218]

Haki ya Kumiliki Mali na Ardhi, Pamoja na Haki za Kimila za Ardhi  

Sheria za Tanzania zinahakikisha haki ya kumiliki ardhi, pamoja na haki za kimila za ardhi. Katiba inaratibu haki ya kumiliki mali iliyopatikana kwa njia halali.[219] Sheria ya Ardhi ya 2001 inatambua umiliki wa ardhi kwa mujibu wa umiliki wa kimila na inaeleza kwamba umiliki huo na matumizi ya ardhi kwa ufugaji ni mali kisheria.[220]  Sheria ya Vijiji ya mwaka 2001 inatambua ardhi ambayo imekuwa ikikaliwa na kutumika na Kijiji kwa ajili ya ufugaji na malisho ya mifugo kwa miaka 12 kabla ya kupitishwa kwa sheria kama “ardhi ya Kijiji.”[221] Hivyo, chini ya sheria za kitaifa, Wamasai wa NCA, kama watu binafsi na kama jamii – ambayo imekuwa ikikaa na kutumia ardhi kulisha mifugo vizazi kwa vizazi, muda mrefu hata kabla ya kutungwa kwa Sheria ya Ardhi au Sheria ya Vijiji – kuwa na haki ya umiliki wa ardhi.[222]  

Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu (Mkataba wa Afrika) na Azimio la Dunia la Haki za Binadamu zinalinda haki ya kumiliki mali.[223] Muhimu, vyombo hivi vinalinda watu binafsi na jamii, pamoja na wale wenye hati za kimila, dhidi ya uingiliwaji holela wa haki zao za kumiliki mali na ardhi, na ulinzi huu hautegemei uwepo ya hati rasmi kwa mtu binafsi au jamii. Kamati ya UN ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni, ambayo inatafsiri ICESCR imesisitiza kuwa ulinzi huo unatambulika bila kujali kama mtu ana hati rasmi au la, na “bila kujali aina ya umiliki.” [224]

Sheria za kikanda na kitaifa zimeangazia uhusiano kati ya ardhi na haki za binadamu.[225] Katika kesi ya COHRE v. Sudan,  Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu,ambayo inatoa muongozo wa kimamlaka kwa nchi wanachama wa Mkataba wa Afrika na kusimamia utekelezaji wa Mkataba, iliamua kuwa haki ya mtu kumiliki mali inalindwa iwe wana hati miliki ya kisheria au la.[226] Mahakama za Tanzania pia ziliamua kuwa hati za kimila za ardhi zinahusu “mali halisi inayolindwa na masharti ya ibara ya 24 ya Katiba.”[227]

Kwa kuongezea, Tanzania ilipiga kura kuunga mkono vyombo viwili vya kimataifa vinavyohusiana na haki za Watu wa Asili na watu wanaoishi maeneo ya vijijini. Azimio la UN kuhusu Haki za Watu wa Asili (UNDRIP), ni chombo kinachoeleza kuwa watu wa Asili wana haki ya ardhi waliyoimiliki kimila, kuishi humo au  kuipata kwa njia nyingine.[228]  Azimio la UN kuhusu Haki za Wakulima na Watu Wengine Wanaofanya kazi Vijijini (UNDROP) linazitaka nchi kulinda haki ya wakulima na watu wengine wanaofanya kazi vijijini kuwa “kufikia na kutumia katika njia endelevu rasilimali zinazopatikana katika jamii zao ambazo zinatakiwa ili kufurahia maisha kamili.”[229]

Marufuku ya Kuondoshwa kwa Lazima

Sheria za Kimataifa zinakataza “kuondoshwa kwa lazima.”[230] Kamati ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni katika Maoni yake ya Jumla Na. 7 kuhusu haki ya makazi yanayokidhi, inafafanua kuondoshwa kwa lazima kama kuondoshwa kwa mtu bila ya hiyari kutoka katika makazi au ardhi yao wakati mtu huyo hana njia ya sahihi za kupata ulinzi wa kisheria au ulinzi mwingine. Mamlaka zinapaswa kuhakikisha kuwa “njia zote mbadala zinazowezekana” zinaangaliwa kwa mashauriano na wakazi na kwamba ‘fidia inayokidhi” inatolewa. Kila mtu anapaswa kuwa na haki, na fursa ya dhati, kupinga uhalali wa kuondoshwa.[231] Chomo cha Haki za Binadamu Afrika Kikanda inasisitiza marufuku hii.[232]

Haki ya Utamaduni

Mkataba wa Afrika unaakikisha haki ya utamaduni, unaeleza kwamba “Kila mtu ana uhuru wa kujihusisha katika utamaduni wa jamii yake.”[233] Sheria za kimataifa za haki za binadamu pia zinaeleza haki ya kufuata mfumo flani wa maisha kama sehemu ya haki ya utamaduni.[234] Watu wa asili wana haki ya kutekeleza na kudumisha mila na desturi zao za kitamaduni.[235] Kwa kuzuia ufikaji katika baadhi ya maeneo ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro—ikiwa ni pamoja na katika bonde—ambazo ni sehemu muhimu kwa mila na sherehe za utamaduni za Wamasai, mamlaka imeinyima jamii kupata kipengele muhimu cha utamaduni wao na mtindo wa maisha.

Haki ya Maendeleo

Mkataba wa Afrika unaeleza kwamba “watu wote watakuwa na haki ya maendeleo yao ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kwa kuzingatia uhuru na utambulisho wao na kufurahia kwa usawa urithi wa pamoja wa wanadamu.”[236] Vivyo hivyo, Azimio la UN kuhusu Haki ya Maendeleo linahimiza maendeleo jumuishi.[237] Serikali inakiuka haki ya maendeleo ya Wamasai katika eneo la NCA kwa kushindwa kuwashirikisha ipasavyo katika mipango ya maendeleo na kushindwa kuwahakikishia ustawi endelevu wa jamii ikiwa wanaamua kuhama au la.

Katika uamuzi wa Endorois, Tume ya Afrika ilieleza kuwa haki ya maendeleo ina pande mbili, kuwa ni ya kikatiba na kisheria, au muhimu kama njia ya kufikia lengo au lengo lenyewe.[238] Ukiukaji wa kipengele chochote ni ukiukajai wa haki ya maendeleo.[239] Haki ya maendeleo ni kuhusu serikali kuwapatia watu uwezo wa kuchagua maisha yao ya baadaye,[240] ikiwa ni pamoja wa sehemu ya kuishi, na kuweka mazingira rafiki kwa maendeleo ya watu kuliko kuamua kiholela sehemu watakayoishi Wamasai kwa kuchagua Msomera, kujenga nyumba na kuhamishia familia huko.[241]

Haki ya Kushiriki katika Mchakato wa Kufanya maamuzi, pamoja na Ridhaa Huru, ya Awali na Inayotokana na kuwa na Taarifa (FPIC)

Katiba ya Tanzania inawakikishia raia haki ya kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kufanya maamuzi katika masuala yanayowaathiri, ustawi wao au nchi.[242]

Chini ya Mkataba wa Afrika, serikali inao wajibu wa kuhakikisha inashauriana kwa dhati na jamii kabla ya kufanya mabadiliko katika utoaji wa huduma za umma muhimu kwa haki zao, ikiwa ni pamoja na huduma za afya na elimu. Katika Maoni yake ya Jumla Na. 7, Tume ya Afrika ilisisitiza kuwa serikali inapaswa kutoa majukumu kwa watumishi wa umma kwa huduma zote za kijamii ikiwa za umma au binafsi, na kuhakikisha kwa uchache kuwa wanawajibika kidemokrasia kwa umma.[243]

Kwa watu wa Asili, ushiriki wenye ufanisi unahusishwa na haki ya kujitawala, kipengele muhimu cha majadiliano yoyote kuhusu kufanya mabadiliko ya kufikia, kutumia na kudhibiti ardhi.[244] UNDRIP inaeleza: “Hakuna zoezi la kuwahamisha watu litafanyika bila ya kuwa na ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa [FPIC] kutoka kwa watu wa asili na baada ya kukubaliana kuhusu fidia sawa na ya haki na, pale inapowezekana, kuwa na uamuzi wa kurudi.”[245] Serikali inapaswa kushauriana na kushirikiana kwa nia njema na watu wa Asili wanaohusika kupitia taasisi zao za uwakilishi kutafuta ridhaa yao ambayo ni huru na inayotokana na kuwa na taarifa kabla ya kuidhinisha maamuzi yoyote au sera ambayo inaweza kuwaathiri.[246] Chini ya Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Wakulima, serikali inapaswa “kuchochea ushiriki, wa moja kwa moja na/au kupitia taasisi zao za uwakilishi, wa wakulima na watu wengine wanaofanya kazi vijijini katika mchakato wa kufanya maamuzi ambayo yanaweza kuathiri maisha yao, ardhi na mueneno wa maisha.”[247] Tume ya Afrika pia inatambua umuhimu wa serikali kutafuta ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa kutoka kwa watu wa Asili.[248]

Wanawake na wasichana pia wana haki ya ushiriki kamili na wa usawa katika kufanya maamuzi na kushauriana.[249] Mkataba wa Kutokomea Aina zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake (CEDAW) unazitaka serikali “kuchukua hatua zote stahiki: (a) Kurekebisha mifumo ya kijamii na kitamaduni ya mwenendo wa wanaume na wanawake, kwa lengo la kukomesha ubaguzi na mila na desturi zinazoegemea kwenye dhana ya uduni na ubora wa jinsia mojawapo au juu ya mgawanyo wa majukumu ya wanaume na wanawake.”[250] Mkataba huo pia unazitaka serikali “kuchukua hatua zote stahiki kuondoa ubaguzi dhidi ya wanawake vijijini. … na kuhakikisha haki za wanawake hao kutendewa saw ana wanaume katika masuala ya ardhi na mageuzi ya kilimo.”[251] 

Kwa kuzingatia masuala ya ardhi, Azimio la Rio kuhusu Mazingira na Maendeleo linatangaza kwamba watu wanapaswa kupata “fursa ya kushiriki kwenye mchakato wa kufanya maamuzi” na serikali inapaswa “kuwezesha na kuhimiza ufahamu na ushiriki wa umma kwa kuhakikisha taarifa zinapatikana kwa wingi.”[252] Zaidi ya hayo, Mkataba wa Afrika uliorekebishwa kuhusu Uhifadhi wa Mazingira na Maliasili, ambao Tanzania haijauridhia, unazitaka nchi wanachama kupitisha sheria na hatua nyingine muhimu za udhibiti kuwezesha umma kupata taarifa za mazingira, kushiriki katika kufanya maamuzi, na kutafuta suluhu kupitia mahakama kwa masuala yahusuyo mazingira.[253]

Haki ya kushiriki katika kufanya maamuzi ni ulinzi muhimu na mazingira ambayo kuondolewa kunaonekana kuwa kwa halali. Kamati ya UN kuhusu Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni inaeleza hatua muhimu za ulinzi ambazo serikali inapaswa kuwapatia watu na jamii wanaotakiwa kuhama bila hiyari yao, ikiwa ni pamoja na fursa ya kushauriana kwa dhati na wale wanaoathirika.[254]  

Haki ya Kupata Taarifa

Katiba ya Tanzania inahakikisha haki ya kupata taarifa, pamoja na haki ya kutafuta, kupokea na kusambaza taarifa.[255]

ICCPR inatoa haki kwa kila mmoja kupata taarifa zilizo katika taasisi za umma.[256] Kamati ya UN kuhusu Haki za Binadamu, amabyo inatafsiri ICCPR, inazielekeza serikali “kutoa kwa ukamilifu taarifa za serikali zenye maslahi ya umma kwa umma,” kuhakikisha upatikanaje wake ni rahisi, wa haraka, wenye ufanisi na wa kimatendo.[257] Mkataba wa Afrika pia unahakikisha haki ya kupata taarifa.[258]

Kuhusiana na habari za mazingira, Azimio la Rio la Mazingira na Maendeleo, ambalo nchi ikiwemo Tanzania imelipitisha katika Mkutano wa UN kuhusu Mazingira na Maendeleo mwaka 1992, inaeleza kwamba “kila mtu anapaswa kupata taarifa zilizo katika mamlaka za umma kuhusu mazingira,” hii ni pamoja na shughuli zinazofanyika katika jamii zao.[259]

Haki ya Uhuru wa Kujieleza na Kukusanyika

Katiba ya Tanzania inahakikisha haki ya uhuru wa kujieleza na uhuru wa kukusanyika kwa amani.[260]

Sheria za kimataifa na kikanda zinaitaka Tanzania kuhakikisha haki ya kutoa maoni bila ya kuingiliwa na kukusanyika kwa amani.[261] Mkataba wa Afrika unahakikisha haki ya kujieleza na kusambaza maoni kwa kuzingatia matakwa ya sheria na haki ya kukusanyika kwa uhuru ndani ya mipaka ya “mipaka muhimu iliyowekwa na sheria hususan ile iliyowekwa kwa maslahi ya usalama wa Taifa, usalama, afya, maadili na haki na uhuru wa wengine.”[262]

Vile vile ICCPR inaruhusu vizuizi vya uhuru wa kujieleza na kukusanyika vinavyotolewa na sheria, ambavyo ni muhimu katika kufikia lengo halali, ikiwa ni pamoja na ulinzi wa usalama wa taifa, utulivu wa umma au afya ya umma na maadili na zisizobagua.[263]

Haki ya Kupata Elimu

Tanzania ni mwanachama wa Mkataba wa Haki za Mtoto (CRC) na Mkataba wa Afrika wa haki na Ustawi wa Mtoto, ambao, kama iivyo kwa ICESCR, unazitaka serikali kuheshimu, kulinda na kutimiza haki ya kupata elimu,[264] bila ya kubagua, ikiwa ni pamoja na kutokana na rangi, kabila, jinsia, lugha, asili ya utaifa au kijamii, kuzaliwa, ulemavu, au “hadhi nyingine.”[265] Kamati ya UN ya Haki za Mtoto inaeleza kuwa “Watoto wa jamii za asili ni miongoni mwa watoto ambao wanahitaji hatua chanya ili kuondoa masharti ambayo yanasababisha ubaguzi na kuhakikisha wanafurahia haki ya Mkataba kwa usawa na watoto wengine.”[266]

Serikali zinawajibu wa kutoa “upeo wa rasilimali zilizopo, kipekee au kupitia msaada na ushirikiano wa kimataifa” ili kutambua haki hii hatua kwa hatua.[267] Kuna dhana kali dhidi ya kuruhusu hatua yoyote ya kurudi nyuma kuhusu haki ya kupata elimu, pamoja na haki nyingine zilizoelezwa kwenye ICESCR.[268] Kamati ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni inaeleza kuwa inapotokea hatua zozote za makusudi za kurudi nyuma zinapotekelezwa, serikali lazima ioneshe kuwa vitendo hivyo vilifanyika baada ya kuangazia njia zote mbadala na ndani ya misingi ya kutumia upeo wa rasilimali zilizopo za za serikali.[269] Kamati ya Haki za Mtoto imeeleza kuwa “ili mtoto wa jamii ya asili afurahie haki yake ya kupata elimu kulingana na Watoto wengine… Nchi wanachama zinapaswa kutenga fedha, nyenzo na rasilimali watu zinazohitajika ili kutekeleza sera na mipango mahususi inayolenga kuboresha upatikanaji wa elimu kwa watoto wa jamii ya asili.”[270]

Serikali pia zinawajibika kuhakikisha upatikanaji wa haki ya kupata maji na mazingira masafi katika muktadha wa shule kwa kadri ya rasilimali zilizopo.[271] Haki ya  usafi wa mazingira na haki ya elimu vinahusiana na bila ya kupata mazingira masafi shule, watoto wataendelea kukosa fursa adhimu ya kwenda shule na kujifunza. Mkataba wa CEDAW, ambao Tanzania ni mwanachama, unatafsiri na kutumia haki ya kupata elimu na kuweka mkazo kwa mahitaji ya kipekee na mazingira ya wanawake na wasichana.[272]

Haki ya Kupata Huduma Bora ya Afya

ICESCR inatambua “haki ya kila mmoja kufurahia kupata huduma bora ya kiwango cha juu kabisa ya afya ya mwili na akili.”[273] Inazitaka serikali kuchukua hatua madhubuti, za makusudi, na zinazolenga kufikia upatikanaji wa haki ya kupata huduma za afya, na inakataza hatua za kurudi nyuma katika hili “isipokuwa Serikali inaweza kuonyesha kuwa imefanya kila juhudu kutumia rasilimali zake zote kutimiza wajibu wake.”[274] Huduma zinahusiana na afya, bidhaa na vifaa lazima ziwepo, zipatikane, zikubalike na ziwe ni za kiwango cha juu.[275] Upatikanaji unaofikika unamaanisha “ufikiaji salama kwa watu aina zote ikiwa ni pamoja na watoto, watu wazima, wazee, watu wenye ulemavu, na makundi mengine hatarishi,” pamoja upatikanaji wa fedha.[276]

CEDAW na Mkataba wa Afrika[277] inaangazia haki ya kupata huduma za afya kwa makundi maalumu kama vile wanawake na wasichana[278] na watoto.[279] CEDAW inaeleza kuwa serikali zinapaswa kuhakikisha wanawake wanapata huduma stahiki zinazohusiana na ujauzito, uangalizi, kipindi baada ya kujifungua, kutoa huduma za bure pale inapobidi pamoja na lishe ya kutosha kipindi cha ujauzito na kunyonyesha.[280]

Kwa mujibu wa Kamati ya UN ya Haki za Mtoto, “Nchi zinapaswa kuchukua hatua zote muhimu kuhakikisha kuwa Watoto kutoka jamii ya watu wa asili, familia na jamii yao wanapata taarifa na elimu kuhusu masuala ya afya na huduma za kujikinga kama vile lishe, kunyonyesha, huduma kipindi cha ujauzito na baada ya kujifungua, afya ya Watoto na vijana, chanjo, magonjwa yanayoambukiza (hususan VVU/UKIMWI na kifua kikuu), usafi, usafi wa mazingira na hatari ya wadudu na magugu.”[281]

Mbinu za Uhifadhi zinazozingatia Haki

Mnamo Agosti 2021, mwandishi maalumu wa UN kuhusu haki za mazingira na binadamu alitoa mapendekezo ya kuoanisha juhudi za kulinda mazingira na wajibu wa nchi kwa haki za binadamu.[282] Mwandishi maalumu alizitaka nchi kutoa kipaumbele kwa watu wa Asili, jamii za ndani, wakulima, wanawake wa vijijini na vijana, sambamba na uelewa wao wa asili na utaratibu wa usimamizi endelevu wa mazingira, katika kutambua, kutenga na kusimamia maeneo muhimu kiutamaduni na kibaiolojia.

Mwandishi maalumu pia alitoa mapendekezo ya kufanya marekebisho ya sheria za uhifadhi na maeneo yanayolindwa ili kulinda haki za watu wa Asili na watu wengine wenye haki vijijini wanaotegemea maeneo ya hifadhi.[283] Vile vile, Mkataba wa Afrika uliofanyiwa marekebsiho unaohusu Uhifadhi wa Mazingira na Rasilimali unazitaka serikali “kuchukua hatua za kisheria na nyinginezo kuhakikisha haki za kimila na haki miliki za jamii za ndani ikiwa ni pamoja na haki za wakulima zinaheshimiwa kwa mujibu wa maelezo ya Mkataba huu.”[284]

Katika ripoti ya 2022, mwandishi maalumu wa UN wa haki za watu wa Asili alisisitiza umuhimu wa juhudi za pamoja za uhifadhi ambazo zinatambua haki za watu wa Asili na kulinda mtindo wao wa maisha na ufahamu wao, pamoja na ardhi yao.[285]

Haki ya Kufidiwa

Sheria za Tanzania zinaeleza juu ya kulipwa fidia kwa upotevu wa ardhi au mali. Katiba na Sheria ya Vijiji inaharamisha unyang’anyi wa mali, ikiwa ni pamoja na “kwa madhumuni ya kutaifisha,” bila ya fidia ya haki na ya kutosha.[286] Shetia ya Utwaaji Ardhi, ambayo inatoa muongozo wa mchakato wa fidia, inawapa watu haki ya kulipwa fidia hata kama Rais ametwaa ardhi yao kwa matumizi ya umma.[287] Zaidi ya hayo, chini ya Sheria ya Vijiji, ardhi ya Kijiji haipaswi kuhamishwa umiliki mpaka aina, kiasi, njia na muda wa kulipa fidia utakapokubalika kati ya baraza la Kijiji na Mkuu wa Wilaya.[288]

Mwandihi maalumu wa UN kuhusu haki za mazingira na za binadamu amesisitiza kifungu cha UNDRIP[289] kinachoelekeza nchi “kutoa fidia ya haki, inayokubalika kiutamaduni na inayolingana” pale ambapo urejeshaji hauwezekani. Kwa mujibu wa mwandishi maalumu:

Isipokuwa inapokubalika kwa uhuru na watu wa Asili au watu wa kijijini wenye haki wanaohusika, fidia inapaswa kuwa katika hali ya ardhi, maeneo na rasilimali sawa kwa ubora, ukubwa na hadhi ya kisheria au fidia ya fedha au njia nyingine zinazofaa.[290]

Haki ya Utatuzi

Chini ya ICCPR, Tanzania ina wajibu wa kusimamia haki ya kupata suluhisho madhubuti kwa waathirika wa ukiukwaji wa haki za binadamu.[291] Waathirika wana haki ya kushughulikiwa malalamiko yao na mahakama yenye uwezo, mamlaka za utawala au za kisheria au mamlaka yoyote yenye uwezo, ambayo inaweza kusimamia suluhu kama hizo.[292]

Mwaka 2019, Tanzania iliondoa tamko lake lililotolewa chini ya kifungu cha 34 cha Itifaki ya Mkataba wa Afrika ya Kuanzishwa kwa Mahakama ya Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu kukubali uwezo wa mahakama.[293] Kujiondoa kwa serikali kunazuia watu binafsi na NGOs kufungua kesi moja kwa moja dhidi ya serikali mbele ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu iliyoko Arusha.[294] Huku mamlaka zikitishia kuwakamata wanajamii wa NCA na wakazi wa Msomera, wale walioathirika wanakabiliana na changamoto kubwa kupata suluhisho nchini Tanzania.

Mapendekezo

Kwa Serikali ya Tanzania

  • Kupitisha Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori iliyofanyiwa marekebisho ili kuakisi historia ya Tanzania ya maeneo yaliyo hifadhiwa yenye matumizi mtambuka ya ardhi na kuhakikisha ya kwamba vifungu vinaheshimu haki za watu kwenye ardhi, mali, maisha na utamaduni.

Juu ya Ulinzi wa Umiliki wa Ardhi

  • Kuheshimu haki za binadamu ikiwa ni pamoja na haki za ardhi na umiliki, na ardhi inayomilikiwa kimila na jumuiya ya watu wa Asili na wengine wenye haki katika kuendeleza na kutekeleza hatua zote za uhifadhi.
    • Kutambua kisheria ardhi na rasilimali ambazo jamii za wafugaji wilayani Ngorongoro wamezitumia na kuzisimamia kwa vizazi na vizazi, kwa kuheshimu mifumo yao ya sheria, mila na desturi zao ikiwa ni pamoja na njia na taratibu za asili kuchunga na matambiko.

Juu ya Ridhaa Huru, ya Awali na inayotokana na kuwa na Taarifa na Kushiriki

  • Kushauriana vya kutosha na kutafuta ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa kutoka kwa jamii wenyeji iliyoathirika katika eneo la NCA na kushauriana ipasavyo na wakazi waliopo Msomera walioathiriwa na makazi mapya kulingana na wajibu wa kitaifa na kimataifa.
    • Kuzipatia jamii zote zilizoathirika taarifa muhimu kuhusu mikakati yote iliyopendekezwa ya uhifadhi na maendeleo ambayo yataathiri maisha yao kama watu binafsi na kama jamii.
    • Kuhakikisha ushiriki wa jamii yote inayoathirika katika kufanya maamuzi kuhusiana na ardhi na maliasili, ikiwa ni pamoja na kupitia michakato inayozingatia ushirikishwaji wa jinsia na vijana katika kuamua mikakati ya uhifadhi inayoheshimu na kulinda haki zao.

Juu ya Elimu na Afya

  • Kulinda haki za Wamasai kupata elimu, kiwango cha juu cha afya kinachoweza kufikiwa, maji na usafi wa mazingira, makazi ya kutosha, chakula na kushiriki katika maisha ya kiutamaduni katika eneo la NCA.
  • Kurejesha nafasi za kazi kwa wafanyakazi wa afya wanaolipwa na serikali katika vituo vya afya, pamoja na hospitali ya Endulen na zahanati zingine katika eneo la NCA.

Juu ya Askari Wanyamapori wa NCAA

  • Kuhitaji na kuhakikisha kwamba askari wanyamapori wanapata mafunzo ipasavyo kuhusu sheria na viwango vya haki za binadamu kitaifa na kimataifa na kuwa chini ya uangalizi huru na uwajibikaji.
  • Kuwawajibisha askari wanyamapori ikiwa pamoja na maafisa wakuu, waliojihusisha na utovu wa nidhamu kupitia njia stahiki za kinidhamu na mahakama.

Juu ya Ufuatiliaji na Utaratibu wa Malalamiko

  • Kufanya ufuatiliaji unaoendelea na kusitisha utekelezaji wa mikakati ya uhifadhi ambayo inakiuka haki kama vile maeneo ya hifadhi au uhamishaji wa lazima unaohusiana na uhifadhi na uhamishaji bila hiari.
  • Kuweka utaratibu mbadala wa kujitegemea wa malalamiko na utatuzi ambao unaweza kupokea malalamiko na kutoa masuluhisho ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaohusiana na kuhamishwa kwa wakazi kutoka NCA na makazi mapya Msomera.

Juu ya Kuzuia Kuondoshwa kwa Lazima

  • Kuhakikisha kwamba mfumo wa ndani wa kisheria wa Tanzania unaosimamia utwaaji wa ardhi ya umma unawiana na viwango vya sheria na kanuni za kimataifa vya haki za binadamu. Hii ina maana kukataza uhamishaji wa lazima, bila kujali umiliki au hali ya umiliki wa wale walioathirika, na kuhakikisha kwamba utaratibu wa utwaaji ardhi ya umma unahusisha:
    • Kuheshimu utu wa binadamu na kanuni za jumla zinazozingatia busara, uwiano na mchakato unaostahili;
    • Kutafuta njia mbadala za kuhamisha watu kwa kushauriana na watu wanaoathiriwa kabla ya kutekeleza zoezi la kuhamisha; kwa kuzingatia athari kwa watu wanaohamishwa kutokana na sababu zikiwemo jinsia, kabila, tabaka, umri, dini na ulemavu, miongoni mwa mengine;
    • Kushiriki katika mashauriano ya dhati na wale wanaoathirika;
    • Kutoa notisi ya kutosha na ya kuridhisha kwa watu wote wanaoathirika kabla ya tarehe iliyopangwa ya kuwahamisha;
    • Kutoa suluhu za kutosha na zinazofaa za kisheria au nyingine zinazofaa zipatikane kwa mtu yeyote anayedai kuwa haki yake ya kulindwa dhidi ya kuhamishwa kwa lazima imekiukwa au iko kwenye tishio la kukiukwa;
    • Kutoa njia za kupata haki katika mchakato mzima na sio tu wakati kuhamishwa kunakaribia;
    • Kutoa upatikanaji wa msaada wa kisheria kwa watu wanaohitaji kutafuta suluhu la kisheria;
    • Kutoa fidia ya kutosha kwa upotevu wowote wa mali; na
    • Kuhakikisha kwamba kuhamishwa hakupelekei kusababisha watu kuachwa bila makazi au kuwa katika hatari ya kukiuka haki nyingine za binadamu.

Kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro

  • Kurejesha ufadhili wa huduma na utunzaji wa miundombinu iliyopo NCA, ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Endulen na shule, kuanzisha upya na kuimarisha Baraza la Wafugaji la Ngorongoro, na kuhakikisha hakuna vikwazo kwa Baraza la Wafugaji kutekeleza majukumu yake.
  • Kuhakikisha vyuo vikuu vinaarifiwa kuhusu wanafunzi wanaopata ufadhili wa masomo, na kuhakikisha kuwa fedha zinazohusiana na vyuo vikuu zinatolewa mara moja.
  • Kushauriana na wawakilishi wa jamii ikiwa ni pamoja na Baraza la Wafugaji kuanzisha miongozo ya wazi kuhusu vibali vya ujenzi na vifaa vya ujenzi vinavyoruhusiwa, kwa mfano vile vinavyopatikana katika mazingira yale yale, ambavyo vyanzo vyake ni endelevu na vina umuhimu kiutamaduni kwa jamii.

  • Kubuni mfumo ulio wazi, kwa kushirikisha wawakilishi wa jamii ya NCA, ambao utaondoa au kupunguza mzigo wa kulipa ada ya kuingia kwa wakazi wa NCA ambao hawana vitambulisho vinavyowaruhusu kuingia getini na kutoa njia nyepesi ya kuingia kwa wanajamii hawa wa asili.

  • Kuanzisha mikakati ya uhifadhi inayoheshimu haki na viwango na utaratibu wa utekelezaji ulio wazi unaoshirikisha wanajamii wa NCA katika mchakato.

    • Kushirikiana na jamii ya NCA kuandaa mpango wa vyanzo endelevu vya chakula na maji ambavyo vinakubalika kitamaduni, vitakavyowasaidia kimaisha na kuhakikisha wana usalama wa chakula.

  • Kutekeleza mpango wa muda mrefu wa ufuatiliaji na tathmini unaoongozwa na wanajamii kwa kuelewa kwamba mipango ya kuhamisha watu inahitaji usaidizi na usimamizi wa muda mrefu.

  • Kuongeza muda wa kutoa misaada kwa familia ambazo zimehamishwa kutoka NCA.
  • Kuwaruhusu wakazi kurudi NCA, ikiwa watajisikia kufanya hivyo na kuwawezesha kurudi ikiwa ni pamoja na kuwapa msaada wa kifedha kujenga nyumba zao na kununua mifugo.

  • Kufanya uchunguzi kuhusu udhalilishaji unaofanywa na askari wanyamapori wa NCAA katika eneo la NCA, ikiwa ni pamoja na vikwazo vya kutembea na kuwawajibisha.

Kwa Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu

  • Kwa kuzingatia mamlaka yake chini ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu:
    • Kuunda na kuweka kanuni zinazolenga kutatua ukiukwaji wa haki za binadamu zilizoandikwa katika ripoti hii ambapo serikali ya Tanzania inaweza kutumia kama msingi wa sheria na sera zao.
    • Kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ili kuamua haki za Wamasai na jamii nyingine zilizoathiriwa na mradi wa NCA na wajibu wa serikali ya Tanzania.
  • Kuendelea kutoa mapendekezo mahususi ya kuheshimu haki kwa serikali ya Tanzania ili kusitisha uhamishaji wa lazima wa watu na uhamishaji wa jamii za Wamasai bila hiari yao, kushauriana na jamii zilizoathirika, na kuhakikisha kuwa serikali inaheshimu haki za jamii ziliyoathirika za ardhi, ustawi wa maisha yao na utamaduni, dini na maendeleo.

Kwa Washirika wa Kimataifa wa Tanzania, ikijumuisha Mashirika ya Uhifadhi, Mashirika ya Maendeleo ya nchi mbalimbali

  • Kuwataka viongozi wa Tanzania kukomesha sera za unyanyasaji katika wilaya ya Ngorongoro na kuhifadhi haki za kijamii za Wamasai, kupata elimu na afya miongoni mwa mambo mengine kama msingi wa ustawi wa uchumi wa pamoja.
  • Kusaidia serikali ya Tanzania katika kufanya uangalizi wa haki za binadamu kuhusu hatari zinazoweza kutokea zinazohusiana na mipango mikakati yake ya utalii na uhifadhi, hasa kuhusiana na maeneo yaliyohifadhiwa, kuhamishwa kwa lazima na makazi mapya.
  • Kujiondoa katika shughuli zozote za uhifadhi ambazo hazikidhi sheria na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu.
  • Kutoa rasilimali kwa serikali ya Tanzania ili kuendeleza na kutelekeza sera mahususi zinazozingatia jinsia na vijana kuhusu uhifadhi zinazoheshimu haki za jamii za Wamasai katika eneo la NCA na wenye haki vijijini huko msomera.
  • Kusaidia serikali katika kuandaa na kutekeleza sera mahususi za kuajiri, kutoa mafunzo na kusaidia askari wanyamapori na wengine wenye jukumu la kulinda maeneo yaliyo hifadhiwa au maeneo mengine yaliyotengwa kwa ajili ya uhifadhi.
  • Kuweka masharti ya ufadhili kwa askari wanyamapori kuzingatia kutekeleza programu za mafunzo kuhusu sheria na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu na operesheni zao kuzingatia viwango hivi.

Kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)

  • Kurekebisha miongozo ya utendaji ambayo Mkataba wa Urithi wa Dunia unatekelezwa ili kuoanisha Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Watu wa Asili na kupitisha taratibu za kuhakikisha kuwa watu wa Asili wanatoa ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa taarifa.
  • Kukuza na kuhimiza NCAA na serikali ya Tanzania kukuza nafasi ya jamii za Wamasai katika eneo la NCA katika usimamizi wa eneo la Urithi wa Dunia kwa mujibu wa sheria na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na Mkataba uliopo wa Urithi wa Dunia na malengo yake ya kimkakati hususani “C ya tano” ya Jamii.


 

Shurkani

Ripoti hii ilifanyiwa utafiti na kuandikwa kwa pamoja na Juliana Nnoko-Mewanu, mtafiti mkuu wa wanawake na ardhi katika Idara yaa Haki za Wanawake, na Oryem Nyeko mtafiti mkuu wa Tanzania na Uganda katika Idara ya Afrika. Bernice Mutinda, mwanafunzi wa ndani wa zamani katika Idara ya Afrika alitoa usaidizi wa utafiti wa kisheria.

Ashwanee Budoo-Scholtz, naibu mkurugenzi Idara ya Afrika, na Regina Tames, naibu mkurugenzi Idara ya Haki za Wanawake walihariri ripoti hii. Babatunde Olugboji, naibu mkurugenzi wa programu alifanya mapitio ya programu. James Ross, mkurugenzi wa sheria na sera na Clive Baldwin mshauri mkuu wa sheria, walifanya mapitio ya sheria. Luciana Téllez Chávez, mtafiti mkuu wa Programu ya Mazingira na Haki za Binadamu; Elin Martinez, mtafiti mkuu katika Idara ya Haki za Watoto na Jim Wormington, mtafiti mkuu na wakili na Matt McConnell mtafiti, (Matt alipitia ripoti kwa upande wa Programu ya Afya na Haki za Binadamu na Idara ya Haki za Kiuchumi na Haki), katika Idara ya Haki na Haki za Kiuchumi walitoa maoni ya kitaalamu. Susanné Bergsten, afisa katika Idara ya Haki za Wanawake na Amu Mnisi, mshirika katika Idara Ya Afrika walitoa usaidizi wa uzalishaji na Travis Carr, afisa uchapishaji alitayarisha ripoti kwa ajili ya kuchapisha.

Muhimu zaidi tunapenda kuwashukuru wote waliozungumza nasi wakati wa utafiti huu, na hasa wana jamii wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na wakazi wa Msomera.


 

[1] Ofisi ya Makamu wa Rais, “Wasifu: Mhe. Samia Suluhu Hassan,” undated, https://www.vpo.go.tz/vpos/vice-president-3 (imepitiwa Julai 2, 2024).

[2] Human Rights Watch, “Ukimya Wangu, Usalama Wangu”: Vitisho kwa Vyombo vya Habari na Asasi za Kiraia Tanzania, Oktoba 2019, https://www.hrw.org/report/2019/10/28/long-i-am-quiet-i-am-safe/threats-independent-media-and-civil-society-tanzania.   

[3] “Tanzania: Rais Hasn aondoa marufuku ya mikutano ya kisiasa,” Amnesty International, Taarifa kwa Umma, Januari 3, 2023, https://www.amnesty.org/en/latest/news/2023/01/tanzania-president-hassan-lifts-the-blanket-ban-on-political-assemblies/ (imepitiwa Julai 2, 2024); “Rais Hasan wa Tanzania amaliza marufuku ya mikutano ya kisiasa iliyodumu miaka 6”, Aljazeera, Januari 3, 2023, https://www.aljazeera.com/news/2023/1/3/tanzania-president-hassan-lifts-ban-on-opposition-rallies (imepitiwa Julai 2, 2024).

[4] “Tanzania: Wakosoaji wa Mkataba wa Bandari Wakamatwa”, taarifa iliyotolewa na Human Rights Watch, Agosti 7, 2023, https://www.hrw.org/news/2023/08/07/tanzania-critics-port-deal-arrested#:~:text=(Nairobi)%20%E2%80%93%20Tanzania%20authorities%20have,Human%20Rights%20Watch%20said%20today   

[5] Wakati wa janga la UVIKO-19, kama ilivyukuwa kwa nchi nyingine, utalii nchini Tanzania ulisimama na sekta za uzalishaji, kilimo na nyinginezo zilidorora. Kutokana na hatua za watu kufungiwa na uchumi kudorora, Tanzania ilikabiliana na usumbufu wa kuvurugika kwa mnyororo wa usambazaji ikiwa ni pamoja na biashara zinazovuka mipaka za bidhaa za chakula kama vile mahindi na mchele na kupungua kwa nguvu ya manunuzi katika kaya. See World Bank Group, “Taarifa ya Uchumi wa Tanzania: kushughulikia madhara ya Uviko-19,” Juni 7, 2020, https://documents.worldbank.org/en/publication/documents-reports/documentdetail/850721591546081246/tanzania-economic-update-addressing-the-impact-of-covid-19 (imepitiwa Julai 2, 2024).

[6] Peter Greenberg, “Tanzania: The Royal Tour,” Public Broadcasting Service, April 18, 2022,  https://pbsinternational.org/programs/tanzania-the-royal-tour/ (imepitiwa Julai 2, 2024); Emily Burack, “PBS’s The Royal Tour Returns with First Episode Filmed Since COVID-19 Pandemic Began,” Town & Country, May 20, 2022, https://www.townandcountrymag.com/leisure/arts-and-culture/a40061566/pbs-the-royal-tour-tanzania/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[7] Apolinari Tairo, “Royal Tour documentary showcases Tanzania’s tourism gems,” The East African, May 14, 2022, https://www.theeastafrican.co.ke/tea/magazine/royal-tour-documentary-showcases-tanzania-tourism-gems-3811836 (imepitiwa Julai 2, 2024).

[8] Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (ACHPR), Kituo cha Maendeleo ya Haki za Wachache (Kenya) na Kundi la Haki za Wachache (kwa niaba ya Baraza la Ustawi wa Endorois) v. Kenya, 276/03, Hukumu, https://www.escr-net.org/sites/default/files/Endorois_Decision.pdf (imepitiwa July 2, 2024), para. 150.

[9] Ibid., para. 154.

[10] ACHPR, “Watu wa Asili Afrika: Watu Waliosahaulika?,” 2006, https://achpr.au.int/index.php/en/special-mechanisms-reports/indigenous-peoples-africa-forgotten-peoples (imepitiwa Julai 2, 2024). ACHPR inawatambua Wamasai wa Tanzania kama watu wa Asili. Tazama: pp. 10, 14, na 16.

[11] Tamko la Dkt. Mario Mejia Montalvo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Kudumu la UN kuhusu “Masuala ya watu wa asili kwa kutolea mfano kuondoshwa kwa lazima kwa Wamasai kutoka Eneo la Hifadhi ya nchini Tanzania,” taarifa kwa vyombo vya Habari kutoka Umoja wa Mataifa, Juni 14, 2022, https://www.un.org/development/desa/indigenouspeoples/wp-content/uploads/sites/19/2022/06/Statement_Loliondo_letterhead.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024). Pia tazama, Thomas M. Lekan, “Our Gigantic Zoo: A German Quest to Save the Serengeti,” in Serengeti II: Dynamics, Management, and Conservation of an Ecosystem, eds. A.R.E. Sinclair and Peter Arcese. (Chicago: The University of Chicago Press, 1995). Makundi mengine ya kikabila katika eneo la Ngorongoro ni pamoja na Datooga, Hadza au Hadzabe, na Iraqw. Wamasai wana idadi kubwa ya watu (takribani asilimia 98) katika eneo hilo. Tazama Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Utamaduni: Muhtasari,” haina tarehe, https://www.ncaa.go.tz/cultures/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[12] Melubo, K., “Why are wildlife on the Maasai doorsteps? Insights from the Maasai of Tanzania.” AlterNative: An International Journal of Indigenous Peoples, 16(3) (2020): 180-192, imepitiwa Julai 2, 2024, doi: 10.1177/1177180120947823.

[13] Robin S. Reid, Savanna of Our Birth: People, Wildlife, and Change in East Africa, (Berkeley: University of California Press, 2012).

[14] “Historia ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti,” Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, imepitiwa Julai 2, 2024, https://www.serengetiparktanzania.com/information/serengeti-national-park-history/.

[15] Hii inahusiana kwa karibu na historia ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ugawaji wa hifadhi hiyo, na kuhamishwa kwa mipaka yake upande wa kaskazini na mashariki. Mwaka 1957, mamlaka ya kikoloni ya Uingereza ilitenga eneo la Bonde la Ngorongoro na Uwanda wa Mashariki wa Serengeti na kuanzisha eneo la matumizi “mtambuka” kwa ajili ya Wamasai, mifugo yao na wanyamapori. Tazama Lekan, “Our Gigantic Zoo.”  

[16] Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ya mwaka 1959. Tazama, Michael Grzimek na Bernard Grzimek, “A Study of the Game of the Serengeti Plains,” Zeitschrift fur Saugetierkunde, vol. 25, (1960), p. 13 Makundi mengine ya kikabila katika eneo la Ngorongoro ni pamoja na Datooga na Hadza au Hadzabe. Tazama “Utamaduni: Muhtasari,” Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro, imepitiwa Julai 2, 2024, https://www.ncaa.go.tz/cultures/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[17] “Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro”, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Kituo cha Urithi wa Dunia, https://whc.unesco.org/en/list/39/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[18] Anthony Sinclair et al., “Shaping the Serengeti ecosystem,” in Serengeti IV: Sustaining Biodiversity in a Coupled Human-Natural System, eds. Anthony Sinclair et al. (University of Chicago Press, Chicago, 2015).

[19]  Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Na. 14 of 1959, kipengele cha 5(1).

[20] Ibid., section 7(1).

[21] Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro ya mwaka 1959.

[22] Kata za tarafa ya Ngorongoro ni Alailelai, Alaitolei, Endulen, Evasi, Kakesio, Misigiyo, Nainokanoka, Naiyobi, Ngoite, Ngorongoro, na Olbalbal. Nchini Tanzania “kata” ni eneo la utawala kati ya Kijiji na Wilaya, ambalo hupitia mapendekezo ya miradi ya halmashauri ya Kijiji na kuidhinisha kupelekwa kwa Kamati ya Maendeleo ya Wilaya. Jaba Shadrack, “Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini Tanzania,” 2010, https://jabashadrack.blogspot.com/2010/05/local-government-authorities-in.html (imepitiwa Julai 2, 2024). Baadhi ya vijiji havijasajiliwa kwa sababu usajili nchi nzima umesuasua kutokana na gharama, na utaratibu wa serikali wa kuendelea kuwahamisha wakazi inaweza kuwa imesitisha mchakato wa usajili kuendelea.

[23] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi (MLUM) ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Mafunzo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii, 2019, p. xvi. Tazama pia Sheria ya Vijiji, Cap 114, iliyoanza 1 Mei 2001.

[24] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Administrative Units Population Distribution Report: Tanzania,” December 2022, https://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/Census2022/Administrative_units_Population_Distribution_Report_Tanzania_volume1a.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024).

[25] Thompson, D. M., ed., Multiple Land-Use: The Experience of the Ngorongoro Conservation Area, Tanzania, (Gland: IUCN, 1997). A multiple land use category of protected area that allowed wildlife conservation along with pastoralism and tourism.

[26] UNESCO, “Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Mpango Mkuu wa Usimamizi 1996,” Oktoba 26, 1979, https://whc.unesco.org/uploads/nominations/39bis.pdf (accessed July 2, 2024), pp. 15 – 149.

[27] Mkataba unaohusu Ulinzi wa Urithi wa Kitamaduni na wa Asili wa Dunia (Mkataba wa Urithi wa Dunia) ulipitishwa Novemba 16, 1972, na Mkutano Mkuu katika kikao chake cha kumi na saba, ukaanza kutumika Disemba 17, 1975.

[28] “Kuhusu Urithi wa Dunia: Bodi za Ushauri,” UNESCO, Mkataba wa Urithi wa Dunia, imepitiwa Julai 2, 2024, https://whc.unesco.org/en/advisorybodies/.

[29] UNESCO, Ripoti ya Kituo cha Pamoja na Urithi wa Dunia /ICOMOS/IUCN Ujumbe kwenda Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Machi 4-8, 2019, https://whc.unesco.org/document/174817 (imepitiwa Julai 3, 2024). P. 21, para. 3.2.5.

[30] “Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro” UNESCO, Mkataba wa Urithi wa Dunia, imepitiwa Julai 2, 2024.  

[31] UNESCO, Ripoti ya Kituo cha Pamoja na Urithi wa Dunia /ICOMOS/IUCN Ujumbe kwenda Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Jamhuri ya Muungano waTanzania, Machi 2019, https://whc.unesco.org/document/174817 (imepitiwa Machi 29, 2024).

[32] UNESCO, “Ripoti ya Kituo cha Pamoja na Urithi wa Dunia /ICOMOS/IUCN Ujumbe kwenda Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Jamhuri ya Muungano waTanzania, Machi 2019,” June 13, 2019, https://whc.unesco.org/document/174817 (imepitiwa Julai 2, 2024). pp. 33-34, para. 4.2.6.1.

[33] Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (Kuanzishwa kwa Baraza la Wafugaji Ngorongoro) Rules, 2000 (G.N. No. 234 of 2000); United States Agency for International Development (USAID) Tanzania, “The Case of Ngorongoro Conservation Area,” 2000, https://pdf.usaid.gov/pdf_docs/Pnack611.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024).

[34] Kanuni za Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, kifungu 8(1).

[35] Kanuni za Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, kifungu 8(2).

[36] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Note Verbale, Ref. No: NC291/738/02/182.

[37] Kulingana na tovuti ya NCAA, NCAA ilianzisha Programu ya Ufadhili wa Wanafunzi mwaka 1994 na kuendelea kufadhili program. Hata hivyo, program hiyo kwa sasa inasimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro. “Maendeleo ya Jamii: Programu na Huduma - Elimu” NCAA, https://www.ncaa.go.tz/community-development/ (imepitiwa Julai 2, 2024); tazama pia: Ngorongoro Community Report, “The Truth, Falsity, and Mismanagement,” 2022, https://pingosforum.or.tz/wp-content/uploads/2022/05/Ngorongoro-Community-Report.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024).

[38] Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (Marekebisho), 1975.

[39]  Mwishoni mwa miaka ya 1970, makazi ya kudumu ya Wamasai katika bonde la Ngorongoro yaliondolewa chini ya sera za ujamaa za serikali zilizolenga kuziunganisha kaya zilizosambaa kuwa vijiji. Ujaama Vijijini ni sera ya Ujamaa (1967-1973) iliyoanzishwa na Rais Julius Nyerere kuchochea maendeleo katika maeneo ya vijijini kwa kujipanga na kushawishi watu kuishi kwa kukaribiana, kufanya kazi na kulima kwa kushirikiana. Misingi mikuu ilikuwa: 1. Watu wanapaswa kuishi pamoja; 2. Wanatakiwa kumiliki zana za uzalishaji kwa pamoja; 3. Wanatakiwa kufanya kazi pamoja, ili kuwa Kijiji cha Ujamaa, makazi ya kilimo yalipaswa kuwa na kaya angalau 250, kila nyumba ikizingatia vipimo maalumu. Kila familia, bila kujali ukubwa wake ilipewa ekari 1 au mbili za ardhi. Tazama Gazeti la Serikali Na. 4 la mwaka 1967; Taarifa ya Waraka wa Rais wa mwaka 1969. Mpango huu hapo mwanzo ulikuwa wa hiyari, lakini kuhama kwa lazima kulianza mwaka 1972 na kuwalazimisha watu kwenda kwenye vijiji vya Ujamaa kufikia mwisho wa mwaka 1976. Tazama Jaclynn Ashly, “Tanzania: Remembering Ujaama, the good, the bad, and the buried,” African Arguments, December 17, 2020, https://africanarguments.org/2020/12/tanzania-remembering-ujamaa-the-good-the-bad-and-the-buried/ (imepitiwa Julai 2, 2024). Sera ujamaa hapo awali ilianza na sera ya vijiji iliyoanza mwaka 1974.

[40] Kilimo kilizuiwa tangu mwaka 1975 kwa sababu ya masuala ya uhifadhi, ingawa marufuku hiyo iliondolewa kwa muda toka wakati huo. Kwa sasa, NCAA imeweka sheria kali ambayo imekomesha kilimo ndani ya eneo la NCA.

[41]  Barua ya Umoja wa Mataifa ya Taratibu Maalumu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ref.: AL TZA 3/2021, Februari 2022, https://spcommreports.ohchr.org/TMResultsBase/DownLoadPublicCommunicationFile?gId=26938 (imepitiwa Julai 2, 2024).  

[42] Mahojiano ya Human Rights Watch na Albert Msando, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mji wa Handeni, Aprili 11, 2023.

[43] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi (MLUM) ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Mafunzo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii, 2019, p. 94.

[44]  Kwa mujibu wa Ripoti Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi (MLUM), jamii wenyeji ilipinga kuhamishwa familia za Wamasai kutoka eneo la NCA kwenda katika eneo lao. Kwa mfano, wakazi wa Kijiji cha Oldonyo Sambu, ambacho kiko karibu na eneo la makazi mapya, “walivamia” eneo hilo na “kuwabughudhi” wakazi waliohamia, “ikiwa ni pamoja na kuwanyang’anya ardhi iliyotengwa kwa ajili yao.” Tazama p. xvi – xvii.

[45]   Kwa mujibu wa Ripoti Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi, baadhi ya wakazi waliohama wamekwenda “hadi Wilaya za Handeni na Kilindi katika mkoa wa Tanga.” Tazama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, MLUM ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Masomo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii, 2019, p. xvii.

[46] Ibid.

[47] “Tanzania: Wamasai Wanaondolewa kwa Nguvu kwa ajili ya Pori la Akiba: Toa njia za kushughulikia malalamiko; Chagua Njia Mpya ya Uhifadhi baada ya Mashauriano,” taarifa kutoka Human Rights Watch, Aprili 27, 2023, https://www.hrw.org/news/2023/04/27/tanzania-maasai-forcibly-displaced-game-reservehttps://www.hrw.org/news/2023/04/27/tanzania-maasai-forcibly-displaced-game-reserve; Oryem Nyeko and Juliana Nnoko (Human Rights Watch), “Tanzania’s Eviction of Maasai Pastoralist Continues,” commentary All Africa, February 2, 2023, https://www.hrw.org/news/2023/02/02/tanzanias-eviction-maasai-pastoralists-continues.

[48] Katika Eneo la Hifadhi watu wanaruhusiwa kuingia na kutumia lakini hawaruhusiwi kuua wanyamapori  

[49] “Tanzania: Wamasai Wanaondolewa kwa Nguvu kwa ajili ya Pori la Akiba,” taarifa kutoka Human Rights Watch, Aprili 27, 2023.  

[50] Kwa mujibu wa Ripoti ya MLUM, jamii wenyeji ilipinga kuhamishwa familia za Wamasai kutoka eneo la NCA kwenda katika eneo lao. Kwa mfano, wakazi wa Kijiji cha Oldonyo Sambu, ambacho kiko karibu na eneo la makazi mapya, “walivamia” eneo hilo na “kuwabughudhi” wakazi waliohamia, “ikiwa ni pamoja na kuwanyang’anya ardhi iliyotengwa kwa ajili yao.” Tazama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi (MLUM) ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Mafunzo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii, 2019, p. xvi – xvii.

[51] Kituo cha Urithi wa Dunia cha UNESCO, Ripoti ya Hali ya Uhifadhi Iliyowasilishwa na Nchi Wanachama, Jamhuri ya Muungano wa, 2023, https://whc.unesco.org/document/198961 (imepitiwa Julai 2, 2024) p. 1.

[52] Kwa mujibu wa Ripoti ya MLUM, jamii wenyeji ilipinga kuhamishwa familia za Wamasai kutoka eneo la NCA kwenda katika eneo lao. Kwa mfano, wakazi wa Kijiji cha Oldonyo Sambu, ambacho kiko karibu na eneo la makazi mapya, “walivamia” eneo hilo na “kuwabughudhi” wakazi waliohamia, “ikiwa ni pamoja na kuwanyang’anya ardhi iliyotengwa kwa ajili yao.” Na kwamba baadhi ya wakazi waliohamishwa wameenda mbali hadi kufika wilaya za Kilindi na Handeni katika mkoa wa.” See p. xvi – xvii.

[53] Mahojiano ya Human Rights na Albert Msendo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mji wa Handeni, Aprili 11, 2023.

[54] Imeelezwa kwa kina katika sehemu yenye kichwa cha habari “Unyanyasaji unaofanywa na Askari wanyamapori wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro” hapo chini.

[55] Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (ICESCR), iliyopitishwa Disemba 16, 1966, G.A. Res. 2200A (XXI), 21 U.N. GAOR Supp. (No. 16) at 49, U.N. Doc. A/6316 (1966), 993 U.N.T.S. 3, kuanza kutumika Januari 3, 1976, art. 11; Kamati ya UN ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (CESCR), Maoni ya Jumla Na. 7, Haki ya Makazi yanayokidhi (Kip. 11 (1) cha Mkataba): Kuondolewa kwa lazima, U.N. Doc. E/1998/22 (1997); Baraza la UN la Haki za Binadamu, Ripoti ya Mtaalamu Maalumu juu ya Makazi yanayokidhi kama sehemu ya haki ya kuwa na kiwango kizuri cha maisha, Miloon Kothari, A/HRC/4/18, February 5, 2007, https://documents.un.org/doc/undoc/gen/g07/106/28/pdf/g0710628.pdf?token=g5felgKH0uqeJhX7Vi&fe=true (imepitiwa Julai 2, 2024).

[56] ACHPR, “Azimio la Mtazamo Unaozingatia Haki za Binadamu katika Usimamizi wa Maliasili,” ACHPR/Res.224(LI)2012, https://achpr.au.int/en/adopted-resolutions/224-resolution-human-rights-based-approach-natural-resources-governance-ac (imepitiwa Julai 2, 2024), para 4, wito kwa nchi: “kuhakikisha tathmini huru za athari za kijamii na haki za binadamu ambazo zinahakikisha ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa (FPIC),” kwa kuzingatia hasa haki za wanawake, watu wa asili na mila za watu; Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Watu wa Asili (UNDRIP), iliyopitishwa Septemba 13, 2007, G.A. Res. 61/295, U.N. Doc. A/RES/61/295 (2007), art. 32(2): “Nchi zinapaswa kushauriana na kushirikiana kwa nia njema na watu wa asili kupitia taasisi zao za uwakilishi ili kupata ridhaa huru, ya awali na inayotokana na kuwa na taarifa kabla ya kuidhinisha mradi wowote unaoathiri ardhi au maeneo yao na rasilimali nyingine”; na ILO, Mkataba wa Watu wa Asili na Wakabila, 1989 (No. 169), iliyopitishwa Juni 27, 1989, kuanza kutumika Septemba 5, 1991, (C169) ambao una ujumbe mkuu wa kushauriana na ushirikishwaji, pamoja na Kip. 6, 7.1, 16, and 17.

[57]  Haki ya kujitawala ni kanuni ya msingi katika sheria za kimataifa za haki za binadamu. See ICESCR, art. 1; Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR), iliyopitishwa Disemba 16, 1966, G.A. Res. 2200A (XXI), U.N. Doc. A/6316 (1966), 999 U.N.T.S. 171, art. 1. FPIC vile vile haki za watu wa asili za ardhi, maeneo na maliasili ni sehemu ya haki ya kujitawala. Tazama, kwa mfano, UNDRIP, utangulizi, arts. 3 na 4.

[58] UNDRIP, art. 32(2).

[59] UNDRIP, art. 10.

[60] ACHPR, Azimio la Mtazamo Unaozingatia Haki za Binadamu katika Usimamizi wa Maliasili, ACHPR/Res.224(LI)2012; UNDRIP, art. 32(2); and the ILO C 169, ambao una ujumbe mkuu wa kushauriana na ushirikishwaji, pamoja na arts. 6, 7.1, 16, na 17.

[61] Mahojiano ya Human Rights Watch na Naorokot O., kiongozi wa kimila, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[62] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi (MLUM) ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Mafunzo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii,” Oktoba 2019, https://www.oaklandinstitute.org/sites/oaklandinstitute.org/files/pdfpreview/mlum-final-oct-2019.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024); Wizara ya Maliasili na Utalii, “Mamlaka ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro: Management Zone Plan (2021 – 2025),” Aprili 2021.

[63] Joseph M.L. Oleshangay, “The Truth, Falsity, and Mismanagement: Need for an Interdisciplinary Community-led multi-functional Landscape Management Model in Ngorongoro.” May 2022, https://www.academia.edu/88472219/Truth_Falsity_and_Mismanagment_of_Ngorongoro_Community_Assesment_report_MAY (imepitiwa Julai 2, 2024).

[64] Mahojiano ya Human Rights Watch na Isaac L., diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[65] Mahojiano ya Human Rights Watch na Isaac L., diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[66] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasinka N., councilor, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[67] Mahojiano ya Human Rights Watch na Naorokot O., kiongozi wa kimila, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[68] Mahojiano ya Human Rights Watch na Legishon K., Baraza la Wafugaji Ngorongoro, Arusha, Juni 20, 2023.

[69] Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya mwaka 1982, iliyofanyiwa marekebisho 2002, art. 35(1)(d).

[70] Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya mwaka 1982, iliyofanyiwa marekebisho 2002, art. 45(1)(e). Kuna aina tatu ya muundo wa utawala wa miji nchini Tanzania: Halmashauri ya Mji, Halmashauri ya Manispaa na Halmashauri ya Jiji.

[71] Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) yam waka 1982, iliyofanyiwa marekebsiho 2002, section 19(2)(c), na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya mwaka 1982, iliyofanyiwa marekebisho 2002, art. 56(1)(c). Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992, iliyofanyiwa marekebisho 2019 kupitia Sheria ya Marekebisho ya Vyama vya Siasa (PPAA), pia inavitaka vyama vya siasa kuzingatia kanuni za jinsia na ushirikishwaji wa kijamii katika uteuzi wa wagombea wake, uchaguzi wa viongozi wake na katika kutengeneza nyaraka za sera. Tazama: UN Women, “Viwango vya Jinsia vilivyowekwa kisheria na Serikali za Mitaa, 1 Januari,” 2023, https://localgov.unwomen.org/sites/default/files/2023-06/UN%20Women%20Legislated%20gender%20quotas%20for%20local%20governments%201%20January%202023.pdf (imepitiwa Julai 3, 2024); Isabella Nchimbi, “Ensuring women’s participation in land governance: ‘Brining the law home’ in Tanzania,” International Institute for Environment & Development, January 20, 2021, https://www.iied.org/ensuring-womens-participation-land-governance-bringing-law-home-tanzania (imepitiwa Julai 3, 2024).

[72] UN Women, “Viwango vya Jinsia vilivyowekwa kisheria na Serikali za Mitaa: Tanzania,” Januari 1, 2023, https://localgov.unwomen.org/access-quota-information (imepitiwa Julai 2, 2024).

[73] ACHPR, Azimio la Mtazamo Unaozingatia Haki za Binadamu katika Usimamizi wa Maliasili, ACHPR/Res.224(LI)2012; UNDRIP, art. 32(2); and the ILO C 169, ambao una ujumbe mkuu wa kushauriana na ushirikishwaji, pamoja na arts. 6, 7.1, 16, na 17.

[74] Tazama “Tanzania: Wamasai Wanaondolewa kwa Nguvu kwa ajili ya Pori la Akiba”, taarifa kutoka Human Rights Watch, Aprili 27, 2023, https://www.hrw.org/news/2023/04/27/tanzania-maasai-forcibly-displaced-game-reserve. 

[75] Mahojiano ya Human Rights Watch na Loolenjai N., mwenyekiti wa Kijiji, Karatu, Aprili 6, 2023.

[76] Mahojiano ya Human Rights Watch na Gabriel O., mwenyekiti wa Kijiji, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[77] Mahojiano ya Human Rights Watch na Legishon K., Baraza la Wafugaji wa Ngorongoro, Arusha, Juni 20, 2023; Isaac L., diwani, Lekipisia M., James M., Gabriel O., wenyeviti wa vijiji, na Oleitiko K., kiongozi wa kimila, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[78] Mahojiano ya Human Rights Watch na Isaac L, diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[79] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sadera L., Maasi mwanafunzi wa chuo, Arusha, Juni 20, 2023.

[80] ICESCR, art. 11; CESCR, Maoni ya Jumla Na. 7, Haki ya Makazi ya Kutosha (art. 11 (1) ya Mkataba): Kuondoshwa kwa Lazima, U.N. Doc. E/1998/22 (1997); Baraza la UN la haki za Binadamu, Ripoti ya Mwandishi Maalumu juu ya makazi yanayokidhi kama kigezo cha haki ya kiwango cha maisha kinachotosha, Miloon Kothari, A/HRC/4/18, Februari 5, 2007, https://documents.un.org/doc/undoc/gen/g07/106/28/pdf/g0710628.pdf?token=g5felgKH0uqeJhX7Vi&fe=true (imepitiwa Julai 2, 2024).

[81] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Mafunzo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dodoma, Oktoba 2019.

[82] Mahojiano ya Human Rights Watch na Leinot O., aliyekuwa muuguzi wa kujitolea katika Hospitali ya Endulen, Arusha, Novemba 15, 2022; mahojiano ya kikundi na msimamizi wa NGO ya afya, na mfanyakazi wa usafiri wa anga wa afya, Arusha, Novemba 16, 2022.

[83] Tara B. Mtuy et al., “The role of cultural safety and ethical space within postcolonial health care for Maasai in Tanzania,” BMJ Global Health, vol 7, 11 (2022), imepitiwa Julai 2, 2024, doi:10.1136/ bmjgh-2022-009907; David W. Lawson et al., “Ethnicity and child health in northern Tanzania: Maasai pastoralists are disadvantaged compared to neighboring ethnic groups,” PLoS One (2014) imepitiwa Julai 2, 2024, doi: 10.1371/journal.pone.0110447.; Joseph Christopher Pesambili, “Exploring the responses to and perspectives on formal education among the Maasai Pastoralists in Monduli, Tanzania,” International Journal of Educational Development, vol. 78 (2020), imepitiwa Julai 2, 2024, doi.org/10.1016/j.ijedudev.2020.102267, pp. 1-9; Adella Raymond, “Girls’ participation in formal education:  A case of Maasai pastoralists in Tanzania,” Educational Research for Policy and Practice, vol. 20, 2 (2020): 165-185, imepitiwa Julai 2, 2024, doi:10.1007/s10671-020-09273-7.   

[84] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lolkerra K., Arusha, Novemba 15, 2022.

[85] Kwa mujibu wa NCAA, wanatumia takribani Shilingi za Tanzania bilioni 2 katika program ya ufadhili kila mwaka. “Maendeleo ya Jamii: NCAA na Jamii,” NCAA, imepitiwa Julai 2, 2024, https://www.ncaa.go.tz/community-development/.

[86] Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, 2007.

[87] Mahojiano mbalimbali ya Human Rights Watch na Legishon K., Ngorongoro Baraza la Wafugaji, Juni 20, 2023, Machi 28, 2024.

[88] Mahojiano ya Human Rights Watch na Legishon K., Baraza la Wafugaji wa Ngorongoro, Juni 20, 2023.

[89] Ibid.

[90] Ibid.

[91] Ibid.

[92] Kwa mujibu wa tovuti ya NCAA, NCAA ilianzisha programu ya ufadhili kwa Wanafunzi mwaka 1994 na inaendelea kufadhili programu hiyo. Hata hivyo, programu hiyo kwa sasa inasimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro (NDC). “Maendeleo ya Jamii, Programu na Huduma: Elimu,” NCAA, imepitiwa Julai 2, 2024, https://www.ncaa.go.tz/community-development/.

[93] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sadera L., mwanafunzi Mmasai wa Chuo Kikuu, Arusha, Juni 20, 2023.

[94] Mahojiano ya Human Rights Watch na Leleito L., Arusha, Septemba 15, 2022.

[95] Denis Oleshangay, “Conservation racism in Ngorongoro: A tragic loss of common sense and leadership,” MzwanoTV, August 14, 2023, https://mwanzotv.com/2023/08/14/conservation-racism-in-ngorongoro-a-tragic-loss-of-common-sense-and-leadership/ (imepitiwa Aprili 8, 2024).

[96] Mahojiano kwa njia ya simu ya Human Rights Watch na John O., December 13, 2023; mahojiano ya kikundi na Nasinka N., diwani, Nkasiogi L., Neeris N., na Neelai O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[97] Mahojiano ya Human Rights Watch na Neeris N., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[98] Mahojiano ya Human Rights interview na Naorokot O., kiongozi wa kimila, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[99] Mahojiano ya Human Rights Watch na Neeris N., na Gabriel O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[100] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nkasiogi L., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[101] Mahojiano ya Human Rights Watch na Gabriel O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[102] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasinka S., Karatu, Aprili 10, 2023.

[103] Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, NOTISI: Kuhamishwa kwa fedha za mradi wa kukabiliana na Uviko-19 jumla ya Tzs 160,000,000 kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Machi 31, 2022, NGOR/DC/F.1/02/VOL III/68, Maelekezo haya yako kwenye jalada la Huma Rights Watch; Mahojiano ya Human Rights na Gabriel O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[104] Jess Craig, “‘It’s becoming a war zone’: Tanzania’s Maasai speak out on ‘forced’ removals,” The Guardian, January 16, 2023, https://www.theguardian.com/global-development/2023/jan/16/tanzania-maasai-speak-out-on-forced-removals (imepitiwa Julai 2, 2024).

[105] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasinka N., diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[106] Oleshangay (@Oleshangay), “Don’t panic: African languages are not going extinct. These languages are resilient, evolving, and adapting. They are here to stay. #AfricanLanguages,” Twitter, Oktoba 13, 2022, https://twitter.com/Oleshangay/status/1580638762039549957.

[107] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sironka M., mtumishi wa afya, Endulen, Juni 22, 2023.

[108] Ibid.

[109] Ibid.; Jess Craig, “It’s becoming a war zone:’ Tanzania’s Maasai speak out on ‘forced’ removals,” The Guardian, January 16, 2023, https://www.theguardian.com/global-development/2023/jan/16/tanzania-maasai-speak-out-on-forced-removals (imepitiwa Julai 2, 2024); Doreen Ajiambo, “‘We will not go anywhere’: Maasai resist Tanzanian government evictions,” Global Sisters Report, October 9, 2023, https://www.globalsistersreport.org/news/we-will-not-go-anywhere-maasai-resist-tanzanian-government-evictions (accessed July 2, 2024).

[110] Mahojiano kwa njia ya simu ya Human Rights Watch na Dr Luke M., daktari, Aprili 6, 2023.

[111] Ibid.

[112] “Maasai Rising to Resist Eviction Plans in Ngorongoro Conservation Area,” Oakland Institute news release, February 17, 2022, https://www.oaklandinstitute.org/maasai-rising-resist-eviction-plans-ngorongoro-conservation-area (imepitiwa Julai 2, 2024). Huduma za Usafiri na Anga zilieleza kuwa Huduma za Matibabu za Anga (FMS) hazijalipa ada ya utawala na kupata idhini ya kuruka katika eneo hilo, ijapokuwa kutoka na wasilisho kutoka FMS, ada hiyo iliondolewa kutokana na kuwa ni NGO na inatoa huduma za bure kitu ambacho imekuwa ikifanya tangu 1983.

[113] Mahojiano ya Human Rights Watch na Olumisi L., mwanaharakati, Arusha, Septemba 15, 2022.

[114] Michelle V. Evans et al., “Geographic barriers to care persist at the community healthcare level: Evidence from rural Madagascar,” PLOS Global Public Health, vol. 2, 12 (2022), accessed July 2, 2024, doi: 10.1371/journal.pgph.0001028.; D,J Weiss et al., “Global maps of travel time to healthcare facilities,” Nature medicine, vol. 26, 12 (2020): 1835-1838, imepitiwa Julai 2, 2024, doi: 10.1038/s41591-020-1059-1; Owen O'Donnell, “Access to health care in developing countries: breaking down demand side barriers.” Cadernos de saude publicavol. 23 (2007): 2820-2834, accessed July 2, 2024, doi: 10.1590/s0102-311x2007001200003.

[115] Mahojiano ya Human Rights Watch na Neeris N., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[116] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasinka N., diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[117] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nkasiogi L., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[118] Mahojiano ya Human Rights Watch na Neeris N., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[119] “Kanzidata ya Matumizi ya Afya Ulimwenguni,” WHO, Disemba 2023, imepitiwa Julai 2, 2024, https://apps.who.int/nha/database.

[120] Umoja wa Afrika, “Azimio la Abuja la VVU/UKIMWI, Kifua Kikuu na Magonjwa Mengine ya Kuambukizwa,” OAU/SPS/ABUJA/3, Aprili 27, 2001, https://au.int/sites/default/files/pages/32894-file-2001-abuja-declaration.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024).

[121] Baada ya mkutano ulioandaliwa na Waziri Mkuu Februari 17, 2022, kuwaeleza wakazi kuhusu zoezi la kuwahamisha na mahali pa kujiandikisha.

[122] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sadera L., Maasai mwanafunzi wa chuo kikuu, Arusha, Juni 20, 2023.

[123] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasinka N., councilor, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[124] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemuani N., Arusha, Novemba 15, 2022.

[125] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sadera L., mwanafunzi Mmasai wa chuo kikuu, Arusha, Juni 20, 2023.

[126] Mahojiano ya Human Rights Watch na Oleitiko K., kiongozi wa kimila, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[127] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lolkerra K., mwanaharakati, Arusha, Septemba 15, 2022.

[128] Tazama Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, 1959, kifungu 9A kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (Marekebisho), Na. 14, 1975, kifungu 14, kwa sasa Sheria ya Eneo la Hifahi ya Ngorongoro, 2002, Sehemu ya IV – Udhibiti wa kilimo  na ufugaji na ulinzi wa maliasili, kifungu 24-28; Sheria ya Eneo la Hifadhi (Marekebsiho Mengineyo), 1975, Na. 14; Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (Udhibiti wa Makazi, Wakazi na Kuzuia Mmonyoko wa Udongo, Mimea na Wanyama) Sheria ndogo, 1992; Wizara ya Maliasili na Utalii, “Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro: Mpango wa Eneo la Usimamizi (2021 – 2025),” Aprili 2021; na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moduli ya Matumizi Mtambuka ya Ardhi ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: Mafanikio na Mafunzo, Changamoto na Machaguo ya baadaye: Ripoti Kamili, Wizara ya Maliasili na Utalii, 2019.

[129] Mahojiano ya Human Rights Watch na Joseph M., diwani, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[130] Mahojiano ya  Human Rights Watch na Loolenjai N., mwenyekiti wa kijiji, Mto wa Mbu, 21 Juni 2023.

[131] Anthony Jan Mills and Antoni V. Milewski, “Geophagy and nutrient supplementation in the Ngorongoro Conservation Area, Tanzania, with particular reference to selenium, cobalt and molybdenum,” Journal of zoology, vol. 271, 1 (2006): 110-118, imepitiwa Julai 2, 2024, doi: 10.1111/j.1469-7998.2006.00241.x.

[132] Ibid.

[133] Mahojiano ya Human Rights Watch na Simon M., Joseph M., na Naengop S., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[134] Ibid. Kwa mujibu wa Ripoti ya Tanzania ya mwaka 2015 ya Hali ya Uhifadhi katika eneo la NCA kwa Kituo cha Urithi wa Duni cha UNESCO, mradi wa kuboresha mifugo katika shamba la majaribio kitongoji cha Ngairish, kata ya Kakesio uliandaliwa kwa ajili ya kushughulikia athari hasi zilizotokana shinikizo la kuongezeka kwa ufugaji na idadi ya watu. “Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro: 2015” UNESCO, imepitiwa Julai 2, 2024, https://whc.unesco.org/en/soc/3255/.

[135] Joseph Moses Oleshangay, “Unmasking Government Controversial Proposals in Ngorongoro,” The Chanzo, February 7, 2022, https://thechanzo.com/2022/02/07/unmasking-government-controversial-proposals-in-ngorongoro/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[136] Wakala wa Maabara ya Mifugo Tanzania (TVLA), Cheti cha Ripoti yaa Uchunguzi: Kipengele cha Chakula, Disemba 27, 2021, Wizara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi. NCAA iliwasilisha Sampuli TVLA. Uchunguzi uligundua kiwango cha madini ya calcium katika sampuli kilikuwa juu kuliko ilivyooneshwa katika kibandiko, kulikuwa na chembechembe za madini risasi kwa kiwango cha juu kuliko kinavyokubalika katika mchanganyiko wa malisho, na sampuli zilikuwa zimechafuliwa na silicon. “Dalili za Uchakachuaji na kuweka taarifa zinazopotosha katika kibandiko kumepelekea hitimisho kuwa chumvi haikuzingatia Kanuni za Rasilimali za Malisho ya Wanyama na Ardhi ya Malisho (Kiwango cha Rasilimali ya Malisho kwa Wanyama) ya 2012.”

[137] Mahojiano ya Human Rights Watch na Namunyal S., mwenyekiti wa kijiji, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[138] Mahojiano ya Human Rights Watch na Simon M., Joseph M., na Naengop S., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[139] Mahojiano ya Human Rights Watch na Loolenjai N., mwenyekiti wa kijiji, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[140] Mahojiano kwa njia ya simu ya Human Rights Watch na John O., Oktoba 19, 2023.

[141] Mahojiano ya Human Rights Watch na Loolenjai N., mwenyekiti wa kijiji, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[142] Mahojiano ya Human Rights Watch na Neeris N., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[143] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lenein O., Isaac L., diwani, Nkasiogi L., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[144] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nkasiogi L., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[145] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sheria ya kurekebisha Sheria ya Hifadhi za Taifa na Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Na. 14, 1975, Sec. 9a; Sheria ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro (Marekebisho), Na. 14, 1975, kifungu 14; kwa sasa Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, 2002, Part IV – Kudhibiti kilimo na malisho na ulinzi wa maliasili, vifungu 24-28.

[146] Issa Shivji and Wilbert B. Kapinga, Maasai Rights in Ngorongoro, Tanzania (London: International Institute for Environment and Development, 1998), https://www.iied.org/7382iied (imepitiwa Julai 2, 2024), pp. 25-26. See: McCabe, J. Terrence, Scott Perkin, and Claire Schofield. “Can Conservation and Development be Coupled among Pastoral People? An Examination of the Maasai of the Ngorongoro Conservation Area, Tanzania.” Human Organization vol. 51, no. 4 (1992): 353–366, imepitiwa Julai 2, 2024, doi: 10.17730/humo.51.4.d20010q600v50240.

[147] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasinka N., Diwani, Nkasiogi L., Neeris N., na Neelai O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[148] John G. Safari, Moita K. Kirwa, and Christina G. Mandara, “Food insecurity in pastoral communities of Ngorongoro conservation area, Tanzania,” Agriculture and Food Security, vol. 11, no. 36 (2022), imepitiwa Julai 2, 2024, doi:  10.1186/s40066-022-00374-5; International Work Group for Indigenous Affairs (IWGIA), “Tanzania: Hunger in a World Heritage Site. Where is the World?,” 2012, https://www.iwgia.org/en/tanzania/1788-tanzania-hunger-in-a-world-heritage-site-where-is.html (imepitiwa Julai 2, 2024).

[149] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemarti O., kiongozi wa kimila, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[150] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemein O., Endulen, Juni 22, 2023.

[151] “Taarifa,” NCAA, imepitiwa Julai 2, 2024, https://www.ncaa.go.tz/information/.

[152] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lolkerra K., mwanaharakati, Arusha, Septemba 15, 2022.

[153] Mahojiano ya Human Rights Watch na Isaac L., diwani, na Naorokot O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023. Askari Wanyamapori ndani ya NCA wanasimamiwa na NCAA na sio Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) au Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA).

[154] Tazama “Tanzania: Wamasai Wanaondolewa kwa nguvu kupisha Pori la Akiba,” taarifa ya Human Rights Watch, Aprili 27, 2023, https://www.hrw.org/news/2023/04/27/tanzania-maasai-forcibly-displaced-game-reserve. 

[155] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemuani N., Arusha, Novemba 15, 2022.

[156] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lolkerra K., mwanaharakati, Arusha, Novemba 15, 2022. Kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi za Taifa, 2003, Cap 412, Kanuni, art. 18, “Shughuli za kuruka na parachuti, kuendesha baiskeli, kutelea kwenye theluji, na kuning’inia kwa mikono haziruhusiwi.”

[157] Musa Juma, “Ngorongoro Rangers Accused of Pulling Out Herder’s Teeth,” The Citizen, Julai 16, 2023, https://www.thecitizen.co.tz/tanzania/news/national/ngorongoro-rangers-accused-of-pulling-out-herder-s-teeth--4305222 (imepitiwa Julai 2, 2024).

[158] Mahojiano ya Human Rights Watch na Neeris N., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[159] Mahojiano ya Human Rights Watch na Naetoi L., Arusha, Apriil 10, 2023.

[160] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemein O., Endulen, Juni 22, 2023.

[161] Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori, 2022, art. 13. Haki ya Kumiliki na kutumia silaha za moto na risasi Cap. 223

[162] Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, 2002, kifungu 37. Mamlaka ya Kukamata; Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori, 2022, art 106.

[163] Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, 2002, section 37; Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori, 2022, art 106.

[164] Mahojiano ya Human Rights Watch na Simon M., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[165] “Halmashauri ya Wilaya ya Handeni: Takwimu za haraka,” imepitiwa Julai 2, 2024, https://handenidc.go.tz/.

[166] Oakland Institute, “Fact Finding Report: Field Research at the Resettlement Site,” 2022, https://www.oaklandinstitute.org/sites/oaklandinstitute.org/files/pdfpreview/field_research_msomera_resettlement_site_october_2022.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024).

[167] UNESCO, “Ripoti ya Hali ya Uhifadhi,” 2023, https://whc.unesco.org/document/198961 (imepitiwa Julai 2, 2024), p. 1; “Social services availability attracts more villagers to shift to Msomera,” Daily News, August 15, 202, https://dailynews.co.tz/social-services-availability-attracts-more-villagers-to-shift-to-msomera/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[168] Mahojiano ya Human Rights Watch na Albert Msendo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Handeni, Aprili 11, 2023.

[169] Bob Karashani and Apolinari Tairo, “Tanzania spends millions to move, build new life in Tanga for Loliondo Maasai,” The East African, June 26, 2022, https://www.theeastafrican.co.ke/tea/news/east-africa/tanzania-relocates-loliondo-maasai-to-tanga-3860046 (imepitiwa Julai 2, 2024).

[170] Hilda Mhagama, “PM Majaliwa directs two districts to manage Msomera village,” Daily News, March 8, 2023, https://dailynews.co.tz/pm-majaliwa-directs-two-districts-to-manage-msomera-village/ (imepitiwa Julai 2, 2024).Mwezi Machi 2023, Waziri Mkuu aliweka Kijiji cha Msomera chini ya usimamizi wa wakuu wawili wa wilaya– wilaya za Handeni na Kilindi.

[171] Mahojiano ya Human Rights Watch na Micheal R., Msomera, Juni 24, 2023.

[172] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemayian L., Msomera, Juni 24, 2023.

[173] Ibid.

[174] Ibid.

[175] Mahojiano ya Human Rights Watch na Micheal R., Msomera, Juni 24, 2023.

[176] Mahojiano ya Human Rights Watch na Samuel M., Msomera, Juni 24, 2023.

[177] Mahojiano ya Human Rights Watch na Micheal R., Msomera, Juni 24, 2023.

[178] Damian Gowela, “Govt: All Projects at Msomera to be Completed On,” Daily News, November 27, 2023, https://dailynews.co.tz/govt-all-projects-at-msomera-to-be-completed-on/ (imepitiwa Julai 3, 2024).

[179] Mahojiano ya Human Rights Watch na Samson L., Msomera, Juni 24, 2023.

[180] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemayian L., Msomera, wilaya ya Handeni, Juni 24, 2023. Serikali iliahidi hati za umiliki wa ardhi kwa familia zilizohamia Msomera. Mipango ya serikali inakinzana, ikidai kwamba umiliki wa mtu binafsi utasababisha usalama wa umiliki kwa wakazi waliohamia kutoka NCA, i.e. hati miliki itatambulika, kuweka kumbukumbu sahihi, na kulinda haki yao ya ardhi Msomera, wakati ikipuuza madai ya wakazi wa Msomera juu ya ardhi hiyo, ikiwa ni pamoja na madai ya hati miliki. Madai mbalimbali ya ardhi yapo katika ardhi moja katika hali hii, uwezekano wa usajili wa haki ya kumiliki kwa wakazi waliohamia kutoka NCA unapelekea mashaka kwa wakazi wa Msomera waliokuwepo tangu awali, na inaweza kudhoofisha haki ya ardhi kwa watu kama, wanawake, ambao wanategemea mila na desturi kulinda upatikanaji wa rasilimali na madai yao ya ardhi.

[181] Mahojiano ya Human Rights Watch na Micheal R., Msomera, Juni 24, 2023.

[182] Ibid.

[183] Sheria ya Ardhi, Cap 113, kifungu 3(1)(g), iliyoanza Mei 1, 2001, inasisitiza kanuni za msingi za Sera ya Tanzania ya Ardhi kuwa “kulipa fidia kamili, ya haki na kwa wakati kwa mtu yeyote ambaye haki yake ya kumiliki au umiliki wa muda mrefu unaotambulika au matumizi ya kimila ya ardhi yamebatilishwa au kuingiliwa na serikali chini ya Sheria hii au inachukuliwa chini ya Sheria ya Utwaaji Ardhi.” Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, Kifungu 24(2), kinaeleza: “Itakuwa ni kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kunyang’anywa mali yake kwa madhumuni ya kutaifisha au madhumuni mengine yeyote bila ya mamlaka ya sheria ambayo inatoa nafasi kwa fidia ya haki na inayokidhi.”

[184] Kanuni ya Ardhi (Uthamini wa Thamani ya Ardhi kwa ajili ya Fidia) 2001, Kanuni ya 7.

[185] Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu (OHCHR), “Haki za Wanawake ni Haki za Binadamu,” 2014, https://www.ohchr.org/sites/default/files/Documents/Events/WHRD/WomenRightsAreHR.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024), p. 30: hii itapelekea ubaguzi kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Kutokomeza Aina zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW), imepitishwa Disemba 18, 1979, G.A. Res. 34/180, U.N. Doc. A/RES/34/180 (1980), art. 16(1)(c).

[186] Mahojiano ya Human Rights Watch na Legishon K., Baraza la Wafugaji la Ngorongoro, Arusha, Juni 20, 2023.

[187] Mahojiano ya kikundi ya Human Rights Watch na Wamasai wanaume saba, Endulen, Juni 22, 2023.

[188] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lemarti O., Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[189] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lankenua L., Msomera, Aprili 11, 2023.

[190] Mahojiano ya Human Rights Watch na Evelyn S., Msomera, Aprili 11, 2023.

[191] Rosemary Mirondo, “‘We’ll Not Apply Force to Relocate Maasai Families,’” The Citizen, November 4, 2023, https://www.thecitizen.co.tz/tanzania/news/national/-we-ll-not-apply-force-to-relocate-maasai-families--4452742 (imepitiwa Julai 3, 2024).

[192] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lankenua L., Msomera, Aprili 11, 2023.

[193] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mary I., Msomera, Aprili 11, 2023.

[194] Mahojiano ya Human Rights Watch na Legishon K., Baraza la Wafugaji la Ngorongoro, Arusha, Juni 20, 2023.

[195] Ibid.

[196] Rosemary Mirondo, “‘We’ll Not Apply Force to Relocate Maasai Families,’” The Citizen, November 4, 2023, https://www.thecitizen.co.tz/tanzania/news/national/-we-ll-not-apply-force-to-relocate-maasai-families--4452742 (imepitiwa Julai 3, 2024).

[197] Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), “Taarifa ya Hali ya Hewa Tanzania 2022,” Machi 2023, https://www.meteo.go.tz/uploads/publications/sw1680520682-Tanzania%20Climate%20Statetement%202022.pdf (accessed July 2, 2024), pp. 17, 18, 22, 26.

[198] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mary I., Msomera, Aprili 11, 2023.

[199] Mahojiano ya Human Rights Watch na Albert Msendo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Handeni, Aprili 11, 2023.

[200] Mahojiano ya Human Rights Watch na Koinet S., – mwenyekiti wa kijiji, Mto wa Mbu, Juni 21, 2023.

[201] Tazama histori, Kitabu: Kuondoshwa kwa Lazima kwa Wamasai kutoka Maeneo mengine ya Wilaya ya Ngorongoro, p. 22.

[202] “Tanzania: End the crackdown on the Maasai standing up against forced evictions in Ngorongoro,” Amnesty International new release, August 25, 2023, https://www.amnesty.org/en/latest/news/2023/08/tanzania-must-end-crackdown-on-masaai-fighting-forced-evictions/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[203] Chapisho la Twitter la Gerson Msigwa, Katibu Mkuu Utamaduni, Sanaa na Michezo na zamani msemaji mkuu wa serikali, mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu, Msigwa Gerson (@MsigwaGerson), “Today, President Samia will witness the signing of the agreement for the project to construct a natural gas pipeline from Tanzania to Kenya, from Dar es Salaam to Mombasa. The agreement will be signed by Kenya's Minister of Energy, Davis Chirchir, and Tanzania's Dr. Doto Biteko (Leo, Rais Samia atashuhudia utiaji saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Tanzania kwenda Kenya, kutoka Dar es Salaam hadi Mombasa. Mkataba huo utasainiwa na Waziri wa Nishati wa Kenya Davis Chirchir na Dkt. Doto Biteko wa Tanzania)” Twitter, Agosti 16, 2023, https://twitter.com/MsigwaGerson/status/1691541542928809984?t=6bbryis7g5F8VsSVSbO6eg. 

[204] “Msomera Villagers Pleading with To President Samia Suluhu Hassan, Enable Them Given Back Their land,” First Newsroom, April 24, 2023, https://firstnewsroom.com/2023/04/24/msomera-villagers-pleading-to-president-samia-suluhu-hassan-enable-them-given-back-their-land/ (imepitiwa July 2, 2024).

[205] Mahojiano ya Human Rights Watch na Matthew K., Msomera, Juni 24, 2023.

[206] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa NGO, Dar es Salaam, Juni 25, 2023.

[207] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa NGO, Arusha, Juni 23, 2023.

[208] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa NGO, Dar es Salaam, 25 Juni 2023.

[209] Mahojiano ya Human Rights Watch mwakilishi wa NGO, Arusha, Juni 23, 2023.

[210] “Alarm Raised on Safety of Human Rights Activist Joseph Moses Oleshangay,” The Chanzo, March 28, 2024, https://thechanzo.com/2024/03/28/alarm-raised-on-safety-of-human-rights-activist-joseph-moses-oleshangay/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[211] Doreen Ajiambo, “‘We will not go anywhere:’ Maasai resist Tanzanian government evictions,” Global Sisters Report, October 9, 2023, https://www.globalsistersreport.org/news/we-will-not-go-anywhere-maasai-resist-tanzanian-government-evictions (imepitiwa Julai 2, 2024).

[212] Mahojiano ya Human Rights Watch na wawakilishi wa NGO, Dar es Salaam, 25 Juni 2023. Pia tazama: “Alarm Raised on Safety of Human Rights Activist Joseph Moses Oleshangay,” The Chanzo, March 28, 2024, https://thechanzo.com/2024/03/28/alarm-raised-on-safety-of-human-rights-activist-joseph-moses-oleshangay/ (imepitiwa Julai 2, 2024).

[213] Mkata wa Kimataifa wa Kutokomeza Aina Zote za Ubaguzi wa Rangi (ICERD), imepitishwa Disemba 21, 1965, G.A. Res. 2106 (XX), annex, U.N. GAOR, 20th Sess., Supp. No. 14, U.N. Doc. A/6014 (1966), 660 U.N.T.S. 195, ambao Tanzania imeridhia mwaka 1972; ICCPR, ambao Tanzania imeridhia mwaka 1976; ICESCR, ambao Tanzania imeridhia mwaka 1976; CEDAW, ambao Tanzania imeridhia mwaka 1985; Mkataba wa Haki za Mtoto (CRC), uliopitishwa Novemba 20, 1989, G.A. Res. 44/25, U.N. Doc. A/RES/44/25 (1989), ambayo Tanzania imeridhia mwaka 1991.

[214] Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu (Mkataba wa Afrika), uliopitishwa Juni 27, 1981, OAU Doc. CAB/LEG/67/3 rev. 5, 21 I.L.M. 58 (1982), ambao Tanzania imeridhia mwaka 1984; Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto, uliopitishwa Julai 11, 1990, OAU Doc. CAB/LEG/24.9/49 (1990), ulioanza kutumika Novemba 29, 1999, ambao Tanzania imeridhia mwaka 2003; Itifaki ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu kuhusu Haki za Wanawake Afrika, umepitishwa Julai 11, 2003, OAU Doc. CAB/LEG/66.6/Rev.1, 1 I.L.M. 1000 (2003), ambayo Tanzania imeridhia mwaka 2007.

[215] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Constitution ya mwaka 1977.

[216] Sheria ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro ya mwaka 1959; Sheria ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro (Marekebisho), Cap 284. No. 43 ya 1963, kifungu 6(c). 

[217] Sheria ya Hifadhi Eneo la Ngorongoro (Marekebisho), Cap 284, kifungu 6(c).

[218] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara 9(a) and (f).

[219] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara 24(1).

[220] Sheria ya Ardhi, Sura 113, iliyoanza 1 Mei 2001, section 4(3).

[221] Sheria ya Vijiji, Sura 114, iliyoanza 1 May 2001, section 7(e)(iii).

[222] “Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa juu ya Masuala ya Watu wa Asili,” Juni 14, 2022, https://www.un.org/development/desa/indigenouspeoples/wp-content/uploads/sites/19/2022/06/Statement_Loliondo_letterhead.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024). Tazama pia, Thomas M. Lekan, “Our Gigantic Zoo: A German Quest to Save the Serengeti,” in Serengeti II: Dynamics, Management, and Conservation of an Ecosystem, eds. A.R.E. Sinclair and Peter Arcese. (Chicago: The University of Chicago Press, 1995).

[223] Azimio la Dunia la Haki za Binadamu (UDHR), G.A. Res. 217A (III), U.N. GAOR, 3rd Sess., pt. I, U.N. Doc. A/810 (1948), art. 17; ACHPR, June 27, 1981, CAB/LEG/67/3 rev. 5, 21 I.L.M. 58, art. 14.

[224] CESCR, Maoni ya Jumla No. 4, Haki ya makazi yanayokidhi (Sixth session, 1991), U.N. Doc. E/1992/23, annex III, art. 114 (1991).

[225] Umoja wa Mataifa, Haki za Ardhi na Binadamu: Mkusanyiko wa Ufafanuzi wa Sheria ya Kesi, HR/PUB/15/5

[226] Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu: Kituo cha Haki za Makazi na Kuondoshwa (COHRE) v. Sudan, Communication No. 296/2005, Julai 29, 2009, para. 205. Katika kesi ya COHRE v. Sudan, Tume ya Afrika iligundua kwamba “haijalishi kama wana hati miliki ya ardhi, ukweli kuwa waathirika hawawezi kuendesha maisha yao kutokana na kile walichomiliki vizazi kwa vizazi inamaanisha kuwa wamenyimwa kutumia mali yao chini ya masharti ambayo hayaruhusiwi na Ibara ya 14 [haki ya kumiliki mali].”

[227]Mwanasheria Mkuu vs. Lohay Akonaay na Mwengine (Civ. App. No. 31 of 1994) https://tanzlii.org/tz/judgment/court-appeal-tanzania/1994/1 (imepitiwa Julai 2, 2024), para 25.

[228] “General Assembly Adopts Declaration on Rights of Indigenous Peoples; ‘Major Step Forward’ towards Human Rights for All, Says President,” Meeting Coverage and Press Releases, September 13, 2007, https://press.un.org/en/2007/ga10612.doc.htm (imepitiwa Aprili 18, 2024); UNDRIP, art. 26.

[229] Azimio la UN kuhusu Haki za Wakulima na Watu Wengine Wanaofanya kazi Vijijini (UNDROP), iliyopitishwa Septemba 28, 2018, U.N. Doc. A/HRC/RES/39/12; Azimio la Umoja wa Mataifa la Haki za Wakulima na Watu Wengine Wanaofanya Kazi Vijijini, Kumbukumbu za Kura katika Mkutano Mkuu, 2018, https://digitallibrary.un.org/record/1656160?ln=en (accessed July 2, 2024).

[230] ICCPR inaeleza kuwa “hakuna mtu atakayeingiliwa kiholela au kinyume cha sheria katika … makazi yake,” na kila mtu ana haki ya kulindwa dhidi ya kuingiliwa huko. ICCPR, art. 17. Tazama pia ICESCR, art. 11.

[231] Maelezo ya ICESCR kuhusu haki ya makazi yametafsiriwa na CESCR, Katika Maoni yake ya Jumla Na. 7, kupiga marufuku kuondoshwa kwa lazima.

[232] Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu pia imehimiza kumaliza uondoshwaji wa lazima, kwa nchi au mtu mwingine, pamoja na kwa sababu za maendeleo. Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, “Azimio juu ya haki ya makazi na ulizni dhidi ya kuondoshwa kwa lazima,” 2012, https://achpr.au.int/en/adopted-resolutions/231-resolution-right-adequate-housing-and-protection-forced-eviction (imepitiwa Julai 2, 2024); Tazama pia Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, “Kanuni na Miongozo ya Utekelezaji wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni katika Mkataba wa Afrika wa haki za Binadamu na Watu,” 2010, https://archives.au.int/bitstream/handle/123456789/2063/Nairobi%20Reporting%20Guidelines%20on%20ECOSOC_E.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024), para. 55 (a). Vile vile, Mkataba wa Umoja wa Afrika wa Ulinzi na Msaada wa Wakimbizi wa Ndani Afrika (Mkataba wa Kampala), iliyopitishwa Oktoba 23, 2009, AU Doc. EX.CL/568 (XVII) (2009), art. 4, inaeleza, “kila mtu ana haki ya kutokuondolewa kwa lazima kutoka kwenye makazi, ardhi au mali yake na atalindwa dhidhi ya kuhamishwa kiholela.”

[233] Mkataba wa Afrika art. 17(2).

[234] UDHR, art. 27; ICESCR, art. 15(1). Kwa uchambuzi, tazama Elissavet Stamatopoulou-Robbins, Haki ya Utamaduni katika Sheria ya Kimataifa: Ibara ya 27 ya Azimio la Dunia kuhusu Haki za Binadamu na zaidi (Leiden: Koninklijke Brill NV, 2007); Gudmundur Alfredsson and Asbjørn Eide, Azimio la Dunia kuhusu Haki za Binadamu (Boston: Martinus Nijhoff Publishers, 1999); Ana Vrdoljak, ed., Kipimo cha Utamaduni wa Haki za Binadamu (New York: Oxford University Press, 2013).

[235] UNDRIP, art. 11(1).

[236] ACHPR, art. 22.

[237] Azimio la U.N. kuhusu Haki ya Maendeleo, U.N. GAOR, 41st Sess., Doc. A/RES/41/128 (1986), art. 1.1. “Haki ya maendeleo ni haki ya binadamu isiyoweza kuondolewa kwa sababu hiyo kila mtu na watu wote wanastahili kushiriki, kuchangia, na kufurahia maendeleo ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa ambapo haki zote za binadamu na uhuru wa msingi unapatikana kikamilifu.”

[238] Kituo cha Maendeleo ya Haki za Wachache (Kenya) na Kundi la Haki za Wachache (kwa niaba ya Baraza la Ustawi wa Endorois) v. Kenya, 276/03, Uamuzi, para. 277.

[239] Ibid.

[240] Azimio la U.N. kuhusu Haki ya Maendeleo, U.N. GAOR, 41st Sess., Doc. A/RES/41/128 (1986), Kipengele cha 2.3, ambacho kinaeleza “ushiriki hai, huru na wa maana katika maendeleo.” See Arjun Sengupta, “Development Cooperation and the Right to Development,” Francois-Xavier Bagnoud Centre Working Paper No. 12, 2003, http://tanzaniagateway.org/docs/Development_cooperation_and_the_Right_to_Development.pdf (imepitiwa Julai 3, 2024).

[241] Tazama Kituo cha Maendeleo ya Haki za Wachache (Kenya) na Kundi la Haki za Wachache (kwa niaba ya Baraza la Ustawi wa Endorois) v. Kenya, 276/03, Uamuzi, para 278.

[242] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, art. 21(2).

[243] ACHPR, “Maoni ya Jumla 7: Wajibu wa Nchi chini ya Mkataba wa Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu katika muktadha wa utoaji binafsi wa huduma za kijamii,” imepitishwa Julai 28, 2022, https://achpr.au.int/en/documents/2022-10-20/general-comment-7-state-obligations-under-african-charter-human (imepitiwa Julai 2, 2024), paras. 15-16.

[244] Baraza la U.N la Haki za Binadamu., “Haki ya ardhi chini ya Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki ya Watu wa Asili: mwelekeo wa haki za binadamu,” A/HRC/EMRIP/2019/3/Rev.1, para. 5.

[245] UNDRIP, art. 10; Baraza la U.N. la Haki za Binadamu, “Ridhaa Huru, ya Awali na Inayotokana na kuwa na Taarifa: mtazamo unaozingatia haki za binadamu,” A/HRC/39/62, para. 14.

[246] Ibid. arts. 18, 19, and 32.

[247] UNDROP, art. 10(2).

[248] Tazama Kituo cha Maendeleo ya Haki za Wachache (Kenya) na Kundi la Haki za Wachache (kwa niaba ya Baraza la Ustawi wa Endorois) v. Kenya, 276/03, Uamuzi, para. 291.

[249] CEDAW etc.

[250] CEDAW, art. 5.

[251] CEDAW, art 14(2)(g).

[252] Azimio la Rio kuhusu Mazingira na Maendeleo, uliopitishwa Juni 14, 1992, U.N. Doc. A/CONF.151/26 (vol. I), (1992).

[253] Mkataba wa Afrika wa Uhifadhi wa Mazingira na Maliasili, uliopitishwa Julai 11, 2003, Maputo, Mozambique, AU Doc. CAB/LEG/24.1., arts. XVI(1) and XVII(1).

[254] CESCR, Maoni ya Jumla Na. 7, Haki ya Makazi yanayokidhi (art. 11 (1) of the Covenant): Kuondoshwa kwa Lazima, U.N. Doc. E/1998/22 (1997), para. 15. Kwa kuongezea, mamlaka zinapaswa kutoa notisi inayokidhi na inayoeleweka kwa watu wanaoathrika kabla ya tarehe iliyopangwa kuwaondosha; taarifa kuhusu mapendekezo ya kuondoshwa, na pale inapofaa, kuhusu lengo mbadala la matumizi ya makazi au ardhi, zipatikane kwa wakati sahihi kwa wale wanaoathirika; kuhakikisha pale ambapo makundi ya watu yanahusika, maafisa wa serikali au wawakilishi wao wanakuwepo pale uondoshwaji unapofanyika; kuhakikisha watu wote wanaosimamia uondoshwaji wanatambulika vema; kuhakikisha zoezi la kuwaondoa watu halifanyiki katika hali mbaya ya hewa au usiku isipokuwa pale anayeathirika anapokuwa ameridhia vinginevyo; kuhakikisha utoaji wa suluhu za kisheria; na utoaji, pale inapowezekana wa msaada wa kisheria kwa mtu anayehitaji kutafuta suluhu kupitia mahakama.

[255] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia, Ibara ya 18 (a)-(d).

[256] ICCPR, art. 19.

[257] Kamati ya UN kuhusu Haki za Binadamu, Maoni ya Jumla Na. 34, Haki ya Kupata Taarifa, U.N. Doc. CCPR/C/GC/34 (2011), paras. 18-19.

[258] Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu, arts. 9, 11; Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, Tamko la Kanuni za Uhuru wa Kujieleza na Kupata Habari Afrika, iliyopitishwa Novemba 2019, Part III, Haki ya Kupata Taarifa.

[259] Azimio la Rio kuhusu Mazingira na Maendeleo.

[260] Katiba, Ibara. 18 na 20.

[261] UDHR, art. 19; ICCPR, art. 19; Mkataba wa Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu, arts. 9 and 11.

[262] Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu, art. 9; Tume ya Afrika ya Haki za binadamu na Watu, Tamko la Kanuni za Uhuru wa Kujieleza na Kupata Habari Afrika.

[263] ICCPR, art. 19(3) and 20(2). OHCHR, Maoni ya Jumla Na. 10: Uhuru wa kujieleza (Art. 19), U.N. Doc. 29/06/1983 (1983).

[264] ICESCR, arts. 13 and 14; CRC, art. 28.

[265] ICESCR, art. 2; and CRC, art. 2, Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto, art. 3.

[266] CRC, Maoni ya Jumla Na. 11 (2009) Watoto wa jamii ya Asili na haki zao katika Mkataba, UN Doc. CRCC/GC/11, January 12-30, 2009, para. 25.

[267] ICESCR, art. 2(1); CRC, art. 4.

[268] CESCR, Maoni ya Jumla Na. 13: Haki ya Kupata Elimu (Art. 13), U.N. Doc. E/C.12/1999/10 (1999), para. 45.

[269] CESCR, Maoni ya Jumla Na. 3: Wajibu wa Nchi Wanachama (Art. 2, para. 1, of the Covenant), U.N. Doc. E/1991/23 (1990), para. 9.

[270] CRC, Maoni ya Jumla Na. 11 (2009) Watoto wa jamii ya Asili na haki zao katika Mkataba, para. 60.

[271] Mkutano Mkuu wa UN, Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu 17 Disemba 2015, 70/169. Haki wa binadamu kupata maji safi na usafi wa mazingira, U.N. Doc. A/RES/70/169 (2016), para. 2. Haki ya usafi wa mazingira inaeleza“kila mmoja, bila ya ubaguzi, kupata huduma za usafi wa mazingira, katika nyanja zote za maisha, ambao ni salama, safi, iliyolindwa, inayokubalika kijamii na kiutamaduni na inayotoa faragha na kuhakikisha utu;” CESCR, Taarifa kuhusu Haki ya Usafi wa Mazingira, (Forty-fifth session, 2010), U.N. Doc. E/C.12/2010/1, para. 7.

[272] CEDAW, art. 10; CEDAW, Mapendekezo ya Jumla Na. 36, Haki ya wanawake na wasichana kupata Elimu, (2017), U.N. Doc. CEDAW/C/GC/36.

[273] ICESCR, art. 12.

[274] ICESCR, art. 2(1); OHCHR, Haki ya Afya, Factsheet No. 31. https://www.ohchr.org/sites/default/files/Documents/Publications/Factsheet31.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024), p. 24.

[275] Ibid., p. 4.

[276] Ibid.

[277] ACHPR, art. 16.

[278] CEDAW, arts. 11 (1)(f), 12 na 14 (2)(b).

[279] CRC, art 24.

[280] CEDAW, art. 12; CEDAW, Mapendekezo ya Jumla Na. 24, Kifungu cha 12 Cha Mkataba (Wanawake na Afya), U.N. Doc. A/54/38/Rev.1, chap. I, (1999).

[281] CRC, Maoni ya Jumla Na. 11 (2009) Watoto wa jamii za asili na haki zao chini ya CRC, para. 53.

[282] Tume ya UN ya Haki za Binadamu (UNCHR), Muhtasari wa Sera na Mwandishi Maalumu wa Haki za Binadamu na Mazingira, “Mtazama unaozingatia haki za binadamu katika uhifadhi wa uoto wa asili: usawa, ufanisi na lazima,” Agosti 2021, https://www.ohchr.org/sites/default/files/Documents/Issues/Environment/SREnvironment/policy-briefing-1.pdf (accessed July 2, 2024), p. 20.

[283] Ibid.

[284] Mkataba wa Afrika uliofanyiwa Marekebisho kuhusu Uhifadhi wa Mazingira na Maliasili, Article XVII(1), uliopitishwa Julai 11, 2013, https://au.int/en/treaties/african-convention-conservation-nature-and-natural-resources-revised-version (imepitiwa Julai 2, 2024).

[285] Mkutano Mkuu wa UN, Ripoti ya Mwandishi Maalumu wa haki za watu wa asili, José Francisco Calí Tzay, Maeneo yanayolindwa na haki za watu wa asili: wajibu wa nchi na mashirika ya kimataifa, U.N. Doc. A/77/238 (2022), para. 66; Tazama Kituo cha Maendeleo ya Haki za Wachache (Kenya) na Kundi la Haki za Wachache (kwa niaba ya Baraza la Ustawi wa Endorois) v. Kenya, 276/03, Uamuzi, paras. 277 – 278.

[286] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yam waka 1977, art. 24(2); Sheria ya Vijiji, Cap 114, section 4 (1 and 2), imeanza kutumika Mei 1, 2001.

[287] Sheria ya Utwaaji wa Ardhi, Cap 118, section 11(1), imeanza kutumika Machi 23, 1968. Kifungu cha 11(2) cha Sheria ya Utwaaji wa Ardhi kinaeleza kuwa Rais anaweza, badala ya kulipa fidia ya pesa, kutoa viwanja katika eneo la umma kwa watu walioathirika. Viwanja hivyo lazima viwe na thamani na kwenye hali kama ardhi iliyotwaliwa. Viwanja vinaweza kuwa mbadala wa au nyongeza ya fidia ya pesa. Sharti kubwa ni muathirika kuridhia utaratibu huo. Kifungu cha 12(3) cha Sheria ya Utwaaji wa Ardhi kinaeleza viwanja mbadala lazima vitolewe pale ambapo ardhi iliyochukuliwa ilikuwa inatumika kama makaburi au maeneo ya kuchomea maiti au kwa matumizi mengine mbali nay a kufaidika. Kanuni ya 10 ya Kanuni (Madai ya Fidia) za Ardhi, 2001 inaeleza kuwa fidia inapaswa kuwa ya fedha, lakini inaweza pia kutolewa kwa namna nyingine katika mfumo wa au katika mchanganyiko wa eneo la ardhi ya ubora saw ana ile iliyotwaliwa; jengo au majengo ya ubora unaofanana, na jingo au majengo yaliyotwaliwa; mime ana mazao; au utoaji wa nafaka na huduma nyingine za chakula kwa muda maalumu.

[288] Sheria ya Vijiji, Cap 114, section 4 (8), imeanza kutumika 1 Mei 2001.

[289] UNDRIP, art. 28.

[290] UNOHCHR, Muhtasari wa Sera na Mwandishi Maalumu wa Haki za Binadamu na Mazingira, “Mtazama unaozingatia haki za binadamu katika uhifadhi wa uoto wa asili: usawa, ufanisi na lazima,” Agosti 2021, https://www.ohchr.org/sites/default/files/Documents/Issues/Environment/SREnvironment/policy-briefing-1.pdf (accessed July 2, 2024), p. 20.

[291] ICCPR, art. 2.                                                                               

[292] ICCPR, art. 2(3).

[293] Tume ya Umoja wa Afrika, “Notisi ya Kuondolewa kwa Azimio lililotolewa chini ya kifungu 34(6) cha Itifaki ya Mkataba wa Afrika wa Kuanzishwa kwa Mahakama wa Afrika ya Haki za Binadamu na Watu,” Ref: BC/OLC/66/24/2565.19, Novemba 26, 2019, https://www.african-court.org/wpafc/wp-content/uploads/2020/10/Withdrawal-Tanzania_E.pdf (imepitiwa Julai 2, 2024); Itifaki ya Mkataba wa Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kuhusu Kuanzishwa kwa Mahakama wa Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, art. 34(6), wakati wowote baada ya kupitishwa kwa itifaki, nchi “itatoa tamko la kukubali uwezo wa Mahakama kupokea kesi chini ya kifungu 5(3) cha itifaki hii.” Mahakama haiwezi kupokea maombi kuhusu serikali ambazo hazijatoa tamko kama hilo.

[294] Ibid. art. 5(3), “Mahakama inaweza kuzipa haki Asasi Zisizo za Kiserikali (NGOs) zinazohusika zenye hadhi ya uangalizi mbele ya Tumen a watu binafsi kuanzisha kesi moja moja kwa mujibu wa ibara 34(6) ya Itifaki hii.”